Siwalaumu Marastafari wenzake kumpachika cheo cha unabii katika dini yao. Alikuwa na falsafa nzito sana kuhusu maisha, nafasi ya binadamu hapa duniani, migongano ya kitabaka, ubaguzi na mengineyo mengi. Ukizisikiliza nyimbo zake kwa uangalifu utagundua kwamba alikuwa na ujumbe mzito sana na aliweza kuuwasilisha kwa ustadi wa ajabu.
Basi siku moja niko mitaa fulani huko kwa Trump na Corolla yangu iliyochoka nikiwa bado mgeni mgeni mwanafunzi. Nimechochea "I shot the sherrif but I swear it was in self defense" kwenye red light na madirisha yako wazi. Kuja kuangalia pembeni kumbe kuna polisi naye kafungua madirisha. Jasho lilinitoka kwa sababu hata leseni nilikuwa sina. Kwa bahati nzuri taa zikaruhusu kila mtu akaenda kivyake. Sitakaa nisahau!