Makosa 10 aliyotenda Mungu

Makosa 10 aliyotenda Mungu

1536948978566.png
 
Amsamehe kakosa nini?
Unampa kichwa kwa mambo ya kijinga oho....isaya kama sjakosea 55:8 inasema mawazo yake ni bora zaidi yetu hata maono yake ni bora zaidi yetu.....sasa wew ni nani kukosoa aliekutengeneza
 
Magu alisema wale walioimba 'wana imani na nani sijui' angewatimua wote siku hiyo hiyo... Mimi nasema kama ningelikuwa Mungu pindi tu kidole chako kinabonyeza kitufe cha kupost hapo hapo ningekugeuza senene!!

Unafanya dhihaka kama hizi na bado uko hai! Aisee Mungu ana uvumilivu wa hali ya juu sana... Mwacheni Mungu aitwe Mungu!!
Akiachwa bado haitasaidia kupata majibu ya maswali yake haya 10.Muhimu kutafuta majibu ya haya maswali kwanza.Kama wewe unamwamini na unamjua jibu basi hata baadhi au yote.Sasa nyie binadamu ndio mnamlinda Mungu badala ya kuacha Mungu awalinde nyie.Jibu hoja mkuu sio kumlinda Mungu hata kama ni hoja nzima basi wewe unakataza asihojiwe kwa kusema ni dhihaka.
 
Hiyo kuielewa vizuri mpaka usome Albert Einstein's Relativity halafu ufuatilie malumbano ya Einstein na Niels Bohr.

Halafu umfuatilie Einstein alipoanzia mpaka yalipomshinda. Umsome Bohr naye Copenhagen interpretation. Uwasome Heisenberg, Schrodinger, Dirac, Fermi, Oppenheimer, Wheeler, Everett, Pauli, Feynman, Hawkings, Penrose et cetera. Na malumbano yao wote.

Sasa watu wanabisha wengine hata hayo majina hawayajui.

Licha ya kuwasoma na kujua dunia inaendaje.

Shida sana kubishana kwa fact hapo.
Hivi ni kweli kwamba kujua kama Mungu yupo au hayupo ni mpaka mtu ajue hayo majina?

Hivi kumshukuru (kumwabudu) Mungu na/au kumkufuru (kutokumwabudu) inahitaji mtu mpaka asome hayo uliyoyataja?

Mungu aliweka kila kitu kwa kiwango maalum na ukomo fulani; haikuwa coincidentally bali anajua tu kuwa "Kuchamba sana..."
 
Unampa kichwa kwa mambo ya kijinga oho....isaya kama sjakosea 55:8 inasema mawazo yake ni bora zaidi yetu hata maono yake ni bora zaidi yetu.....sasa wew ni nani kukosoa aliekutengeneza
Hakuna ujinga hapo.Kama unataka kuwa Mtumishi bora ni lazima uwe na majibu hayo pia.Hayo majibu yote yapo kwenye Bible hivyo apatikane mtu sahihi ajibu kumsaidia mleta mada.Wewe hujui hayo majibu na bado unakataza mjadala usiwepo humu,je hutaki kujifunza kutoka majibu ya wanaojua?

Usimlinde Mungu ,muache Mungu akulinde wewe.
 
Hiyo kuielewa vizuri mpaka usome Albert Einstein's Relativity halafu ufuatilie malumbano ya Einstein na Niels Bohr.

Halafu umfuatilie Einstein alipoanzia mpaka yalipomshinda. Umsome Bohr naye Copenhagen interpretation. Uwasome Heisenberg, Schrodinger, Dirac, Fermi, Oppenheimer, Wheeler, Everett, Pauli, Feynman, Hawkings, Penrose et cetera. Na malumbano yao wote.

Sasa watu wanabisha wengine hata hayo majina hawayajui.

Licha ya kuwasoma na kujua dunia inaendaje.

Shida sana kubishana kwa fact hapo.
Tatizo lako wakati mwingine unapenda sifa zisizo na ulazima

Sasa dhana ndogo tu ya kwamba time is illusion

Basi mpaka ukusanye msururu wa majina ya marehemu wasiojielewa..!

Tena wajuzijuzi Tu......!

Wakati kuna watu wa kidini wa kawaida tu ambao wanaamini

Mungu wao akisema kitu 'kuwa'
Kinatokea papo hapo bila chenga

Nayo hiyo utasemaje.!?

Kwamba kati ya watu hawa walioishi zama za Giza na marehemu wako wewe

Ni nani wa kwanza kujua dhana hiyo ya kwamba Muda ni Madogoli Tu si lolote na si chochote.....!?
 
Kwanza hoji imekuaje wewe ukaja duniani bila hiyari yako, ukishapata jibu ndipo uje kuuliza kwanini hizo shida na matatizo yanawapata watu?, pia usisahau kujiuliza raha na starehe pia wanazokula "matajiri".😁😁
Logical non sequitur that contradicts God's omni benevolence and freewill.

Najua hujaelewa hoja, sitegemei uweze kuijibu.
 
Kama unaona sijajibu ulichouliza basi pengine ni kutokana na kukosea kwako kukosea kuuliza,lichunguze vizuri swali lako.
Huna nia ya kuelewa nilichouliza wala kujibu swali.

Ungekuwa na nia hizo, ungekuwa na utashi zaidi.
 
Hivi ni kweli kwamba kujua kama Mungu yupo au hayupo ni mpaka mtu ajue hayo majina?

Hivi kumshukuru (kumwabudu) Mungu na/au kumkufuru (kutokumwabudu) inahitaji mtu mpaka asome hayo uliyoyataja?

Mungu aliweka kila kitu kwa kiwango maalum na ukomo fulani; haikuwa coincidentally bali anajua tu kuwa "Kuchamba sana..."
Hujaelewa hata hoja, ndiyo maana unaleta a priori fallacy.
 
Tatizo lako wakati mwingine unapenda sifa zisizo na ulazima

Sasa dhana ndogo tu ya kwamba time is illusion

Basi mpaka ukusanye msururu wa majina ya marehemu wasiojielewa..!

Tena wajuzijuzi Tu......!

Wakati kuna watu wa kidini wa kawaida tu ambao wanaamini

Mungu wao akisema kitu 'kuwa'
Kinatokea papo hapo bila chenga

Nayo hiyo utasemaje.!?

Kwamba kati ya watu hawa walioishi zama za Giza na marehemu wako wewe

Ni nani wa kwanza kujua dhana hiyo ya kwamba Muda ni Madogoli Tu si lolote na si chochote.....!?
Kuna watu wanafuatilia hizi habari wanashukuru mimi kuandika hayo majina wanapata pa kuanzia.

Hujathibitisha Mungu yupo.

Na kwa kuwa unaniona nataka sifa, basi naondoka kwenye mjadala nisije kufikiriwa najadili kwa kutafuta sifa.

Peace out!
 
Kuna watu wanafuatilia hizi habari wanashukuru mimi kuandika hayo majina wanapata pa kuanzia.

Hujathibitisha Mungu yupo.
Dhana ya wachawi kupaa na ungo kwa speed isiyomithilika Tunayo karne kwa makarne

We utulishe Matango pori Eti kepler, enstien ndio wa kwanza..!

Wakati wamekopi.!?

Kuhusu Mungu sina mda wa kuthibitisha

Kwanza neno lenyewe Mungu linautata wa kurejelewa kwa maana Nyingi

Ukitaja neno Mungu bila ufafanuzi ni sawasawa na Bure
 
Dhana ya wachawi kupaa na ungo kwa speed isiyomithilika Tunayo karne kwa makarne

We utulishe Matango pori Eti kepler, enstien ndio wa kwanza..!

Wakati wamekopi.!?

Kuhusu Mungu sina mda wa kuthibitisha

Kwanza neno lenyewe Mungu linautata wa kurejelewa kwa maana Nyingi

Ukitaja neno Mungu bila ufafanuzi ni sawasawa na Bure
Wapi nimesema Einstein au Kepler ni wa kwanza?

Unaweza kunionesha?

Au ni utoko na ukoko ulio kichwani mwako tu?
 
Back
Top Bottom