Msimu wa lawama huu
UCL RESULTS
Borrusia Dortmund 2-3 Monaco
Bayern Munich 1-2 Real Madrid
Atletico Madrid 1-0 Leicester City
Msimu wa lawama huu
UCL RESULTS
Borrusia Dortmund 2-3 Monaco
Bayern Munich 1-2 Real Madrid
Atletico Madrid 1-0 Leicester City
Mkuuu jana nilitingwa ata hatukupitiaa michezo wa kina...anyway tujikumbushee ...

Tuanze na wahun wa Simeon Diego vs The Fox..mtaji wa goli moja nyumbani ni mtaji mdogo sana kwa Atletico Madrid na pia kuwabakisha mchezoni Leicester city..... Namna Leicester wanavyocheza sina shaka ni miongoni mwa timu ngumu iliyokutana na timu nzuri ya Atletico. Aina yao ya mchezo wa ugenini ni dhahiri shahiri wanamatarajio makubwa katika mchezo wa nyumbani King Power stadium.
Bado maamuzi ya waamuzi yamendelea kuwa tatizo katika michezo mingi ulimwenguni...... Aina ya penalt aliyotoa Mwamuzi wa mchezo huu yanakinzana sana na macho yetu sambamba na screen zetu.....
Mpira ni mchezo wa makosa na katika Zama hizi ukikosea kidogo refa anakosea sana...... Greizman anachezewa faulu nje ya box pembeni kidogo ya mstari wa box lakini kwakua mpira ni mchezo wa makosa basi refa anafunika mkono na kinaliwa tuta lilifanya wawakilishi pekee wa lawama ligi kuu ya Uingereza kulala kwa goli moja Bila.
Sasa shughuli inahamia pale king power stadium na hii inaweza kuwa sehemu ngumu sana kuamua mchezo huu...... Best team loss.... Leicester walikuwa wazuri sana katika pressing ila pia Atletico walikuwa bora kumaliza mchezo japo kwa mbindee.....

Huku sasa Sehemu ya kiungo cha Real Madrid ndio sehemu yenye matatizo..... Inafeli kuwaunganisha timu, inafeli kuwaunganisha washambuliaji sambamba na kuwatengenezea nafasi za magoli, hilo limedhihirika baada ya Martinez kutoka kwa adhabu ya kadi nyekundu ila Bado display ilikuwa chini sana kwa viungo mpaka pale Ramos aliposogea juu kwenye kiungo ili Toni Kroos asogee mbele zaidi.....
Makosa ndio sehemu ya mchezo.... Anafanya makosa Javie Martinez na yanaghatimu timu, kadi ya pili haina shaka ila namna alivyoipata kadi ya kwanza haikuwa na ulazima wa kupanda na mpira kama wewe unaujua ni beki wa kati....... Martinez anapanda na mpira juu alafu anapoteza, Madrid wanaunasa wanapigiana one two anamchezea faulu Christian Ronaldo na anaanza kutengeneza usalama mdogo kwa Wajerumani.....
UEFA champions league pekee ndio inatumia marefa watano ila refa wa tano kashindwa kujua kama ile ni penalt au lah. .. dany carvajol hakuwa ameshika mpira na kwa bahati mbaya mpira wa adhabu ndogo penalt iliyopigwa na muhuni wa chile Atur Vidal inapaa juu kabisa ya lango..... Hapa ndipo tunaendelea kuamini Waamuzi hufanana kasoro rangi tu.
Goli la kwanza linatokana na krosi iliyopigwa kutoka upande wa kulia na goli la pili linatokana na mpira uliopigwa kutoka upande wa kushoto na kikichotokea ni sàfu ya ushambuliaji kuonesha kuwa ikipatiwa mipira sahihi inaweza kufanya kitu sahihi........ Baada ya Xavi Alonso kutoka Madrid walikuwa huru sana ila viungo wake hawakuwa na njaa ya matokeo na hivyo kupelekea kuonekana kama wanarelux zaidi kuliko ku re-act.....
Manuel Neuer alifanya kazi ya ziada sana katika kuwabakisha Wajerumani katika mchezo......
Fc Bayern Munich 1-2 Real Madrid.