Makapuku Forum

Makapuku Forum

15
a14a3d96c0b5f77acaa936c000f70052.jpg
 
Kuna utata kuhusu kifo cha huyu jamaa. Inasemekana hakuna aliyeona maiti yake (iliyoonyeshwa eti haikuwa yake) na watu wa conspiracies wanasema kuwa pengine alisepa kwenda Argentina kama maofisa wake wengi walivyofanya. Wanasema eti wanajua hata sehemu aliyoishi huko Argentina mpaka alipofariki na sasa wapo kwenye harakati za kutafuta kaburi lake.

Yote kwa yote huyu jamaa ana mengi sana ya kutufundisha kama binadamu na kwa sisi wafuasi wa falsafa za mkondo wa Existentialism huwa tunamuona kama taa ya kutuonyesha unyama na ukatili wa binadamu pamoja na tamaa (ya binadamu) isiyoisha ya kutaka siyo tu kuangamiza wengine bali hata yeye mwenyewe ikibidi. Na binadamu huyu ana tabia ya kufanya fatal mistakes, mistakes ambazo zina gharama kubwa mno katika maisha na hata kuwepo kwake. Kwa Hitler fatal mistake ilikuwa ni kupeleka mamilioni ya wanajeshi wake kwenda kuivamia Urusi - bila kujali hali ya hewa, umbali na bila kujua hasa nguvu za adui. Yote haya ni kinyume cha medani za kivita na kilichowapata Wajerumani huko Russia leo hii ni case study ya how not to conduct a war na ilikuwa ndiyo mwanzo wa kushindwa kwa Ujerumani katika WW II.

Hata wewe kuna kosa gani (na pengine la kijinga tu) ulilowahi kufanya ambalo lilikugharimu sana - kiroho, kimwili, kisaikolojia, kijamii na hata financially? Ulijifunza nini kutokana na kosa hilo?

SHIMBA...
Aisee
 
BWANA YESU APEWE SIFA

JIONI HII MUNGU ANASEMA NAWE/NAMI YAKUWA

USIOGOPE/NISIOGOPE

1.....maana nimekukomboa;nimekuita kwa jina lako,na wewe u wangu.

2 upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe;na katika moto,hautateketea;wala mwali wa moto hautakuunguza

3.maana mimi ni BWANA MUNGU WAKO,Mtakatifu wa Israel,MWOKOZI wako.....


ISAYA 43:1-3

HALELUIYA

Hakika hatupaswi kuogopa jambo lolote wala kitu chochote MAANA MUNGU YU PAMOJA NASI KUTULINDA

Jambo muhimu ni kumtii

Wakati mgumu,kukosa kazi,kuachwa,kudharauliwa,kukosa kuoa au kuolewa,kukosa watoto ,kuugua,mazingira magumu ,kuuguza isiwe sababu ya kuacha kumwabudu Mungu.

Mungu anatupenda na kamwe hatatuacha.TUSIOGOPE

TUOMBE

MTAKATIFU MTAKATIFU MTAKATIFU BWANA MUNGU WA MAJESHI ASANTE KWA YOTE UNAYOTUTENDEA TUNAKUSHUKURU KWA UPENDO NA WEMA WAKO KWETU,ASANTE KWA ULINZI WAKO NA AHADI ZAKO ZA MILELE TUNAOMBA UTUIMARISHE KIROHO HATA TUNAPOPITIA CHANGAMOTO YOYOTE TUKUONE WEWE,ASANTE BABA KWAKUA UMETUAHIDI ULINZI DAIMA
TUNAOMBA NA KUSHUKURU

AMEN

MBARIKIWE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom