Katoto Kadogo
Member
- Jul 3, 2015
- 7
- 21
Amesema "Kaka yangu yule mwacheni afanye harambee za Kanisani, na ili harambee za Kanisani ziwe na maana kwake lazima aje kwa watu wa CCM. Ndio maana unamsikia, wengine wanasena kwa sababu ya muda siwezi kuwataja. Lakini nataka kuuliza swali, mimi sikuwepo ila yeye alitioa shilingi ngapi?"
"Kama aliahidi, nitamtafuta Kiongozi pale Kanisani kuuliza kama mchango ulifika. Kama hakutoa mimi nitamsaidia kutoa kwa niaba yake. Sababu yule ni kaka yangu na unajua lazima uwajue Kaka zako, sio? Yule ni kaka yangu na namjua vizuri sana. Kaka yangu Mbowe kweye hela namjua vizuri sana na yeye mwenyewe anajua namjua"
"Kwenye ile 150m iliyotoka labda ilikuwa 100na... halafu nyingine ikarudishwa au inawezekana ikawa kama 200m hivi. Blaza yule namjua, inawezekana ilikuwa 200m halafu kwenye 200m akaomba, Mheshimiwa angalau na mimi nichangie isijekuonekana mimi, hivyo nitasema tu mimi na familia yangu nitoe 20m"
"Utakuta kampa 200m akaomba 20 iwasilishwe na familia na 30m iweze kubalansi pale kwani atakuwa na wangeni na vitu vingine. Halafu 150m ndio ikawasilishwa Kanisani."
Mimi naamini hakupewa 150m, kwa yule mama ninavyomjua mwenye upendo amuache Mbowe pale anawageni hata hakuna soda. Sidhani! Sio Dkt. Samia tunayemfahamu. Halafu niulize yule kaka anunue vyakula vyote vile na mahema yote yake kwa hela yake ya mfukoni? anapata nini yeye?"
Akija jukwaani anasema uongozi wa ovyo. Kama ni wa ovyo mbona unachukua hela zao? Unapata VIP tratement unasema uongozi wa uovyo? Shukrani ya Punda ni mateke.
Alivyotoka Gerezani moja kwa moja nilimuona Ikulu, aliondokaje mule ndani hatujui, alikuwa na begi hatujui, gari alilotumia ni la nani hatujui, ila mimi ninavyojua kwa yule mama Kaka yangu Mbowe aende akae naye aondoke mikono mitupu? mmmh!