Bitoz
JF-Expert Member
- Aug 27, 2015
- 30,823
- 126,632
Ahsante kwa somoHaya wapendwa...
Kuna mashamba wanakodisha ni sh. Elfu hamsini (50000) tu kwa eka moja huko vijiji vya mkulanga (pwan) si mbali sana na Dar
Ulimaji wa tikiti maji hauhitaji mvua bali ni kilimo cha kumwagilia
Kilimo hiki kinachukua siku60 toka Siku ya kwanza kupanda mbegu hadi kuvuna
Mwakajana nililima eka mbili
Na mtaji wake ni ml. 1.8 hadi ml. 2 kwa heka zote mbili
Hiyo gharama ni ya vitu vyote yani nimejumuisha had mafuta ya gar siku nilizokuwa naenda shamba .....
Mbegu yake inauzwa laki mbili kwa nusu kilo inaitwa Sukar F1 na nuau kilo inatosha eka moja hivyo ekari 2 ni kilo moja
Kilimo hiki kinahitaji monitoring ya hali ya juu ili usipate hasara..
Kule shamba (mkulanga)kuna vibarua ila wanahitaj usimamiz kwan mnajua watu wa pwani si wachapakazi sana....
Msimu mzur wa kilimo hiki ni kuanzia mwez wa tano had wa Tisa ....inabid mwez wa Tisa uwah kulima ili usikutane na matunda sokon Yale ya November mwshoni
Eka moja ikihudumiwa vizur inatoa tani 6 yaani gar mbili za tani tatu na msimu mzuri ni milion1.8 to ml 2 hivyo ukilima eka mbili una tani 12 means gar 4 za tani tatu...hapo huwez pata chin ya ml.6 ukirudisha gharama uliyotumia unabak na akiba unajiongeza tena...
Kama hujaelewa ruksa kuuliza
Masoko yapo kwan kipind cha kiangaz tikiti ni dili sana
Narudia tena usimamiz wa karibu unatakiwa. shambani...
...................