Makapuku Forum

Makapuku Forum

2009 - Senator Ted Kennedy anafariki Dunia.

Alikuwa ni Senator wa Massachusetts.

Alikuwa ni mdogo wa Mwisho wa aliyekuwa Rais wa Marekani, John F. Kennedy.

Ni miongoni mwa wanafamilia wachache wa Familia ya Kennedy kufa kifo cha kawaida.

Nitawaletea Laana/ Mkosi wa Familia ya Kennedy " The Kennedy Curse ".

Wengi wakiamini vifo vya ajabu vilivyoikumba baadhi ya wanafamilia wa Familia hiyo ni Mkosi au Laana.
Jamaa alikuwa sanator wa maisha we miaka 40+ useneta gan huo
 
1472143683371.jpg
 
NUKUU NO 1#

Sanaa ya Uongozi au sifa kuu ya kiongozi mzuri ni uwezo wa kusema "hapana" na si ndiyo'.
Ni rahisi kusema "ndiyo" kuliko kusema hapana.
Wakati mwingine ni vyema kukubali kushindwa ukawa umetenda sahihi kuliko kukazania kushinda ukawa umetenda hovyo.

Haya maneno yalisemwa na waziri mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.

Alizaliwa Mei 6,huko Edinburgh, Scotland. Alikuwa kiongozi wa Chama cha Labour kuanzia mwaka 1997 hadi Juni 2007.

Ndiye mwingereza wa kwanza kushika Uongozi wa Chama cha Labour akiwa na umri Mdogo
Moja ya viongozo walio kuwa viongozi haooo
 
NUKUU NO 2#

Kansa ya Uongozi ndani ya CCM isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza nchi yetu badala ya CCM.

Ubovu wa Uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa vyama vingi.
Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza nchi yetu badala ya CCM au ambacho kingekilazimisha CCM kusafisha Uongozi wake kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao.
Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani, wala dalili zozote za kuondoa kansa ya Uongozi ndani ya CCM.

Ni maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, kama yalivyo katika kitabu chake kinachoitwa Uongozi wetu na hatima ya Tanzania alichokiandika mwaka 1994.

Mwalimu alifariki Oct 14,1999
Mwalimu alikiwa ni moja ya viongozi wachche duniani wanao soma sanaa
 
NUKUU NO 3#

Kama haiwezekani ukaogopwa na kupendwa kwa wakati mmoja, basi ni heri uogopwe kuliko kupendwa.
Kwa hakika, ni jambo jema kwa binadamu kuogopwa kuliko kupendwa.

Haya yalitamkwa na mwanafalsafa wa kale wa Italy. Niccolo Machiavelli.

Alizaliwa huko Florence mnamo Mei 3,1469 na kufariki Dunia katika mji huo huo.
Machiavelli, ambaye alikuwa pia mwanadiplomasia, aliandika kitabu chake cha kwanza mwaka 1499 kinachoitwa Discourse on Pisa.
Hata hivyo kitabu chake maarufu na kinachosomwa na watu wengi mpaka sasa kinaitwa The prince na alikiandika mwaka 1513
The Prince

Hahaha, huyu jama namkubali sana
Yeye na THOMAS HOBBES
 
NUKUU NO 4#


Kuna watu wanafikiri pengine hii kazi (urais) ni rahisi lakini kama unawapenda watu wako na unaumizwa na hali zao na unapenda uwavushe, hii si kazi rahisi.

Umekuja huku nje ya nchi na umeona mchakamchaka wa mikutano.
Usiku wa kuamkia leo nimepata usingizi saa11alfajiri na bado nina mambo mengine ya kufanya usiku huu.

Maneno haya yalisemwa na aliyekuwa Rais wa Tanzania awamu ya nne Jakaya Kikwete, wakati wa mahojiano na waandishi wa habari.
Aaaah
Alikuwa ana shinda kwenye ndege tuu naye mweer!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom