Makapuku Forum

Makapuku Forum

*Hekima ya leo

```Kile ambacho mwanaadam amekihifadhi moyoni mwake ipo siku atakizihirisha kwa watu```

""Basi yapasa watu wahifadhi yaliyo mema na Mazuri juu ya nduguzo; kwani huenda unaemuona mbaya na kumchukia akawa ndiyo mwema wako na mwenye mapenzi na wewe na huenda unaempenda ukamuona anakusamini na ndiye muovu wako, ufanye moyo wako uwe nadhana njema juu ya nduguzo ilikitapo dhihirika kilichopo moyoni mwako kiwe Ni chema juu yao;

_Na mwenye kutaka kukutana na mola wake akiwa Salama na mwenye kuriziwa na mola wake; Aongeze mizani yake kwakufanya yaliyo mema!

Asubuhi njema!
Hakika asante sana ubarikiwe
 
2005 - Liverpool yashinda taji la Ubingwa wa ligi ya mabingwa Ulaya.

Ni baada ya kupigwa 3-0 wakati wa kipindi cha kwanza, kabla ya kurudi kipindi cha pili na kusawazisha goli zote.

Wakaenda kushinda kwa mikwaju ya penati chini ya uongozi wa Nahodha Steven Gerrard na kocha Rafa Benitez.

Ni moja kati ya fainali za kukumbukwa.
 
1961 - Apollo program: Rais wa Marekani John F. Kennedy anahutubia Congress na kuwaambia Mpango wa Serikali kupeleka binadamu wa kwanza Mwezini kabla ya kumalizika kwa Muongo.
cec52d129d75dc5edd4f41ca57b9b4d5.jpg
a73f28dc57049e47f748c36e36132056.jpg
Kisha kikatengenezwa kituo maalumu kilichoitwa NASA's Kennedy Space Center
0c9771ae64163160dd98cd4c8d8a4fbb.jpg
ambapo mnamo July 16 1969 safari ya kwanza kwenda mwezini ikazinduliwa ambapo Neil A. Armstrong,Michael Collins na Edwin Aldrin walipaa na chombo hicho kisha wakawa binadamu wa kwanza kufika mwezini
........
 
1953 - Daniel Passarella anazaliwa.

Alikuwa ni beki kisiki wa kati wa timu ya taifa ya Argentina.

Mmoja kati ya mabeki bora kuwahi kutokea.

Alifunga magoli 134 na kuwa beki wa pili katika orodha ya mabeki waliofunga magoli mengi zaidi nyuma ya Ronald Koeman ambaye kwasasa ni kocha wa Everton.

Ni mchezaji pekee wa Argentina kutwaa Kombe la Dunia mara mbili mwaka 1978 wakiwa nyumbani na 1986 pale Mexico.
 
1963 - Umoja wa Nchi huru za Afrika ( OAU ) waanzishwa huko Addis Ababa nchini Ethiopia.
7fa79ece8877033b9f8e0e89238f2670.jpg
dd1f28313e407b9d7d041c3cfbcfe8ed.jpg
Nkrumah na Nyerere walishiriki vilivyo uanzishwaji huo pamoja na Marais wengine wa nchi kadhaa km vile Libya,Senegal,Ethiopia,Togo n.k
Nyerere alienda kama rais wa Tanganyika ....Nchi zilizopata uhuru pekee ndo zulikuwa wanachama
.......
 
- Ni siku ya Watoto wanaopotea nchini Marekani.

Siku hii ilianzishwa na Rais Ronald Reagan baada ya kupotea kwa mtoto Etan Patz.

Mtoto Etan Patz , May 25 mwaka 1979 wakati anaenda kupanda basi la shule.

Hakuwahi kuonekana tena. Hivyo ile siku aliyopotea inaazimishwa kila mwaka.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom