Makapuku Forum

Hata record za mchoraji wa nembo ya taifa tu hamna
 
THE LITTLE MAGIC ANGEL

Sehemu ya 2

Ilipoish
.
.
.Mdau ni simulizi nzuri sana na inavutia ila nakusistiza jitahidi kurekebisha makosa
Naona tatizo kubwa lipo kwenye nomino(majina,sehemu n.k)
Ni lazima yaanze kwa herufi kubwa hata kama ni mawili yote yaanze hivyo hivyo
Mfano
North Nevada
Paradise
Chief Commander
Samuel Viel
Jacob D.C n.k

Ukikazia hilo suala na baadhi ya makosa madogo km l badala ya r na z badala ya dh utafika mbali na kuvutia watu wengi

Rekebisha makosa kabla SHIMBA hajaja

............
 
Muziki sio Ajali

Habari za mapumziko ya usiku huu Makapuku wenzangu, ninajua tumekuwa na mwanzo mzuri wa wiki na wale wote ambao tumekutwa na ya kukutwa, basi kesho ni siku nyingine na jua litawaka tena. Kipindi cha pili tunaweza kusaidiwa na upepo, tusichoke.

Turudi tena kwenye muziki na hasa kuangalia udonoaji wa gitaa bila kujali ni gitaa la kawaida au la umeme ilmradi lina nyuzi 12, au 6 au 4 sisi tutalifurahia katika muziki.

Kwa mnaofunga Ramadhani, mnatenda haki na kwa wasiofunga wanatenda haki pia. Ndiyo maisha na kupanga ni kuchagua.

Gitaa. wikend ya jana Sweetiepie alileta wimbo uliopigwa na The Mountain band, wimbo wa reggae na nikasema nitareta orijino version yake iliyopigwa na kuimbwa na Peter Frampton. 'Baby I Love Your Way ndo jina la wimbo na aliucheza miaka ya kati 1970s.

Pamoja na kupigwa miaka hiyo, wimbo na mipigo haikubadilishwa sana maana Peter aliutengeneza kuishi wakati wote hata ukirudiwa.

Japo alipiga gitaa la nyuzi sita, lakiini Peter katika wimbo 'bebi i lavu yua wai' alijikita katika kugusa nyuzi nne tu za mwanzo na hakujisumbua sana na nyuzi mbili za juu ambazo huwa zina kijibass cha kishikaji

Mcheki hapa katika clip ya YouTube uone 'tenor' na sauti zinavyoendana..

 
Hata record za mchoraji wa nembo ya taifa tu hamna

Kila kitu tufanyiwe na Wazungu ndiyo maana tunaambiwa mtu wa kwanza kuliona Ziwa Victoria ni Mzungu utafikiri mababu zetu walikuwa vipofu(Mimi sijawahi kujaza hivyo kwenye mtihani hata km nimefundishwa hivyo nilikuwa radhi nikose maksi km ni ndogo) maana nilijua ni uongo mtupu tena uliopitiliza na dharau na matusi kwa mababu zetu
......
 
Lazima atiririke SHIMBA YA BUYENZE
 

Mdau shedede , kwanza niseme tu, mwanzo umeanza nao ni mzuri. Ni kitu umekaa chini ukaona na kuamini unaweza kufanya kitu na watu wakapata nafasi ya kukisoma kwa uzuri kabisa. Na ndicho nilichofanya.

Nimeipitia yote na utaona kuna sehemu nimekoleza maandishi, hapo namaanisha sarufi haijakaa sawa na kuna haja ya kuangalia sintaksia na semantikia ya kile unachoandika ili tunaosoma tusiwe na tafasiri mbili mbili (tata).

Najua kabisa unaandika hadithi ya kubuni (fiction) inayohusisha si vitu halisi bali vya kubuni na hisia zaidi. lakini changamoto yangu tu moja kwako, ukiweka vitu vya kubuni halafu ukajidai kuweka miaka basi wapo watu wanasoma sana fition na non-fiction na mmoja wapo ni mimi. Huo mwaka unaosema 1890 unaiongelea karne ya 19 na Amerika haikuwahi kuwa taifa kubwa duniani kipindi hicho, hapo tunaongelea dola la Waingereza, Wafaransa, na Warusi.

Kuwa makini sana, umewahi kusoma vitabu vya Musiba (Wily Gamba) alikuwa akiielezea dola fulani basi utadhani anachoandika si cha kubuni, ni cha kweli kumbe la.
Sikumbuki title ya kitabu lakini aliwahi kuuelezea mji na barabara za Maganzo Shinyanga na kwa kuwa nimewahi kupita maeneo hayo basi nikawa naamini ile hadithi si ya kubuni.

Nadhani umenielewa kwenye kuhakikisha unaweka ukweli kwenye hisia zako unazotaka tuzisome.

Mengine kakuelezea Bitoz na ukiyafuatilia hakyanani utatoka na kitu kizuri na kutufanya Makapuku tujisikie vizuri.

Love
Obe
 
mkuu narekebisha kabula hajaja
 
Ndiyo vizuri kumwambia mapema mapungufu yake ili awe bora baadaye
Ni bora ingekuwa kaandika mwaka 1135 kuliko hivyo

Watu wanaokubali kukosolewa na kuyafanyia kazi mapungufu yao mbeleni huwa watu bora pengine kuwazidi hata waliowakosoa
............
 
Ndiyo vizuri kumwambia mapema mapungufu yake ili awe bora baadaye
Ni bora ingekuwa kaandika mwaka 1135 kuliko hivyo

Watu wanaokubali kukosolewa na kuyafanyia kazi mapungufu yao mbele ni huwa watu bora pengine kuwazidi hata waliowakosoa
............
Na mimi editor nilipaswa kuliona hilo. Asanteni sana jamani. Upendo huu wa Makapuku yaani mpaka raha.

Notion niliyoipata katika kile kipande cha kwanza ni kwamba pengine alikiandika kwa haraka na hakuwa na muda. Na mimi kama editor nilishughulika zaidi na makosa madogo madogo tu ya kisarufi, na pia sikutaka kumkatisha tamaa. Ngoja sasa kama editor niende full throttle kwake. Naamini kazi zake zitakuwa bora zaidi na huko mbele ya safari anaweza hata kutoa kitabu. Kumbe yote yameanzia hapa Makapuku. Asante sana Obe na Madenge kwa moyo wenu huu. Mbarikiwe sana!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…