Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mkuu ilikuwa ni zuga tu watu wasishtuke, ulimi wangu ni mtu balaa, hawa viumbe wakija kwenye maombi..ninapowapa ushauri huwa wanasema wanajuta kuchelewa kuonana nami labda ningefunga nao ndoa, hivi huoni wale waliopotelewa na wenzi wanahisi wako kwangu!
Makubwa..!!kumbe ndio maana wadada wakija kwenye maombi unanituma tuma sana ili upate time ya kuchombezana nao??? Sikuweziiii mtumishi.
 
Nilimuasa baba mtumishi asiwafanyie maombi wadada,kwa sababu wadada ndio maradhi yake makubwa,akadai kuwa Jimena anataka kuungama tu basi,cha kushangaza wamejifungia eti anamuombea toba,matokeo yake ndio haya shemeji. Wacha nipeleke hili kwa baba paroko maana mtumishi sasa anahubiri meno badala ya neno.
Ooooh sweetydarling umekuja, miss you sana,
Jimena tumetoka naye mbali sana ni ngumu kututenganisha japo urafiki wetu ni wa kawaida tu
 
Taharuki jambilo atishia ndoa za watu, wamo wake wa vigogo wa KAPUKUZ FORUM [KF], atumia Neno la Mungu kama ndoano!!

Yule Mch. aliyejizolea sifa na heshima tele hapa KF imefahamika rasmi kuwa ndiye kidudu mtu anayevuruga mahusiano ya watu kwa kigezo cha sala.

Mmoja wa wanafamilia wa KP (jina kapuni) amedhibitisha kuwa toka mwishoni mwa wiki ndoa yake iliyokuwa changa inaelekea kuvunjika sababu ikiwa ni Mch. jambilo, "ni Kweli nipo kwenye wakati mgumu toka huyu Mch. aniombee naona kuna dalili zakuachwa, wife anaondoka bila kuaga, nikim txt wala hajibu kitu kwa kweli sielewi kabisa"

Naye mmoja wa member mkongwe wa KF ametoa ya moyoni kwa kusema "jambilo anatupia watu roho ya kukataliwa, toka ameingia hali si shwari tena, kinachouma zaidi anatumia neno la Mungu kumhadaa mpenzi wangu, alimaliza kwa kusema ila ipo siku yake.

Baada ya shutuma hizo, tuliamua kumtafuta kama ni kweli au laa na alisema kwa sasa nipo kwenye maombi nitafute mda mwingine
 
Nilimuasa baba mtumishi asiwafanyie maombi wadada,kwa sababu wadada ndio maradhi yake makubwa,akadai kuwa Jimena anataka kuungama tu basi,cha kushangaza wamejifungia eti anamuombea toba,matokeo yake ndio haya shemeji. Wacha nipeleke hili kwa baba paroko maana mtumishi sasa anahubiri meno badala ya neno.
Shemeji wacha turudi magotin mwa bwana naamini Mtumishi hajapotea kwa kiasi kikubwa saaaana jambilo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom