Makapuku Forum

Makapuku Forum

62a5211234a035f9ad97779f78d9bcf8.jpg
326a4cca868a2d28b46c452dd6eb40c4.jpg
3273430d3e0cd6b3e705069a639af886.jpg
R.I.P Adolf Hitler na mkewe
 
Kuna utata kuhusu kifo cha huyu jamaa. Inasemekana hakuna aliyeona maiti yake (iliyoonyeshwa eti haikuwa yake) na watu wa conspiracies wanasema kuwa pengine alisepa kwenda Argentina kama maofisa wake wengi walivyofanya. Wanasema eti wanajua hata sehemu aliyoishi huko Argentina mpaka alipofariki na sasa wapo kwenye harakati za kutafuta kaburi lake.

Yote kwa yote huyu jamaa ana mengi sana ya kutufundisha kama binadamu na kwa sisi wafuasi wa falsafa za mkondo wa Existentialism huwa tunamuona kama taa ya kutuonyesha unyama na ukatili wa binadamu pamoja na tamaa (ya binadamu) isiyoisha ya kutaka siyo tu kuangamiza wengine bali hata yeye mwenyewe ikibidi. Na binadamu huyu ana tabia ya kufanya fatal mistakes, mistakes ambazo zina gharama kubwa mno katika maisha na hata kuwepo kwake. Kwa Hitler fatal mistake ilikuwa ni kupeleka mamilioni ya wanajeshi wake kwenda kuivamia Urusi - bila kujali hali ya hewa, umbali na bila kujua hasa nguvu za adui. Yote haya ni kinyume cha medani za kivita na kilichowapata Wajerumani huko Russia leo hii ni case study ya how not to conduct a war na ilikuwa ndiyo mwanzo wa kushindwa kwa Ujerumani katika WW II.

Hata wewe kuna kosa gani (na pengine la kijinga tu) ulilowahi kufanya ambalo lilikugharimu sana - kiroho, kimwili, kisaikolojia, kijamii na hata financially? Ulijifunza nini kutokana na kosa hilo?

SHIMBA...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom