Makapuku Forum

Uko sahihi kabisa, fanya siku moja utumegee japo kwa uchache mambo ya DNA
 
Mkuu hebu tumegee kidogo kuhusu Gregory Mendel
 
Nimegundua kitu katika muziki wa zamani ni kwamba hauchuji ladha pia hauchuji katika kuusikiliza, ndio maana mtaasisi Obe anapenda vitu old.

Mama mchungaji nimekuletea wimbo ulioimbwa miaka 10 iliyopita waimbaji wake wakiwa ni Jacquiline Ntuyabaliwe (Mrs Mengi) akimshirikisha Bushoke Nalia kwa furaha

Cc BlessedHope
Cc Obe
 
Madenge umezidisha sasa. Teknolojia hii ina faida nyingi lakini, kama ilivyo kawaida ya teknolojia nyingi nyingine, inawezekana ikawa na madhara makubwa zaidi. Japo imeweza kutupatia mazao yanayokomaa kwa muda mfupi, yanayostahimili ukame, yasiyoshambuliwa na magonjwa hovyo hovyo, yenye virutubisho vingi zaidi na yasiyohitaji uangalizi wa karibu (mfano kupaliliwa mara kwa mara), madhara yake bado hayajaeleweka sawa sawa; na inatakiwa isimamiwe ili isitumiwe vibaya.
 
Huku kwetu kuna mtu anandimu hazina mbegu ni kubwa mnooo na zina maji mengiii ukitaka kupanda uwe na mti mbegu hakuna,na mti wake unazaaa sana
Napendelea vitu vya kienyeji
Huwezi kunilisha natikiti yenye rangi km kombati za jeshi
Pia napenda mafuta ya mawese cha ajabu nikienda kijijini wananipikia mafuta ya kisasa
.......
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…