Mdau
shedede , kwanza niseme tu, mwanzo umeanza nao ni mzuri. Ni kitu umekaa chini ukaona na kuamini unaweza kufanya kitu na watu wakapata nafasi ya kukisoma kwa uzuri kabisa. Na ndicho nilichofanya.
Nimeipitia yote na utaona kuna sehemu nimekoleza maandishi, hapo namaanisha sarufi haijakaa sawa na kuna haja ya kuangalia sintaksia na semantikia ya kile unachoandika ili tunaosoma tusiwe na tafasiri mbili mbili (tata).
Najua kabisa unaandika hadithi ya kubuni (fiction) inayohusisha si vitu halisi bali vya kubuni na hisia zaidi. lakini changamoto yangu tu moja kwako, ukiweka vitu vya kubuni halafu ukajidai kuweka miaka basi wapo watu wanasoma sana fition na non-fiction na mmoja wapo ni mimi. Huo mwaka unaosema 1890 unaiongelea karne ya 19 na Amerika haikuwahi kuwa taifa kubwa duniani kipindi hicho, hapo tunaongelea dola la Waingereza, Wafaransa, na Warusi.
Kuwa makini sana, umewahi kusoma vitabu vya Musiba (Wily Gamba) alikuwa akiielezea dola fulani basi utadhani anachoandika si cha kubuni, ni cha kweli kumbe la.
Sikumbuki title ya kitabu lakini aliwahi kuuelezea mji na barabara za Maganzo Shinyanga na kwa kuwa nimewahi kupita maeneo hayo basi nikawa naamini ile hadithi si ya kubuni.
Nadhani umenielewa kwenye kuhakikisha unaweka ukweli kwenye hisia zako unazotaka tuzisome.
Mengine kakuelezea
Bitoz na ukiyafuatilia hakyanani utatoka na kitu kizuri na kutufanya Makapuku tujisikie vizuri.
Love
Obe