Siku moja rafiki yangu alinifuata akiomba ushauri, alikuwa na matatizo makubwa sana , na kimsingi alikuwa amekata tamaa ya maisha na kujiona ana mikosi na Mungu amemwacha.Ki ukweli nilishindwa hata la kumwambia.Nikamwomba tukutane siku inayofuata....kwamba kuna ufumbuzi ninao mzuri tu ( kiukweli sikuwa na chochote kichwani)
Jioni nilitafakari sana nifanyeje, na nikapata wazo.
Nikamwambia naomba kesho tuonanane unisindikize mahali....na nikamwambia kama unahela kidogo nunua miche ya sabuni..ntakwambia cha kufanya.
Tukaingia garini...baada ya kama dk 30..akaniuliza kaka..kwani tunaenda wapi lakini? nikwamwambia usiwe na shaka ndugu..
Ghafla akaona tunaingia getini ..na Bango limeandikwa Ocean road hospitali..
Nikapita naye kuona wagonjwa na kuwapa zawadi za sabuni.
Lakini wakati tunapita kuona wagonjwa ....ghafla nikaona ananivuta mkono kwa chini chini...ni kama alikuwa ananizuia tusiendelee mbele.....sikumwelewa...
Akaninong`oneza angaliaa palee...huku akionyesha kwa macho kitanda kinachofuata...
..macho yangu yalipogonga pale kitandani ...ni nili freeze kwa sekunde kadhaa..... tulibaki midomo wazi...maana tuliona kitu kimelala kitandani na kwa haraka haraka huwezi jua kama ni binadamu jinsi kansa ilivyomharibu..
.hujui kichwa kiko wapi..pua..wala mdomo...Tukapita pale na kuendelea ....wengine hata ukiwapa pole wanakutazama tu machozi yanawatoka maana kwa wakati ule pole haina maana yeyote..
Baada ya mzunguko wote tulikuwa macho mekundu kabisa kwa uchungu.
Nikamwambia asante kwa kunisindikiza..
.naomba sasa tuongelee yale ya jana wakati tunarudi.
Akasema..no.no.no..kwanza namshukuru Mungu sana kwa haya ya kwangu...nimepona kaka...mimi sina tatizo kaka ..maaana hwa wagonjwa wasemeje sasa..akanambia kaka nimeelewa kwa nini umenileta huku..Mungu nisamehe na wape kupona hawa ndugu zetu.
Laiti kama kila mtu angetembea na Ubao wenye orodha ya matatizo yake usoni...nakuhakikishia..hayo yanayokutatiza wewe sasa...ungeona kama uko mbinguni...
Wakti wewe unalalmika na Kumlaumu Mungu amekuacha eti hujaolewa, hujaoa, huna kazi, huna nyumba, huna mtoto...
Kuna mtu muda huu yuko msituni anakwepa risasi, yuko kitandani anaoza, yuko mahututi anapumulia machine..Kuna mama mjamzito wakati huu anapoteza maisha wakati wa kujifungua..yupo baba muda huu anapiga yowe kilio cha kumpoteza mkewe...Yupo mtu anapasuka kichwa dakika hii kwa ajali ya gari
Hebu fumba macho kidogo ,tafakari..na naomba ufanye uhakiki wa hali yako.....Kama kweli ni zaidi ya haya..basi ruksa kumlaumu Mungu, Ruksa kukata tamaa..Ruksa kudhani Mungu anakuonea, Ruksa kusema Kwanini mimi tu Mungu..
HEBU SIMAMA ..SHUSHA PUMZI..SEMA ASNTE MUNGU
Acha kulalamika rafiki, Acha kumlaumu Mungu...uliyonayo ni saizi yako..Mwombe Mungu akufunulie kilichoko ndani ya jaribu lako.
. (SHARED)