Makapuku Forum

Makapuku Forum

aeabe1e57fed2c21743716ae4dcfef23.jpg
3ab424475e37709043c24722b981cd5b.jpg
04cf79fd9924c8f053b43286752348cd.jpg
hii kitu ndio nimejua leo kumbe ni jina la mtu
 
Bay of Pig Invansion

17-19 April 1961.

SEHEMU YA KWANZA.

Kwanza kabisa taifa la Cuba na Marekani walianza uhasama wa kisiasa wakati wa vita ya Spanish-ameican war mwaka 1898.

Cuba ilikuwa ni miliki/koloni la wahispania kwa miaka mingi ktk karne ya 19.

Baada ya hapo Cuba ilikuwa miliki ya marekani hadi Cuba ilipopata huru 20/05/1902 kutoka kwa wamerekani na wakamuweka mcuba-mzaliwa marekani Bw. Tomas Palma kuongoza Cuba kwa mara ya kwanza.

Baada ya hapo Cuba ikaja kupata vijana kama Castro wakaondoa mapandikizi ya wamarekani serikali.

Back to the Topic sasa..



Mwaka 1959 marekani chini ya Dwight D. Eisenhower ilikuwa kwenye Vita baridi ambayo kipindi hiki mirengo ya kisiasa ya kibepari na kikomunist ilionyesha tofauti zao sana..

Sasa Cuba chini ya Castro ilifanikiwa kutaifisha mashamba ya kahawa, mashamba ya miwa na viwanda vya wamarekani nchini cuba ila kubwa zaidi ni kuwa Cuba iliweza kujenga ushirika mkubwa na nchi za umoja wa kisovieti ambazo ndio zilikuwa vitani na marekani

kwa hiyo marekani alitaka ampindue Castro manake anakuwa threat sasa..

CIA chini ya mkurugenzi wa wakati huo Bw. Allen Dulles wakaja na mpango wa kumpindua Fidel castro na serikali yake...

Inaendelea sehemu ya 2..
Nondo zimetulia
.....
 
Haswaa mkuu. Halafu huwa hana ubavu wa kwenda vitani pekee yake bila msaada wa Nato.

Rejea Vita ya Vietnam, Vita ya Ghuba.
Sehemu ya 2 ya Bay of pigs Invasion.

Baada ya CIA Chini ya Allen Dulles na ushirikiano wa Kaka yake John Dulles aliyekuwa Secretary of State kwa kipindi hicho wakaja na mpango wa kutengeneza kikosi ambacho kitakuwa kinaongozwa na Wanajeshi wacuba waliokimbia Cuba wakati mapinduzi ya fidel Castro

Lengo la CIA kuwatumia hao rai wa cuba walioko uahamishoni ni :

1. Walikuwa wanalijua jeshi la Cuba vizuri na wengi walikuwa ni infatry Soldiers walikuwa trained kwenye millitary Academy za Cuba.

2.Ni watu ambao tayari walikuwa na kisasi cha kisiasa ya Serikali ya Fidel Castro.

3. Ni rahisi kwa wao kujenga imani na picha wa raia wengine wa Cuba kuwa kumpindua Fidel ni sahihi kwa sababu kuleta demokrasia

4. Waliahidiwa kuongoza serikali ya Cuba kama mapinduzi yakifanikiwa

Baada ya hapo CIA ikawapata hawa wanajeshi wa Cuba ambao wengi walikuwa ni wakufunzi katka academy za jeshi nchini marekani.

1.José Alfredo Pérez San Román
2. Erneido Andres Oliva Gonzalez

Baada ya kuwapa hawa jamaa, wakaaza kutafuta wacuba hasa wanajeshi walikuwa uhamishoni na kuwapeleka nchini Guatemala na Nicaragua kwa ajili ya mafunzo..

CIA wanakaunda kikosi hicho na kukiita Brigade 2506,

Tarehe 4 April 1961 , Rais John F kennedy anatoa approval ya kufanyika kwa misheni ya kumpindua Fidel Castro wakitumia Brigade 2506 .

Tareh 13 April 1961, wajaeshi 1400 wanaounda kikosi cha Brigade 2506, wakiwa wamegawanywa kwenye vikosi 5 wanaondoka kwa boti kwenda Cuba kupitia fukwe za Bay of pigs..

Tar. 15 April 1961 , ndege 8 aina ya B-12 zinashambulia maeneo ya kijeshi ya Cuba na kurudi ktk Ardhi ya marekani..Hii ilifanywa na wamarekani wenyewe kikosi cha Anga.

Usiku wa tar. 16 April kuamkia 17 april 1961, Uvamizi rasmi unafanyika na vita inapigwana kwa siku 3 mfululizo..

Majeshi ya Cuba chini ya José Ramón Fernández wakiwa na wanajeshi 25000 yanapambana na kikosi cha watu 1400 na kuwapiga . John Kennedy akatuma ndege zingine na kusaidia kazi ya kumtoa Castro..

Fidel Castro akadouble wanajeshi kwenye uwanja wa vita.Watu wakala kichapo kitakatifu..

April 20 , kikosi cha Brigade 2506 kikajisalimisha kwa vikosi vya Fidel Castro..

US walitumia zaidi ya 13.1 million UsD

Ilikuwa na aibu kwa CIA ya vyombo vya usalama vya marekani

Mwaka huo huo Allen Dulles anaachia ngazi baada ya kuongoza CIA kwa muda mrefu zaidi.


Muwe na mchana mwema wakuu..
 
Hahahaha eti mambo ya nyuma ya pazia!!!!!! Watanzania bana hamuish vituko

We kula ugali wako na dagaa ulale

Usiendekeze ubishi fuatilia mtiririko wa mada
Silaha kubwa ya USA ni propaganda kupitia CIA...Nyie mnaoamini anashindaga vita kwa hayo masilaha yake makubwamakubwa mnajidanganya hamjui mambo ya nyuma ya pazia
Naishia hapa
.......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom