Makapuku Forum

Muziki Hutukutanisha Karibu


Habari za usiku huu makapuku wenzangu, saa yangu inaniambia ni saa tau dakika mbili. Napokea asante kwa wote niliowakumbusha muda.

Imani yangu wengi wetu tumekuwa na siku njema kabisa na yote tuliyofanya yameenda kama ilivyokuwa. Kwa wote yaliyoenda kombo, kesho ni siku nyingine na jua litawaka tena.

Unajisikia vipi pale unapokuwa unatembea njiani na unakutana mtu msiyefahamiana na pale mnapokaribiana kila mmoja anatabasamu, hivyo ndivyo siku yangu ilivyokuwa na nilipoenda kwa mangi kupoza koo nikakutana na mnywaji mwingine na tukajikuta tunaongea mengi sana, ya kufurahisha na sasa nimerudi 'nyumbani' kitambo, anawasalimia.

Nisikuchoshe kwa porojo, nakurudisha katika ka-kipengele ketu ka muziki tukiangalia utamu wa gitaa katika muziki.

Nina hakika kabisa umeshahisi 'taste' zangu katika muziki, yeah, napenda country music na kila aina ya muziki wenye gitaa. na leo tumwangalie mkali wa muziki wa country wa zama hizi za miaka ya 2000, acha wale 'mafaza'. namwongelea Billy Currington. Huyu ni mkali wa country na zaidi anajua kulipiga gitaa kisawasawa na hutochoka kusikiza gitaa lake likirandana na mashairi yake mazuri yenye ladha ya tufaa.

Ana tuzo kadhaa za muziki wa country na keshakuwa 'nominated ' kwa tuzo za grammy na academy.

Hapa tumwangalie katika wimbo wake 'People are Crazy'

 
1/Albert Spaggiari
Huyu kibaka ndo baba lao yaani kibaka kiwango cha SGR
Yeye yupo tofauti na wenzake maana pia ni tapeli aliyekubuhu
Alikuwa ni mpiga picha supastaa hivyo hakuna aliyemtilia mashtaka kana jamaa ni kibaka
Tukio linalokumbukwa ni lile ambao 'alichora ramani' na kuwatafuta watu wa kushirikiana nao na kufanikusha wizi uliotikisa Ufaransa na dunia kwa ujumla
Alifanikisha tukio la kuiba katika Vault ya kuhifadhia Vito huko Ufaransa na kisha kuacha maneno ukutani "Bila silaha,bila vurugu' hii ni sababu walichimba sjimo/handaki chini na kufanikiwa kuingia ndani na kisha kutoboa ukani kwenye vault na kufungua viboksi takribani 400 vyenye thamani ya pesa ya Ufaransa Milioni 60
Siku aliyokamatwa wananchi wa Ufaransa walipigwa butwaa yaani ni km Ifrisa Sultan au Kifesi ashikwe kwenye tukio kubwa la ujambazi ]
.
.
.
.
Shukrani kwa mliosapoti mada
Tukutane kesho
Mwisho
.......


 
Asante sana Obe
 
Asante kwa kumi kubwa bitoz

Kwa nini matukio mengi ni Ufaransa tu?
 
Asante Bitoz
 
Binamu asante kwa good music
 
Interesting
 
Sio kama huku bongo, mwizi akiwa anaiba polishi wanajua na mkwanja wanakula
Hao ni Highest level Criminal
Yaani wahalifu daraja la juu/kwanza
Hawaitaji sapoti ya Polisi
Wanafanya mambo kisomi/kwa weledi kiasi hadi uje kuwashtukia/kamata washakula matunda ya kazi yao vya kutosha
........
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…