Makosa 10 aliyotenda Mungu

Makosa 10 aliyotenda Mungu

Kibaya zaidi huyo mungu haiwezi kujithibitisha kwa watu mpaka atumie mtu

Alishindwa kuumba ulimwengu ambao watu wangemjua bila kutumia mtu mwengine?

Kwanini kumjua mungu mpaka amtume mtu ?

Hapo ndipo utaona huyo mungu ni hadithi
Jamaa una hoja za kitoto kichizi,yani kwa hiyo hoja yako maana yake basi hata haya majadiliano hayana maana.
 
Eti unaambiwa kujua neno la Mungu mpaka ujue Kiarabu, utafsiri mambo kutoka Kirabu.

Au ujue Kiyahudi. Utafsiri mambo kutoka Kiyahudi.

Huyo Mungu mbona kawatenga Wadigo hivyo?

Alishindwa kumshushia neno lake kila mtu katika namnanisiyo na shaka kwenye DNA?
Kwani huyo Mungu ana shida gani hadi afanye hivyo unavyofikiri wewe? Hebu tueleze ni manufaa gani zaidi angefaidika nayo kwa kufanya hivyo? Maana inaonesha hivi sasa kwa jinsi ilivyo hapati faida sana anapata hasara.
 
Hapajawahi kutokea manabii au mitume walioandikwa ktk quran au bible kutoka nje ya wayahudi au warabu

Kwanini nchi nyingine kama China Hindus au wazungu hakuna walioandikwa ktk vitabu hivyo

Hivi huyo mungu kweli atakuwa anayo busara kweli?
Kwahiyo imani ya Mungu ilienea vp ulimwenguni kote? Mfano tunajua china wana imani zao tofauti na uislamu na ukristo ila imani ya Mungu ipo kuendana na imani zao,unadhani hili wazo la kuamini Mungu lilianzia wapi na kusambaa ulimwenguni kote?
 
Hapo ndipo utakapoona hivyo vitabu si vitabu vitakatifu vya Mungu.

Ni vitabu vya watu, vilivyoandikwa kufuata muktadha wa tamaduni zao.

Nilikuwa nasoma kitabu cha Karl Evanzz, kinaitwa "The Messenger: The Rise Aand Fall of Elijah Muhammad".

Elijah Muhammad ni founder wa "The Nation of Islam", kundi la Waislamu wa Marekani ambao walikuwa na muamko mkubwa wa kisiasa na kupinga maovu mengi ya serikali ya Marekani, kundi hili ndilo lilimtoa Malcolm X na kum seduce Muhammad Ali mpaka akabadilisha dini.

Kuna sehemu Elijah Muhammad alikuwa anagombana na watu wa Orthodox Islam, wa Sunni, kutokana na mambo yake yaliyo controversial, kwa kutumia jina la Uislamu.

Elijah Muhammad akawaambia ma Sheikh wale wa Sunni kwamba, kama mnataka kuniletea habari za kutaka kunitawala, nitawaambia mamilioni ya Waislamu wanaonifuata mimi huku Marekani, waache kuswali huku waki face Mecca, wote wanze kuswali waki face Chicago, makao makuu ya Nation of Islam Marekani. Kwa sababu hata katika Uislamu kabla ya kwatu kuswali wakielekea Mecca, walikuwa wanaswali kuelekea Jerusalem, tutabadilisha tu.

Wwale ma Sheikh wakampoza, wakendelea naye uzuri, mpaka leo Natiuon of Islam misikiti yao wanaswali kuelekea Al-Qqabr Mecca.

Hili jambo linaonesha kwamba hizi habari ni tamaduni tu watu wanajiwekea.

Tena ni utumwa wa kimawazo.

Ukishaambiwa Mungu kashusha Quran kwa Waarabu, na ukisali lazima uelekee Mecca, automatically unajitoa utu wako, na kujiona wewe hufai, kwenu hakufai, lugha yako haifai.

Kiarabu ndicho kinafaa, Mecca ndiko kunafaa.

Kama wewe ungekuwa unafaa, kwa nini Al-Qqabr isingekuwa kwenu? Kama lugha yenu inafaa, kwa nini Mungu hakushusha Quran au Biblia kwa lugha yenu?

Ni utumwa wa kiutama duni tu.
Unapinga dini unatetea uzalendo na utamaduni,si yale yale tu.
 
Kwani huyo Mungu ana shida gani hadi afanye hivyo unavyofikiri wewe? Hebu tueleze ni manufaa gani zaidi angefaidika nayo kwa kufanya hivyo? Maana inaonesha hivi sasa kwa jinsi ilivyo hapati faida sana anapata hasara.
Unaelewa kwamba hivi ni zaidi na ninavyofikiri mimi?

Unaelewa kwamba hivi ni logical consistency?

Unaelewa kwamba dhana ikikosa kuwa na simpe logical consistency hivi huwezi kusema inaweza kuwepo nje ya dhana, seuze kuwa Mungu mjuzi wa yote?

Unauliza Baba mwenye mapenzi na watoto wake atapata manufaa gani akiamua kutowachoma visu na kuwaua hao watoto wake?

Thibitisha Mungu yupo.
 
Kwahiyo imani ya Mungu ilienea vp ulimwenguni kote? Mfano tunajua china wana imani zao tofauti na uislamu na ukristo ila imani ya Mungu ipo kuendana na imani zao,unadhani hili wazo la kuamini Mungu lilianzia wapi na kusambaa ulimwenguni kote?


Soma vizuri hoja yangu kwanini mitume wote watoke mashariki ya kati?
 
Unaelewa kwamba hivi ni zaidi na ninavyofikiri mimi?

Unaelewa kwamba hivi ni logical consistency?

Unaelewa kwamba dhana ikikosa kuwa na simpe logical consistency hivi huwezi kusema inaweza kuwepo nje ya dhana, seuze kuwa Mungu mjuzi wa yote?

Unauliza Baba mwenye mapenzi na watoto wake atapata manufaa gani akiamua kutowachoma visu na kuwaua hao watoto wake?

Thibitisha Mungu yupo.
Haujajibu nilichouliza,nijibu nilichouliza kwani kuna ugumu gani?

Elezea ni faida zipi angepata kwa kufanya hivyo au hasara zipi anapata kwa hali kuwa hivi ilivyo sasa?
 
Soma vizuri hoja yangu kwanini mitume wote watoke mashariki ya kati?
Kwa hiyo hoja yako ndio maana nikauliza swali ilikuaje imani ya Mungu ikaenea duniani kote ikiwa watu waliyokuwa wakiongelea habari za Mungu walikuwa wanatoka eneo moja tu? Hebu tujadili hili.
 
Wapi nimetetea uzalendo na utamaduni?

Unaweza kunionesha sentensi niliyotetea uzalendo na utamaduni?

Unajua kusoma wewe?

"Ukishaambiwa Mungu kashusha Quran kwa Waarabu, na ukisali lazima uelekee Mecca, automatically unajitoa utu wako, na kujiona wewe hufai, kwenu hakufai, lugha yako haifai.



Kiarabu ndicho kinafaa, Mecca ndiko kunafaa.



Kama wewe ungekuwa unafaa, kwa nini Al-Qqabr isingekuwa kwenu? Kama lugha yenu inafaa, kwa nini Mungu hakushusha Quran au Biblia kwa lugha yenu?



Ni utumwa wa kiutama duni tu."

Kama ulivyomalizia hapo mwisho kwamba ni utumwa wa kiutamaduni tu,kwa maana watu wangekuwa na uzalendo na kupenda tamaduni zao basi wasingefuata hizo dini ambazo unaona zimejaa tamaduni za watu wengine.
 
Na hapo ndipo utakapoona, Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, hayupo.

Angekuwepo, asingeumba ulimwengu ambao viumbe wake wanakufa kila siku.

Kuumba hivyo, wakati anaweza kuumba ulimwengu ambao kifo hakiwezekani, ingekuwa kuwafanyia viumbe wake roho mbaya.

Na Mungu huyo, by definition, hana roho mbaya.
Kiranga mungu hayupo na huyu wanaemsimulia ni mpuuzi kuliko au mzembe sana na kiumbe cha makusudi sana na kibaya kuliko ka ni kweli kipo
 
Maana sifa za maandiko yake walizotusimulia inaonesha mungu ndo mdhaifu kuliko kiumbe chochote ana uwezo wote nguvu zote upendo wote Ila hawezi Ku control chochote mfano Bible tu inathibitisha udhaifu wake kuna kipindi cha Exodus Mungu alitaka kufanya maamuzi ya hovyo kabisa akashauriwa na musa na kubadili mawazo yake ok unajiuliza je huyu nd muweza wa yote?
 
Kiranga mungu hayupo na huyu wanaemsimulia ni mpuuzi kuliko au mzembe sana na kiumbe cha makusudi sana na kibaya kuliko ka ni kweli kipo

Watu wanajiondoa akili tu,kwa uvivu, kwa ujinga, kwa woga, kwa cognitive dissonance, kwa logical non sequitur, kwa deus ex machina, kwa tradition, kwa vitu viiingi, ili mradi Mungu huyu awepo tu.

Maana maisha yao yote yanazunguka habari za Mungu huyo kuwepo.

Hata wakijua ukwelikwamba hayupo, watabisha.

Leo nilikuwa nasikia habari BBC World Service, kuna Jumuiya ya Wajapani ilihamia South America, Brazil huko ndanindani.

Japan kulikuwa kunajaa watu, watu wakaenda Peru na Brazil.

Basi kuna watu wakasikia Japan imepiga, imeshindwa katika vita vikuu vya pili.

Jumuiya ya Kijapani ikakataa ukweli huo,ikawa inawaita wanachama wake, inawauliza, Japan imeshindwa?

Ukisemaimeshindwa, Jumuiya inakutenga, unatumiwa barua za vitisho, unaonekana huna uzalendo.

Kwa Jumuiya hii, kitu muhimu ilikuwa si ukweli,kamaingekuwa kitu muhimuni ukweli, kujua ukweli ilikuwa kazi rahisi kabisa.

Kwa jumuiya hii, kitu muhimu ilikuwa ni imani kwamba Japan haiwezi kushindwa kitu.

Kwa hivyo, imani ikawa muhimu kuliko ukweli.

Kwao, Japan haiwezi kushindwa.

Sasa na hapa, naona habari hizo hizo. Kuchambua ukweli kuhusu uwepo wa Mungu si kitu muhimu.

Watu wanatakakulazimisha Mungu yupo, kwa imani tu.

Ndio wale wale tu wanaosema "Japan haiwezi kushindwa". Wanasema "Mungu wa milele lazima awepo".

Pathetic!
 
Maana sifa za maandiko yake walizotusimulia inaonesha mungu ndo mdhaifu kuliko kiumbe chochote ana uwezo wote nguvu zote upendo wote Ila hawezi Ku control chochote mfano Bible tu inathibitisha udhaifu wake kuna kipindi cha Exodus Mungu alitaka kufanya maamuzi ya hovyo kabisa akashauriwa na musa na kubadili mawazo yake ok unajiuliza je huyu nd muweza wa yote?
Eti Mungu anaumba, anakuwa hapendezwi na alivyoumba, anakasirika, anaghairi, anatakakuua kuanziawatu waliomkose, mpakawanyama wasio na ujuziwa mema na mabaya.

Huyu Mungu au Idi Amin?
 
Watu wanajiondoa akili tu,kwa uvivu, kwa ujinga, kwa woga, kwa cognitive dissonance, kwa logical non sequitur, kwa deus ex machina, kwa tradition, kwa vitu viiingi, ili mradi Mungu huyu awepo tu.

Maana maisha yao yote yanazunguka habari za Mungu huyo kuwepo.

Hata wakijua ukwelikwamba hayupo, watabisha.

Leo nilikuwa nasikia habari BBC World Service, kuna Jumuiya ya Wajapani ilihamia South America, Brazil huko ndanindani.

Japan kulikuwa kunajaa watu, watu wakaenda Peru na Brazil.

Basi kuna watu wakasikia Japan imepiga, imeshindwa katika vita vikuu vya pili.

Jumuiya ya Kijapani ikakataa ukweli huo,ikawa inawaita wanachama wake, inawauliza, Japan imeshindwa?

Ukisemaimeshindwa, Jumuiya inakutenga, unatumiwa barua za vitisho, unaonekana huna uzalendo.

Kwa Jumuiya hii, kitu muhimu ilikuwa si ukweli,kamaingekuwa kitu muhimuni ukweli, kujua ukweli ilikuwa kazi rahisi kabisa.

Kwa jumuiya hii, kitu muhimu ilikuwa ni imani kwamba Japan haiwezi kushindwa kitu.

Kwa hivyo, imani ikawa muhimu kuliko ukweli.

Kwao, Japan haiwezi kushindwa.

Sasa na hapa, naona habari hizo hizo. Kuchambua ukweli kuhusu uwepo wa Mungu si kitu muhimu.

Watu wanatakakulazimisha Mungu yupo, kwa imani tu.

Ndio wale wale tu wanaosema "Japan haiwezi kushindwa". Wanasema "Mungu wa milele lazima awepo".

Pathetic!
Kuna kitu kinatuua kinaitwa indoctrination yaani tumekua indoctrinated kiasi cha kwamba hatuwezi fikiria chochote ila kukubali tu
 
Rapid Tranquilizer Yesu alitoa mfano wa watu aliowapa talanta, kila mmoja akatakiwa kurudisha kwa alivyopewa.

The moralof the story is, with great power, comes great responsibility.

Nashangaa huyu Mungu wanampa great power bila responsibility.
 
Back
Top Bottom