Hoja hupingwa kwa hoja, thibitisha kutokuwepo kwake kwa kuwa pasi na shaka umekili kwamba nimedhihirisha ya kwamba MUNGU yupo.
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote aliyeuumba ulimwengu huu, hayupo. Ni dhana potofu tu.
Ni dhana potofu kwa sababu ina contradiction. Contradiction ni kitu kujipinga chenyewe kwa namna ambayo haiwezekaniki kuwa katika uhalisi wa ukweli. Mathalani, nikisema pembetatu haiwezi kuwa duara na duara haliwezi kuwa pembetatu katika Euclidean geometry, halafu nikasema kuna pembetatu ambayo ni duara hapo hapo, katika Euclidean geometry, pembetatu hiyo ambayo ni duara hapo hapo haiwezi kuwepo, dhana ya kuwepo kwa hiyo pembetatu ambayo hapo hapo ni duara ina contradiction. Hivyo pembetatu duara hiyo haiwezi kuwepo.
Mungu naye ni kama pembetatu duara.
Upande mmoja tunaambiwa ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote (pembetatu). Upande mwingine tunaambiwa kauumba ulimwengu huu unaoweza kuwa na mabaya, licha ya ujuzi wake wote, uwezo wake wote na upendo wake wote (duara).
Kwa nini hakuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezi kutokea? Ulimwengiu huo ungekuwa logically consistent na upendo wake. Usingekuwa na contradiction.
Huu ulimwengu tunaouona, ambao mabaya yanaweza kutokea, unam contradict huyo Mungu.
Kuamini Mungu huyo yupo, ni sawa na kuamini kwamba kuna pembetatu ambayo hapo hapo ni duara katika Euclidean geometry planes.
Haipo, haiwezi kuwepo, kwa sababu ina an inherrent contradiction.
Mungu huyo naye hayupo kama hiyo pembetatu duara.
Kwa sababu dhana ya kuwepo kwake ina an inherrent contradiction.