Hapajawahi kutokea manabii au mitume walioandikwa ktk quran au bible kutoka nje ya wayahudi au warabu
Kwanini nchi nyingine kama China Hindus au wazungu hakuna walioandikwa ktk vitabu hivyo
Hivi huyo mungu kweli atakuwa anayo busara kweli?
Hapo ndipo utakapoona hivyo vitabu si vitabu vitakatifu vya Mungu.
Ni vitabu vya watu, vilivyoandikwa kufuata muktadha wa tamaduni zao.
Nilikuwa nasoma kitabu cha Karl Evanzz, kinaitwa "The Messenger: The Rise Aand Fall of Elijah Muhammad".
Elijah Muhammad ni founder wa "The Nation of Islam", kundi la Waislamu wa Marekani ambao walikuwa na muamko mkubwa wa kisiasa na kupinga maovu mengi ya serikali ya Marekani, kundi hili ndilo lilimtoa Malcolm X na kum seduce Muhammad Ali mpaka akabadilisha dini.
Kuna sehemu Elijah Muhammad alikuwa anagombana na watu wa Orthodox Islam, wa Sunni, kutokana na mambo yake yaliyo controversial, kwa kutumia jina la Uislamu.
Elijah Muhammad akawaambia ma Sheikh wale wa Sunni kwamba, kama mnataka kuniletea habari za kutaka kunitawala, nitawaambia mamilioni ya Waislamu wanaonifuata mimi huku Marekani, waache kuswali huku waki face Mecca, wote wanze kuswali waki face Chicago, makao makuu ya Nation of Islam Marekani. Kwa sababu hata katika Uislamu kabla ya kwatu kuswali wakielekea Mecca, walikuwa wanaswali kuelekea Jerusalem, tutabadilisha tu.
Wwale ma Sheikh wakampoza, wakendelea naye uzuri, mpaka leo Natiuon of Islam misikiti yao wanaswali kuelekea Al-Qqabr Mecca.
Hili jambo linaonesha kwamba hizi habari ni tamaduni tu watu wanajiwekea.
Tena ni utumwa wa kimawazo.
Ukishaambiwa Mungu kashusha Quran kwa Waarabu, na ukisali lazima uelekee Mecca, automatically unajitoa utu wako, na kujiona wewe hufai, kwenu hakufai, lugha yako haifai.
Kiarabu ndicho kinafaa, Mecca ndiko kunafaa.
Kama wewe ungekuwa unafaa, kwa nini Al-Qqabr isingekuwa kwenu? Kama lugha yenu inafaa, kwa nini Mungu hakushusha Quran au Biblia kwa lugha yenu?
Ni utumwa wa kiutama duni tu.