Makapuku Forum

Makapuku Forum

Twin...watoto hawatabiriki...ujue kuna tabia anaweza akaidevelop ukimchekea chekea anaweza kukuwa nayo...ni heri akakanywa na fimbo kidogo juu ndio huwa anaelewa somo. Mfano mimi nakumbuka jambo lolote baya nililofanya utotoni sikuwahi kurirudia baada ya kucharazwa maana nikiwaza yale maumivu tu naishiwa pozi...true story mi nilikuwa nna michezo ya hatari sana ambayo mingine pengine ingeweza kunidhuru hadi mimi mwenyewe...imagine mama angekuwa kimya tu.pengine ningekuwa nimeshapoteza uhai au kuharibikiwa kabisa pia nimeshuhudia watoto waliolelewa kimayai mayai sana walivyokuwa baadae. fimbo inamuhusu mtoto.
Mi sijasema ntamchekea chekea hebu usinilishe maneno
Ila nimeishi kwenye Jamii ambayo haipigi watoto na watoto wana nidhamu ya hali ya juu tatizo nyie mmekariri.
Nimeishi pia kwenye Jamii inayotandika watoto na kuna watoto sugu.
Kwenye malezi kuna mambo mengi sana, na malezi yanaanza dakika ile mtoto anapozaliwa, ukimzoesha vibaya pale basi jua hata akikua atakusumbua sana
Ni hayo tu kwa leo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom