Makapuku Forum

Makapuku Forum

5fa0a926ee5702b4c6721d595a20c844.jpg
Naipenda
 
Pole sana mkuu Mussolin5 naungana nawe katika kumuombea binamu mpendwa

NAMUOMBA MUNGU ATUPE UVUMILIVU WA KIMAPENDO,BWANA ALITOA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIBARIKIWE NA DAIMA TUWE NA MATUMAINI,SINA NENO ZURI LA KUSEMA BALI NAOMBA TUUNGANE HAPA :

1 WATHESALONIKE 4

13.Lakini ,ndugu zangu,hatutaki msijue habari zao waliolala mauti,msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

14.Maana ,ikiwa twaamini ya kwamba,Yesu alikufa akafufuka vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu Mungu atawaleta pamoja naye.

15. Kwakuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana ,kwamba sisi tulio hai tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana,hakika hatutawatangulia wao walioisha kulala mauti.

16. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko ,na sauti ya malaika mkuu na parapanda ya Mungu,nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17.Kisha sisi tulio hai tuliosalia ,tutanyakuliwa pamoja nao mawinguni,ili tumlaki Bwana hewani na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

18.Basi farijianeni kwa maneno haya.

Naomba tuamini kuwa Binamu mpendwa wetu amelala na tutaonana siku ya mwisho,nafsi yake ipokelewe na Mungu wetu

"Wale tunaowapenda hawaendi milele,wanatembea pembeni yetu daima,hatuwasikii,hatuwaoni
Lakini wapo daima nasi,tunawapenda,tunawahitaji,tunawakumbuka wanadumu mioyoni mwetu....upendo wetu kwao ni ishara ya uwepo wao maana waituachia upendo"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom