Wajerumani wamefukia vitu vingi bongo ni wakati ule wa WWI, waliamini watarudi na kuzifukua. Attempt ya WWII ni moja ya jitihada hizo. Lakini wana ramani zote zenye mali. Vijana wengi wa kijerumani wanakuja kwa visingizio mbambali, lakini ukweli wanafuatilia mali hizo na huwa wana ramani na vielelezo vyote. Watafute hao watakufungulia. Makanisa ya Benedictine Fathers mkoani Ruvuma - Peramiho, Kigonsera, LItuhi, Litembo, Liparamba, Tingi, Ngadinda, Nangombo, Lundumato, Mpepo, Tingi, Mahanje, Mbangamao, nk. Kama unaweza kupenyeza maeneo hayo utapiga mali bila shaka. Vita ya kwanza mali nyingi ziko Lindi,Mtwara na Ruvuma hata Tabora unajua wale wajerumani walitokea Msumbiji baada ya kushinda. Pale Tabora Von Wismann aliwacharaza sana askari wa kiingereza 1916 akafanikiwa kukamata wamisionari wengi Waingereza na ali-loot mali zao zote. General Smuts toka South Africa akitokea Nyasaland kupitia Mbamba Bay ndipo wajerumani waliposambaratishwa na wakawa wanaficha mali hadi nyaraka zao wameficha.