Yeah ni kweli kabisa kutoweza kwako kuthibitisha hakuthibitishi kuwa Mungu yupo ila kunatoa jibu la kwamba kushindwa kuthibitisha uwepo wa Mungu hakufanyi kuwa hakuna Mungu.
Unanileta ninakotaka.
Ni kweli kwamba kushindwa kuthibitisha kitu hakufanyi kitu kisiwepo au kisiwe kweli.
Ila, ni kweli pia kwamba kitu ambacho hakipo, hakithibitishiki kuwa kipo, kwa sababu hakipo.
Mtoto wa miaka 15 anaweza kushindwa kuthibitisha kwamba baba yake mzazi, mwenye miaka 45, ni baba yake mzazi.
Kushindwa kwa huyu mtoto kuthibitisha kwamba baba yake mzazi ni baba yake mzazi, hakumfanyi baba yake mzazi asiwe baba yake mzazi.
Kwa hiyo, ni kweli, kushindwa kuthibitisha kitu tu, hakufanyi hicho ambacho hakijaweza kuthibitishwa kisiwe kweli.
Tatizo lako si tu umeshindwa kuthibitisha Mungu yupo tu, umeshindwa kuondoa contradiction pia.
Unakuwa kama mtu mwenye miaka 45, anayesema kwamba mtoto wa miezi mitatu ndiye mama yake mzazi aliyemzaa.
Akaombwa uthibitisho, akashindwa.
Huyu si tu kashindwa kuthibitisha, kashindwa kuthibitisha na kashindwa kuondoa contradiction.
Sasa far and above kuthibitisha tu kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote yupo.
Fanya hivi.
1. Thibitisha yupo
2. Ondoa contradiction ya problem of evil. Kama Mungu huyo yupo, kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanaweza kuwepo, wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezi kuwepo?