Makosa 10 aliyotenda Mungu

Makosa 10 aliyotenda Mungu

Hujaweza kuthibitisha Mungu yupo kw njia iliyo na logical consistency.

Habari zako za Mungu kuwepo zina contradiction.

Hapa mnatuambia Mungu yupo, ana ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote, ana haki kuu.

Pale mnatuambia kaleta gharika ya mafuriko imeua kuanzia vitoto vichanga visivyojua alif wala be, mpaka vinyama visivyo na akili ya kujua mazuri na mabaya.

Huyo Mungu yupo kweli au tunapigana kamba tu?
Kwa nini unataka uthibitishiwe Mungu yupo wakati unadai Mungu hayupo?
 
Huwezi kuwa na mizani kama unakubali contradiction.

Utapimaje wapi kumezidi wapi wakati kulikozidi kunaweza kuzidiwa na kulikozidiwa?

Kama unakubali contradiction, kilo 50 zinaweza kuwa nzito zaidi ya kilo 100.

Sasa hapo utapimaje uzito kujua wapi kuna uzito zaidi?
Bro unapenda sana kupoteza muda na kutoa mifano isiyo na uhalisia. Hakuna utata wowote kuhusu suala la kilo 50 na kilo 100.

Weka vitu vya maana,na itabidi nikupe elimu ya kutoa mifano.
 
Kwa nini unataka uthibitishiwe Mungu yupo wakati unadai Mungu hayupo?
Swali zuri sana,hawa huwa hawawezi kufikiri kinyume na wanavyofikiri. Na ukiwaminya kuwaambia wafikiri kinyume unazidi kuwaumiza.

Wana hoja dhaifu kuliko udhaifu wa nyumba ya BUI BUI.


Asante sana !
 
Wwewe jifunze kusoma kwanza, tafuta mwalimu wa logic akufundishe truth table ni nini, p ni nini, negation ya p ni nini, tautology ni nini, contradiction ni nini, fallacy ni nini.

Halafu ni jinsi gani unaweza kuivunja sentensi ukaipitisha katika truth table.

Halafu, ukimaliza somo hilo, njoo tujadiliane tena hapa.

Kwa sasa naona naweza kubishana na ngumbaru asiyejua kusoma.

Pata darasa la bure hapa kuhusu Truth Table, Boolean Aalgebra, Venn Diagram etc


Bro una yumba kinoma noma !
 
Bro unapenda sana kupoteza muda na kutoa mifano isiyo na uhalisia. Hakuna utata wowote kuhusu suala la kilo 50 na kilo 100.

Weka vitu vya maana,na itabidi nikupe elimu ya kutoa mifano.
Huyu Kiranga ni mweupe sana kichwani huwa hawezi kujenga na kupangua hoja, anachojua yeye kuruka ruka tu kutoka mada moja kwenda nyingine ambazo napo ukimfuata hukohuko unamkuta pia ni mweupe akiona umemzidi zaidi anarudi kwa Id nyingine .
 
Huyu Kiranga ni mweupe sana kichwani huwa hawezi kujenga na kupangua hoja, anachojua yeye kuruka ruka tu kutoka mada moja kwenda nyingine ambazo napo ukimfuata hukohuko unamkuta pia ni mweupe akiona umemzidi zaidi anarudi kwa Id nyingine .
Mimi nimeamua kuanza kiwafundisha sasa. Ni juu yao kuuchukua ukweli au kuuacha.

Bro ukweli kitu cha ajabu sana,huwezi kushindana na ukweli hata sikumoja.

Hawa jamaa ni wagonjwa wa AKILI.
 
Hahahaha,naona unaelekea kule ninapo pataka. Kwa maana baba na mama angu mchakato wao utakuwa ni hivyo hivyo kama nilivyopatikana mimi. Kama hali iko hivyo wa mwanzo wetu ni nani ?
Mkuu, haiwezekani wa mwanzo akawepo bila wewe kuwepo. Hebu fikiria wewe usingekuwepo kabisa, huyo wa mwanzo angekuwepo kwa namna gani? Kimsingi, bila wewe kuwepo, hakuna huo mwanzo, haujakaa kuwepo na hautakaa kuwepo.

Kila uonacho kipo ni kwa sababu wewe upo. Usipokuwepo, hakuna kilichopo. Hakuna Mungu, hakuna ukweli kuwa ulikuwepo, hakuna kifo chako. Hakuna huo uusemao mwanzo. Hakuna maumivu yaliyosababisha kifo chako. Kimsingi, hakuna huo mwanzo, hakuna kilichowahi kuwepo na hakuna kitakachowahi kuwepo. Sababu ni moja tu. Haupo.

Hali ya kuwepo kwako ndio mwanzo wa kuwepo kila kitu. Hadi huo mwanzo unaoufikiria kuwa ulikuwepo, upo na unaweza kuuwaza kwa kuwa upo.

Hebu jaribu kukumbuka katika hali ya kutokuwepo kwako kama Mungu na huo mwanzo vilikuwepo. Hukujua uwepo wa Mungu. Hukujua uwepo wa huo mwanzo. Yani, kabla ya kuwepo kwako, kwa ufupi, hakuna kilichokuwepo na kama ungeendelea na hali ya kutokuwepo, kamwe kusingekaa kuwepo kwa kitu, ukiwemo huo mwanzo unaofikiri unaweza kuwepo bila wewe kuwepo.

Bila shaka nipo ulipotaka nifike.
 
Kwa hiyo una kataa uwepo wa Mungu kisa watu wanakufa?

Hujui kwamba nafsi zina sifa kuu/phases tatu ,ambao ni kuzaliwa ,kuishi na kufa, na lazima zipitie phases zote tatu.
Kufahamu hivyo unahitaji Mungu mkuu? Au kufahamu kuwa viumbe vinahitaji kuthaminiwa tunahitaji Mungu? Ndio maana ninasema Mungu ni ukomo wa kufikiri. Kwa nini kama tunafahamu kuwa kifo ni miongoni mwa hatua za msingi katika maisha, tunaingiza katika hili propaganda za Mungu kampenda zaidi? Mara mchungaji fulani anafufua na hicho kinakuwa miongoni mwa vigezo vya kujipatia wafuasi nyomi?

Yani kwa kuwa hakuna namna watu wanafahamu ni lini watakufa, basi mazingira kama haya ndio ati yanathibitisha kuwa kuna Mungu. Ilihali kwa sasa unakiri kuwa kifo ni sehemu ya hatua za kiumbe hai. Ni lazima afe. Ila kwa kuwa hstujui siku wala SAA, hapa ndipo Mungu anapoingia.

He, tukisema huyu Mungu ndiye anayesababisha hizi ajali kama za kuzama kwa kivuko, au ajali za ndege, magari, mabasi, aliweka magonjwa n.k utabisha? Je, huyu ndiye Mungu wa upendo au ndiye Mungu mkatili kuliko kitu chochote kile?

Tuache sasa kusimamia ukweli kuwa kivuko kuzama ni uzembe wa watu kwa kushindwa kusimamia taratibu na ukweli kuwa kilistahili kubeba watu mia tu? Ndio tuseme mipango ya Mungu haikiukwi? Alishapanga hivyo na ilipaswa kuwa hivyo? Elewa ninaposema Mungu ni ukomo wa kufikiri, unielewe basi. Ni kichaka cha kupata majibu mepesi kwenye maswali magumu.

Eti pale uwezo wa binadamu unapoishia, ndio Mungu anaanzia hapo. Kwamba, kadiri uwezo wetu unapoongezeka, kwa maana ya kupata ufumbuzi wa changamoto, basi tunasogeza mbele uwezo wa Mungu. Huoni uwezo wa Mungu ndio huo uwezo wa binadamu tu?

Kwanza ukichunguza kwa making utakuja kuona kuwa uwepo wa Mungu unategemea sana uwepo wa vitu na hususani vile ambavyo, katika wakati fulani binadamu amekosa majibu wa kwa nini vipo namna hiyo. Kimojawapo ni muda we kufa.

Vitu vingine ni mwanzo wa kila kiumbe, mwonekano wa kipekee wa vitu kama milima, water bodies. Kwa mfano pale bahari mbili zinapokutana. Yani ni muujiza, na hapo tunasema kweli mwache Mungu aitwe Mungu!
 
Kufahamu hivyo unahitaji Mungu mkuu? Au kufahamu kuwa viumbe vinahitaji kuthaminiwa tunahitaji Mungu? Ndio maana ninasema Mungu ni ukomo wa kufikiri. Kwa nini kama tunafahamu kuwa kifo ni miongoni mwa hatua za msingi katika maisha, tunaingiza katika hili propaganda za Mungu kampenda zaidi? Mara mchungaji fulani anafufua na hicho kinakuwa miongoni mwa vigezo vya kujipatia wafuasi nyomi?

Yani kwa kuwa hakuna namna watu wanafahamu ni lini watakufa, basi mazingira kama haya ndio ati yanathibitisha kuwa kuna Mungu. Ilihali kwa sasa unakiri kuwa kifo ni sehemu ya hatua za kiumbe hai. Ni lazima afe. Ila kwa kuwa hstujui siku wala SAA, hapa ndipo Mungu anapoingia.

He, tukisema huyu Mungu ndiye anayesababisha hizi ajali kama za kuzama kwa kivuko, au ajali za ndege, magari, mabasi, aliweka magonjwa n.k utabisha? Je, huyu ndiye Mungu wa upendo au ndiye Mungu mkatili kuliko kitu chochote kile?

Tuache sasa kusimamia ukweli kuwa kivuko kuzama ni uzembe wa watu kwa kushindwa kusimamia taratibu na ukweli kuwa kilistahili kubeba watu mia tu? Ndio tuseme mipango ya Mungu haikiukwi? Alishapanga hivyo na ilipaswa kuwa hivyo? Elewa ninaposema Mungu ni ukomo wa kufikiri, unielewe basi. Ni kichaka cha kupata majibu mepesi kwenye maswali magumu.

Eti pale uwezo wa binadamu unapoishia, ndio Mungu anaanzia hapo. Kwamba, kadiri uwezo wetu unapoongezeka, kwa maana ya kupata ufumbuzi wa changamoto, basi tunasogeza mbele uwezo wa Mungu. Huoni uwezo wa Mungu ndio huo uwezo wa binadamu tu?

Kwanza ukichunguza kwa making utakuja kuona kuwa uwepo wa Mungu unategemea sana uwepo wa vitu na hususani vile ambavyo, katika wakati fulani binadamu amekosa majibu wa kwa nini vipo namna hiyo. Kimojawapo ni muda we kufa.

Vitu vingine ni mwanzo wa kila kiumbe, mwonekano wa kipekee wa vitu kama milima, water bodies. Kwa mfano pale bahari mbili zinapokutana. Yani ni muujiza, na hapo tunasema kweli mwache Mungu aitwe Mungu!
Pointi yako ya msingi ni ipi?
 
Kila mtu anazaliwa akiwa hajui kitu/mjinga.

Mazingira tunayoishi ,vyakula tunavyokula na elimu tunayoipata ndizo zinatufanya tujue vitu mbalimbali/tuondoe ujinga.
Kwa nini unafikiri Mungu mweza wa kila kitu alipanga kutuumba katika hali hii? Unafikiri kwa nini hakutuwezesha kutambua haya ikiwemo kumtambua yeye (werevu) kabla ya kuwepo kwetu?
 
Sasa na wewe hauoni kuwa unajipumbaza kwa kusema hakuna Mungu kisa tu kuna watu wanatumia vibaya imani ya uwepo wa Mungu?
Hapana. Namna watu wanavyotumia vibaya dhana ya Mungu ni sehemu ya uthibitisho kuwa hakuna kitu kama hicho. Ndio kama hivyo inavyofahamika wazi kuwa kifo ni sehemu ya lazima ya mwanadamu lakini kinatumika kama sehemu ya uthibitisho was uwepo wake Mungu, sawasawa na hali ya kuishi. So utasikia watu wanasema kuishi ni kwa neema ya Mungu tu? Na wakati huo huo pia kufa ni kwa mapenzi yake? Unaweza kuona mkanganyiko huu ukivyo.
 
Msijipe tabu sana huyo Otolung'anyi ndio Kiranga mwenyewe ameona anaanza kushindwa akaamua kuja kwa ID nyingine ili akwepe aibu.
Ama kweli wewe ndiye unayethibitisha kuwa umeishiwa hoja na unashindwa vibaya sana. Sasa na Mimi nikisema wewe ndiye huyohuyo Tz mbongo na wengine wote walio against hoja ya kiranga nitakuwa nimekosea?
 
Hapana. Namna watu wanavyotumia vibaya dhana ya Mungu ni sehemu ya uthibitisho kuwa hakuna kitu kama hicho. Ndio kama hivyo inavyofahamika wazi kuwa kifo ni sehemu ya lazima ya mwanadamu lakini kinatumika kama sehemu ya uthibitisho was uwepo wake Mungu, sawasawa na hali ya kuishi. So utasikia watu wanasema kuishi ni kwa neema ya Mungu tu? Na wakati huo huo pia kufa ni kwa mapenzi yake? Unaweza kuona mkanganyiko huu ukivyo.
Hakuna mkanganyiko hapo,nafsi inazaliwa,inaishi na kufa.
 
Hakuna mkanganyiko hapo,nafsi inazaliwa,inaishi na kufa.
Sasa tuishi maisha ya uhalisia kwa namna hiyo. Kushindwa kuelezea kwa uhakika mwanzo wa binadamu ni moja ya uthibitisho kuwa kuna Mungu. Tunamuhitaji Mungu kuelewa kuwa tulizaliwa? Au ili tuishi tuna mahitaji ya msingi? Na kwamba kiumbe hai ipo siku lazima kitapoteza uhai, tunamuhitaji Mungu katika haya? Tunamuhitaji Mungu ili tujue kuwa tunapaswa kuishi kwa amani na upendo? Hakika tunajihitaji mwenyewe katika kila jambo.
 
Nimepitia huu uzi nimegundua kuwa watu wachache tu hapa ndio wana "reason".

Ila wengi ni watu wasio na reason na chochote watakachoambiwa " In the name of God" hata kiwe kisichokuwa na mashiko basi wao watashikilia hivyo hivyo bila kuhoji kwanini iwe hivyo?

Ubaya mkubwa zaidi ni kuwa hao wengi ambao hawataki kuhoji mioyoni mwao wanahoji na wanakubaliana kabisa na hizi facts za mleta mada na Kiranga

Tatizo ule unafki wa nje ndio unafanya waandike vijimaneno hapa ili kuficha ule ukweli wanaoukubali moyoni. Lakini huyu Mungu sianazijua mpaka fikra zetu? Kwahiyo ukikubali kimoyomoyo tayari ushamkataa.

NB: Mimi ni mkristo kwa kurithi, sikuchagua dini mwenyewe nimerithi ya wazazi na kwa mafundisho ya dini yangu niliambiwa Mungu yupo na sifa kedekede.

Lakini kama msomi ambae naweza kukaa na kujenga hoja na wasomi wengine, sina budi kuunga foleni kati ya wale tunaotaka majibu ya maswali yaliyoulizwa maana mpaka sasa hakuna aliejibu zaidi ya kutishiana tishiana tu.
 
Hakuna mtu asiyejua Logic na mambo ya Truth Table, hata mtoto wa O Lev aliyesoma Additional Mathematics anaijua.
Ungejua logic na truth table, usingeandika ulivyoandika.

Halafu unapoweka kiwango cha O level baada ya kusema "hakuna mtu asiyejua logic na mambo ya Truth Table", unafanya watu waliohitimu kindergarten kuwa si watu.

Mpaka hapo tu ushajionesha hujui logic wala truth table ni nini.
 
Maana ya maana ni kuruhusu kuingia yale yote yahusuyo jambo,neno husika na kuzuia yote yasiyo husu neno au jambo husika.
Wewe unaamini Mungu wa contradiction, ukisema lolote sijui nikueleweje.

Ukishakubali contradiction, umekubali usieleweke.

Ukisema juu, uweze kumaanisha chini.

Ukisema kulia, uweze kumaanisha kushoto.
 
Bro unapenda sana kupoteza muda na kutoa mifano isiyo na uhalisia. Hakuna utata wowote kuhusu suala la kilo 50 na kilo 100.

Weka vitu vya maana,na itabidi nikupe elimu ya kutoa mifano.
Unaelewa kwamba unamkubali Mungu wa contradiction?
 
Back
Top Bottom