Makonda apiga simu Clouds Tv 360 kukemea ushoga

Makonda apiga simu Clouds Tv 360 kukemea ushoga

Ndugu,

Jana katika television moja ya hapa kwetu ijulikanayo kama clouds tv, ilirusha kipindi chenye maudhuhi ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja (mashoga).Hoja yangu, katiba yetu na sheria hairuhusu hiloPia mila na desturi zetu haliruhusu hiloJamii yetu haijazoeshwa kuwa na vipindi vyenye mlengo wa kushoto kama hiki.

Najiuliza TCRA wako wapi? Waziri mwenye dhamana ndugu Nape atachukulia poa? Au kwa sababu ni washikaji watakausha?

NB: Hili jambo likifumbiwa macho jamii yetu itapata athari mbili;

1. Watoto wataona ni jambo la kawaida
2. Wapo watu na misimamo mikali hawatakubali hili liendelee sisi siyo kisiwa.

Watu wajue asili ya ndoa ni Mume na mke, fullstop.
Mbaya zaidi wenzetu wapo kwenye mfungo wa Ramadhan.
 
Ungeandika kwa ukamilifu kile ambacho Makonda kazungumza.

View attachment 361123
Makonda ameeleza pumba tupu hapa zilizoshiba..
Hakuna aliyekataa kwamba katika jamii kuna MASHOGA..tunajua wapo wengi tu!

Kinachostaajabisha ni hao MASHOGA kupewa muda wa kujipambanua na kujitangaza kupitia media..
Kibaya ni hao MASHOGA kupewa muda wa kuelezea faida za uchafu wanaofanya.

Kama kipindi hicho kililenga kufundisha..kingehoji madhara ya ushoga ili watu wajifunze!
 
Kama hukuona hicho kipindi kaa kimya.
Watu humu mnakuwa wajinga wakujadili vitu bila ya kufatilia
Kama ulikiona kipindi lazima utamsapot makonda kushauri viongezwe hivyo vipindi ili vielimishe athari za ushoga
Kwangu Mimi nikipindi bora kwani kimeonesha chanzo cha watoto na wajukuu zetu kuwa mashoga
Acha kutoa povu,jiulize pale shoga alipotoa faida kwamba anaingiza elfu 50 kwa siku pia amepangishiwa nyumba.Hapo alikuwa anahamasisha na siyo kukemea.Elewa kwamba every circumstance is conditioned...hilo tukio lina msukumo nyuma ya pazia tena kutoka WEST.
 
Ndugu usitake kututaka kutuaminisha hayo mnayoyafanya huko kwenye NGO zenu kuwa yana faida, kwanza kabisa tuangalie fedha mnazolipwa huko zinatoka wapi na masharti ya hao wanaotoa hizo fedha nichukulie mfano wa hili shirika au NGO inayoitwa SAUTI, shirika hili linafadhiliwa na USA na wanaofanya kazi katika shirika hili fedha zao wanazipata direct kutoka kwa wasimamizi na hazipiti kabisa katika mikono ya serikali na ni nyingi za kumwaga.
1. Kama mna nia njema na hizo NGO zenu kwa nini hawa MASHOGA wakati mnafanya registration zao hamuweki annuani au ukazi wa eneo lake sahihi? yaani huwa mnawaorodhesha kuwa wametoka maeneo tofauti na walipo.

2. Kwa nini katika ujumbe wa elimu mnaotoa kwa hao MASHOGA mmekatazwa kabisa kuwashawishi waache tabia hiyo? kuna nini kinachoendelea hapo yaani mnagawa hayo mafuta, Kondom ili watumie tu huku mkifurahia hicho wanachokifanya.
Nafikiri una miss point ya nilichokisema. Hebu soma tena context ya bandiko langu halafu urudi tena! Ubarikiwe.
 
...sijui na mkulu wa kaya naye alitazama hicho kipindi ,maana naye ni shabiki wa hiyo tv
 
Seriously? yani tumeanza kuandaa vipindi vya mashoga live runingani?
 
Clouds ni jipu. Sio TV tu hata upande wa redio. Nilichogundua kingine ni kwamba wana watangazaji ambao ni weupe kichwani kupindukia. Mara nyingi utakuta wanapotosha jamii hata kwa ishu ambazo ni rahisi tu...hata zile zinazohusu current affairs tu. Pale kuna shida kubwa!! Sijui wanaajiri kwa kuangalia vigezo gani. Wanaojua watatuambia
 
Acha kutoa povu,jiulize pale shoga alipotoa faida kwamba anaingiza elfu 50 kwa siku pia amepangishiwa nyumba.Hapo alikuwa anahamasisha na siyo kukemea.Elewa kwamba every circumstance is conditioned...hilo tukio lina msukumo nyuma ya pazia tena kutoka WEST.
Mkuu we umeliona hilo tu?
Mbona huelezi alivyoeleza alipojifunzia ushoga?
Hujapata namna nzuri ya kumkinga mwanao?
 
Ndugu usitake kututaka kutuaminisha hayo mnayoyafanya huko kwenye NGO zenu kuwa yana faida, kwanza kabisa tuangalie fedha mnazolipwa huko zinatoka wapi na masharti ya hao wanaotoa hizo fedha nichukulie mfano wa hili shirika au NGO inayoitwa SAUTI, shirika hili linafadhiliwa na USA na wanaofanya kazi katika shirika hili fedha zao wanazipata direct kutoka kwa wasimamizi na hazipiti kabisa katika mikono ya serikali na ni nyingi za kumwaga.
1. Kama mna nia njema na hizo NGO zenu kwa nini hawa MASHOGA wakati mnafanya registration zao hamuweki annuani au ukazi wa eneo lake sahihi? yaani huwa mnawaorodhesha kuwa wametoka maeneo tofauti na walipo.

2. Kwa nini katika ujumbe wa elimu mnaotoa kwa hao MASHOGA mmekatazwa kabisa kuwashawishi waache tabia hiyo? kuna nini kinachoendelea hapo yaani mnagawa hayo mafuta, Kondom ili watumie tu huku mkifurahia hicho wanachokifanya.
Nafikiri umemiss point niliyosema. Hebu rudi usome context ya nilichokiandika kwanza.

By the way, hapo MNH ambapo huyo jamaa kasema wanatibiwa ni private?! Nimekupa mfano mmoja ...

Otherwise sihitaji kukuambia mimi ni nani & nafanya kazi wapi.
 
mwenye saut ya makonda akipongeza clous tafadhari aiweke hapa ili tujue namna ya kumhukumu. maana baada ya kuitizama video ya mahojiano ningetegemea clouds kufungiwa na si kupongezwa
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam amepiga simu moja kwa moja (live) kwenye kipindi cha Clouds 360 kinachomhoji mtayarishaji wa kipindi kilichorushwa jana cha Take one Zamaradi. Kipindi hicho kilimuonyesha maisha ya shoga almaarufu KANGE.
Mahojiano yaliyokemewa na Makonda haya




Haya Jamaa Kwa Clouds kwa ujumla hawako innovative kabisa kwani kuonyesha kipindi kama hicho ni kuishiwa ubunifu kwa kweli na kuna vitu vingi sana vya kuonyesha , na vya kuifushisha jamiii. kwa mfano hata kuwa na topic ya why move from 3g to 4g unaita watallamu mbali mbli wanachambua mambo na jamii inaelimika. kingingine ni kwamba tcra wawafungie kwa muda ili waijutie adhabu mambo ya ushoga is not our culture na hasa kwa wenzetu wa imani ya kiislam sasa hivi ni mfungo wa mwezi wa ramadhani.. . vipindi vyao vingi vinapwaya sana lazima waajiri watu wenye utaalamu wa kutosha.
 
Pia jana chn 10 saa nne usiku kuna igizo ambalo shoga alikuwepo naye anaigiza ushoga.
 
TCRA hawatowafanya chochote clouds.kwasababu juzi tu hapa raisi kawapigia cm kuwapongeza.na juma mos hapa katoka kuwapa tuzo.me nilijiskia kichefuchefu vibaya mno.
Sio serikali ya JK hii hata kama aliwapigia simu sheria ni kama msumeno,yuko Anna Kilango na Kitwanga???
 
Back
Top Bottom