Ukiona kitu kama pasi, stovu, sufuria vyenye alama ya minaz au simba au kichwa cha mtu aliyevaa kofia usikimbilie kwa mganga ni bora ukakichuku na kukihifadhi ktk mazingira mazur na kutafuta mtu anayejua mambo ya maficho ya kijerumani. Tatizo kubwa tulilo nalo watz ni kuwepo kwa matapeli wengi zaidi kuliko wahusika wenyewe. Na kwa sababu matapeli ni wengi wamesababisha watu kukosa iman na ukweli wa jambo hili.
Ukiona pango na ukaona sanduku/masanduku ndani ya pango hilo ukajaribu kupita ukaona aidha mtu au nyoka usitafute mganga wa kienyeji bali tafuta wataalam wanaohusika na mambo ya kale hasa ya kijeruman hao ndo wenye uwezo wa kuondoa mauza uza hayo na kuitoa mali hiyo.
Kitu cha kushauri hapa ni kuwa usipende sana kutafuta rupia maana ina mashart mengi zaidi kuliko mali nyingine ya mjerumani. Na ndo maana wengi waliohangaika kutafuta rupia walifilisika. Kama unatafuta rupia na ukaipata huyo uliyemkuta nayo unatakiwa ufuatilie kwanza je, ni ya kwake, ukoo wake au aliiba, au aliikota?