Makapuku Forum

Makapuku Forum

2015 - Deo Filikunjombe anafariki Dunia katika ajali ya Helikopta.

Alikuwa ni mbunge wa Jimbo la Ludewa. Alifariki siku kadhaa kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 nchini Tanzania.

Anatajwa kama Mbunge machachari katika Bunge lililopita na anakumbukwa sana kwa kuwa sehemu ya kamati ya Bunge iliyoundwa kuchunguza skandali ya Escrow kando ya Zitto Kabwe.
R.I.P. Deo.....Mungu atakulipia
 
UJUMBE WA LEO...

Mwanamke na mwanaume walikuwa wakiendesha magari tofauti, yakagongana. Magari yote yakaharibika vibaya kwani ajali ilikuwa mbaya na ilisababishwa na uzembe wa mwanamke.

Pamoja na magari yao kuharibika vibaya cha kushangaza kati yao hakuna aliyeumia. Walipojivuta kutoka kwenye magari, mwanamke akasema, "Wewe ni mwanaume!...inafurahisha sana, na mimi ni mwanamke. Angalia magari yetu, hakuna kilichobakia lakini bahati nzuri hakuna aliyeumia. Lazima hii ni ishara kutoka kwa Mungu kwamba tuwe marafiki na tuishi pamoja kwa siku zote za maisha yetu zilizobakia".

Mwanaume akajibu, "Nakubaliana na wewe kabisa. Lazima hii ni ishara kutoka kwa Mungu".

Mwanamke akaendelea "...na angalia huu muujiza mwingine, gari yangu imeharibiwa vibaya, lakini chupa hii ya mvinyo (wine) haikuvunjika. Kwa kweli, mungu anataka tunywe mvinyo huu na kusheherekea tulivyo na bahati nzuri.

Mwanamke akampa Mwanaume ile chupa. Mwanaume akainamisha kichwa kutoa ishara ya kukubali. Mwanaume akaifungua na kunywa nusu ya mvinyo na kumrudishia mwanamke.

Mwanamke akachukua chupa, akafunga kizibo haraka na kumrudishia tena mwanaume.

Mwanaume akauliza "Haunywi hata kidogo?"
Mwanamke akajibu "Hapana, nadhani nitasubiri POLISI waje kuchukua ushahidi wao (KOSA LA DEREVA KUENDESHA GARI HUKU AMELEWA)."

UMEJIFUNZA NINI?
1. Adam amekula tunda tena!
2. Wanaume hawajifunzi kamwe!
3. Wanawake hawabadiliki!

Jumamosi Njema.
Aiseee...
 
Back
Top Bottom