Makapuku Forum

Makapuku Forum

ZABURI 33

1.Mpigieni BWANA vigelegele,enyi wenye haki,kusifu kunawapasa wanyofu wa moyo.

2.Mshukuruni BWANA kwa kinubi kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.

3.Mwimbieni BWANA wimbo mpya ,pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe.

TUOMBE

Tuna kila sababu ya kukushukuru Mungu kwa kutuamsha salama tukiwa na nguvu na kauli,tunapaswa kupiga vigelegele tukishangilia wema wa BWANA Mungu wetu ambaye umetupa siku ya leo.
Tunaomba toba kwa kwa lolote tulilokukosea.Tunaenda kinyume na roho zote zilizo kinyume nawe MUNGU wetu mwema.
Tunajikabidhi kwako Baba Tembea nasi kuanzia Jumatatu ya leo hadi wiki hii iishe,tunaomba bariki familia,kazi,watoto,wake,waume na ndugu wote.
Tunawaombea wagonjwa ,wafiwa,wenye changamoto zozote tupe amani BABA tunaomba Roho Mtakatifu atufundishe kuishi maisha ya kukupendendeza na kuwa msaada kwa wenzetu,tujazwe upendo,kujali,kuombeana,kusaidiana,kutiana moyo na pia kuwapenda wenzetu ,tukifanya hivyo tunajua Mungu utakua nasi popote tulipo.
Bariki wasafiri nchi kavu,majini,angani wafike salama.
Asante Baba maana utatupa kushinda .
Tuomba yote katika jina la Yesu Amen

SIKU NA WIKI NJEMA MBARIKIWE
Ameen
 
BlessedHope na shululu asanteni kwa sala ya kupendana na kutiana moyo asubuhi, asante kwa magazeti.

Makapuku wenzangu tuwe na wiki njema, tuwe na afya njema wiki yote na furaha huku kile tunachofanya kifanikiwe na tukumbuke kusema asante kwa kila anayeiwezesha siku iwe njema. ima ni shoeshiner, ama housegirl/boy, kondakta au mpigadebe au chizi anayekufahamu, daktari au mwalimu, polisi au hakimu, muuza maziwa au mchoma mahindi. Ilmradi tu tuseme asante na kutabasamu.

BH hujambo
Hivi binamu umemuona mama mchuchu tu ndio wa kumsalimia sisi wengine hatuna umuhimu kwako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom