Ongera man united ...ongera sana..england kuingiza timu tano uefa jambo jema ...ongera sana .
Nilichokiona kwenye mchezo huo kwa ufupii tu hawa Mabarobaro wa Ajax wanahitaji misimu miwili waweze kumalizia quality yao katika baadhi ya maeneo ili waweze kufika hatua waliyofika na kumalizia walichokishindwa dhide ya united. Nje ya uwanja Ajax wanaonekana wanaweza kucheza na kumaliza fainali dhide ya united, ila ndani ya uwanja Peter Bosz kashindwa kumuingia Jose Mourinho kichwani. Ajax walikuwa bora sana nyuma ya ule ukuta wa United na mpira wao.
Mourinho ni aina ya waalimu ambao hawasumbuliwi sana na falsafa ya kiholanzi yaani Toto football

...... Amefanikiwa kupambana nayo mara kadhaa akiwa na Chelsea dhide ya fc Barcelona, lakini pia akiwa na Inter Milan na Real Madrid dhide ya fc Barcelona na sasa akiwa na United dhide ya mizizi ya falsafa hiyo Ajax.

Namna Mourinho alivyocheza dhide ya Ajax ni aina ya mbinu na falsafa zilizompa heshima...... Ni ngumu kuwachukia Ajax na falsafa yao, ila kilichowashinda ni mbinu za ku unloack mipango ya Mreno Tu..... Kumbuka Jose Mourinho ni aina ya waalimu ambao muda mwingi amekuwa akitumia mbinu zake kuanzia eneo la kiungo kurudi nyuma na kuwaacha washambuliaji wakitumia individual skills kuamua matokeo.
Ajax walishindwa kuwafikisha United mpaka katika ule muda ambao huwa wanashindwa kuelewa lakufanya dk 80, kosa la kwanza ni kuruhusu goli la mapema, approach ya dk 15 za mwanzo united walionekana kucheza kwa mipango kabla Ajax hajakaa sawa...... Lengo lilitimia baada ya kupata goli la kuongoza na kuanza mipango mipya. Aina ya goli walilokuwa wanalitaka ajax, ni aina ya magoli ambayo Jose Mourinho hajafungwa mda mrefu sana.....
Ubora wa Younes na traore uliishia nje ya box na mbele ya ukuta wa United..... Nadhani faida ya kuwa na veterani au mseto wa wachezaji wenye experience umeonekana kuwa na tija kwa Ajax. Ajax walikuwa bora zaidi wakati wanamiliki mpira miguuni mwao lakini walikosa mbinu mbadala za kupata au kuifungua beki ya United ili wafanye kile walichofundishwa darasani...... Moja ya vitu vinasumbua katika mtihani ni kukutana na swali ambalo hujafundishwa namna ya kulijibu/solve..... Ajax wamekutana na mbinu ambazo hawakufundishwa namna ya kuzifungua.
Ushindi ni kile unachokipigia hesabu kinapotimia ndio heshima ya hesabu..... Hapa Jose Mourinho kashinda yeye kama yeye lakini pia hesabu zake za plan B zimetimia. hongera special One najua ungefeli ningekuwa wa kwanza kukupa Pole.
Hongera Manchester united....... Hongera Jose Mourinho ule wimbo wa jumanne saa nne usiku najua utawahusu.......sema futuhi washakamilisha usajili mpya
Fans wote wa man u ongereniii