shululu
JF-Expert Member
- Jan 26, 2015
- 28,137
- 109,911
Muziki ni Maisha
Habari za mapumziko Makapuku wenzangu, binafsi furahiday ilikuwa safi sana na kama kawaida kuna kijiposho nilipata ikabidi niende fukwe moja matata sana kuburudika na bakulutu, na kwa kismati nilichokuwa nacho jana Safari Lager walikuwa wanakiji hafla pale, mimi member, huitaji kununua, zinaletwa tu, mbwa anazagaa zagaa Iringa. Na kwa tachi niliyonayo nimedownload Uber so ni kuclick tu usafir unakuja.
Wakati naangusha moja moja huku nikisikiza sauti tamu za gitaa toka kwa Zahir akiimba nyimbo za kucopy, alikuwa akiimba wimbo wa 'I Heard It Through the Grapevine' wa Marvin Gaye, mara hamad namuona Komandoo Hamza Kalala kwa mbali. nami bila hiyana nikaona isiwe tabu kwanini nisiwashirikishe Makapuku wenzangu habari za gwiji hili la muziki wa dansi hapa bongo. Mondray
Muite komandoo, ndivyo alivyojulikana katika tasnia ya muziki wa dansi nchini. Hamza Kalala ni muimbaji, mpiga ngoma, mtunzi na zaidi mpigaji wa gitaa maarufu kabisa nchini.
Udonoaji wake wa gitaa uliwafanya kina Mbaraka Mwinshehe na Juma Kilaza (wazee wa Morogoro hawa, Moro Jazz na Cuban Marimba respectively) kutamani kufanya naye kazi, na alifanya kwa muda na Mbaraka kisha akafanya kazi ni Kilaza.
Komandoo alipata umaarufu mkubwa akiwa na band ya Vijana jazz ikimilikiwa na chama, keshafanya kazi na kina Hassan Dalali, Kitime, Pembe, na wengine wengi, kisha akaenda washirika Jazz band 'watunjatanjata'. Baadaye akaamua kujitegemea na kuanzisha band yake iliyoitwa Bantu Group.
Umewahi kuusikia wimbo wa Baba Jeni? Ni kati ya nyimbo chanche sana za dansi zilizokuwa na toleo la kwanza, la pili na la tatu.
Sikiza gitaa lake akilivuta kiumakini kabisa huku kinanda kikipapaswa na Abdul salvador akak 'Faza Kidevu'
![]()
Kesho ni siku maarufu ya kumsheherekea Mama na Ushawishi wa Wamama wote kwetu. (sio siku maarufu sana kwetu lakini ni kati ya sherehe ambazo huwa najitahidi kuhakikisha angalau ninafanya kitu kizuri kwa ajili ya mama na wamama wote)
Baba jeni ehiiiii, ehiiiii nimweleze nani
Asante Obe
Ya kale ni dhahabu
