Sio kila mtu anaishi kutafuta utajiri. Wapo watu wengi sana wanafurahia kuwa na elimu nzuri na kutumikia jamii. Ndiyo maana tuna madaktari, marubani, waandishi wa vitabu na kadhalika. Hakuna hata nchi moja iliyoendelea kwa kuwa tu na matajiri. Nchi zinaendelea kwa kuwa na wasomi wazuri, hivyo kuwa na wahandisi, wanasayansi, madaktari na kadhalika. Mwisho mtu akikwambia Sio vizuri kuwekeza kwa ujumla katika elimu ya darasani, mwambie akatibiwe kwa madaktari uchwara ambao hawakujielimisha vizuri au apande ndege yenye rubani ambaye alikuwa anakacha masomo. Usichezee elimu, na tusidanganyike na hawa motivational speakers
............................................
Mi nahisi inazungumziwa maendeleo ya nchi sio mtu
.............................................