Makapuku Forum

Makapuku Forum

4c672f9dcec9fb0567eda947e90876fd.jpg
Umaskini ni sawa na matusi mnaweza kushindwa ht kuizika maiti......tutafute hela jamani tusije kufa na kuacha soo

.................
Sana aisee
 
MASOMO MATATU

SOMO LA KWANZA.

Nilikuwa kanisani nikimsikiliza muhubiri mmoja maarufu, muhibiri alitoa mfukoni noti za shilingi elfu kumi kumi zilizokuwa na jumla ya Tsh laki moja, akauliza, "ni nani miongoni mwenu anataka nimpe hii laki moja?"

Watu wengi waliokuwa mle kanisani walinyosha mikono, kila mmoja alikuwa akishauti mimi! Mimi!. Nikaanza kushangaa ni nani atakuwa na bahati ya kupewa ile pesa kati ya mamia ya watu waliohudhuria ile ibada.

Pia nikajiuliza kwa nini (ambapo bila shaka na baadhi ya wahudhuriaji wengine nao walijiuliza) atoe kitita cha shilingi laki moja kirahisi rahisi hivyo.

Wakati watu wakiendelea kupiga kelele kusema nipe mimi, nipe mimi huku wamenyosha vidole vyao, kutokea nyuma akaibuka msichana mdogo mwenye umri kama miaka 18 hivi, akaenda mbele kule aliko yule muhubiri akafika mbele na kuchukua ile laki moja kutoka mkononi mwa yule muhubiri.

"Safi sana, msichana! Umefanya vema," alisema yule muhubiri.
"Wengi wetu tunapenda kukaa tu na kusubiri mambo mazuri yaje yenyewe. Hii haitaweza kuwasaidia hata kidogo, unatakiwa kuinuka na kutafuta mafanikio. Mafanikio hayawezi kuja kama umekaa tu.

Na maisha yetu ndivyo yalivyo, tunaziona fursa nyingi sana zikiwa zimetuzunguka, kila mtu anahitaji mambo mazuri. Ila tatizo hatutaki kusimama na kuzifuata hzo fursa. Simama sasa na ufanye kitu, usisubiri mafanikio huku umekaa, kamwe hayatakuja. Usijali kuhusu watu watasema nini. Chukua hatua.

SOMO LA PILI.

Baadae yule muhubiri akatoa tena noti ya shilingi 10000 na akainyanyua ili wote tuione. Nikafikiri anarudia kama mwanzo tena. Lakini akauliza swali jepesi. "Noti hii inathamani gani?" Waumini wakajibu "shilingi elfu kumi". "Mko sahihi" akawajibu.

Akaichukua ile noti akaifinyanga finyanga na kuwauliza tena noti ile inathamani ya shilingi ngapi!? "shilingi elfu kumi" wakajibu wale wauminii!

Akaitupa chini ipe noti, akaikanyaga kanyaga sana, akaichukua na kuuluza tena noti hii ina thamani ya kiasi gani? "Shilingi elfu kumi" waumini walijibu vilevile.

Muhubiri akawaambia nataka muweka katika akili yenu hili, "mtu hata aichakaze, aikunje kunje na kuikanyaga noti ya fedha, thamani ya noti itabaki pale pale."

"Maisha yetu ndivyo yalivyo, tunatakiwa tuwe kama noti ya shilingi elfu kumi. Ktk maisha kuna kipindi tutasalitiwa, tutakanyagwa, tutaonewa na kupigwa. Ila usiache thamani yako ipotee, kwa sababu mtu amekuumiza tu, hiyo haimaanishi ndio thamani yako imepotea. Wewe ni wa thamani mno jinsi ulivyo. Usiache thamani yako ipotee kwa sababu ya wachache!

SOMO LA MWISHO.

Njia tofauti, jibu moja.
2+5=7
6+1=7
3+4=7
7-0=7
7+0=7
9-2=7
8-1=7

Pointi yangu iko wapi?

Pointi yangu ni kwamba kuna njia nyingi za kufikia mafanikio yako. Mungu hawezi kukufikisha katika mafanikio yako labda kama mama yako, baba yako, marafiki au ndugu walivyofanikiwa, kila mmoja hua na njia ya mafanikio tofauti Mungu aliyompangia.

Unaweza fikia mafanikio yako aitha kwa kuongeza watu katika maisha yako au kupunguza watu. "kujumlisha na kutoa" marafiki na baadhi ya vitu katika maisha yako kunaweza kusiwe kwa furaha kwa upande wako, ila Mungu ana makusudi yake.

Katika safari yako unaweza ukakumbana na kusalitiwa, kuumizwa kihisia, kuchekwa na kusimangwa! Acha kulia na futa machozi yako kila hali unayopitia ina makusudi yake. Mungu anakutengeneza uwe bora zaidi ya hivyo ulivyo.
By
Jibu langu ni jepesi tu

TUTAKUA KAMA VILE MUNGU ALIVYOTUPANGIA TUWE!
Mungu awabariki.
 
Habarini makapuku;
Natambua uwepo wa bitoz, Jimena, musolin5, werrason na shululu kwa wakati huu.
Musolin5 ametukumbusha jambo muhim sana lililotuunganisha tukawa family, hakika ni family sababu kila siku lazima tukutane, tusalimiane, tufundishane, tukosoane nk.
Mshikamano wetu umekua sana ndani na nje ya kf, nami nasema hongera kwa waasisi na members wote.
Kama tujuavyo wanadamu hatukosi mapungufu, hata kwetu hujitokeza, na yakijitokeza hurekebishana na maisha yanasonga. Jambo la msingi ni tumefahamiana kiasi flani na hii imetupa fursa ya kuvumiliana na mambo yanasonga.
Jambo lingine; tulikuwa wengi lakini kwa sasa tuko wachache LAKINI TUPO IMARA KULIKO WAKATI WOWOTE, cha msingi ni kushikamana zaidi na KUONGEZA UBUNIFU NA LUGHA ZA STAHA MIONGONI MWETU.
Wale ambao hawaonekani aidha;
1) kukosa uvumilivu
2)kutingwa na majukumu
3)kukosa mb
4) au hata kujitoa
Hili lisiwe tatizo sisi tuendelee tukiwa wamoja na kuleta ubunifu ili kuleta mvuto zaidi. Na ndg zetu wakirudi pia itakuwa jambo la kheri kwetu na wasiporudi isiwe tabu pia.
Ni maombi yangu kama family tutambue tuna wajibu wa kuchukuliana, kupendana na kuvumiliana.
Mwisho ni maombi yangu kf idumu zaidi.
Nawaomba mniruhusu wanaume wenzangu ni mpongeze huyu kiumbe jimena a.k.a jike shupavu, mwanamke wa shoka, kwa kusimama kidete peke yake bila kukata tamaaa, najua dada zake ipo siku watarudi.
Nawapenda wote mliopo
Pia nawamiss waliotingwa na walio tuacha, nawakaribisha tena na tena tulisongeshe
 
Habarini makapuku;
Natambua uwepo wa bitoz, Jimena, musolin5, werrason na shululu kwa wakati huu.
Musolin5 ametukumbusha jambo muhim sana lililotuunganisha tukawa family, hakika ni family sababu kila siku lazima tukutane, tusalimiane, tufundishane, tukosoane nk.
Mshikamano wetu umekua sana ndani na nje ya kf, nami nasema hongera kwa waasisi na members wote.
Kama tujuavyo wanadamu hatukosi mapungufu, hata kwetu hujitokeza, na yakijitokeza hurekebishana na maisha yanasonga. Jambo la msingi ni tumefahamiana kiasi flani na hii imetupa fursa ya kuvumiliana na mambo yanasonga.
Jambo lingine; tulikuwa wengi lakini kwa sasa tuko wachache LAKINI TUPO IMARA KULIKO WAKATI WOWOTE, cha msingi ni kushikamana zaidi na KUONGEZA UBUNIFU NA LUGHA ZA STAHA MIONGONI MWETU.
Wale ambao hawaonekani aidha;
1) kukosa uvumilivu
2)kutingwa na majukumu
3)kukosa mb
4) au hata kujitoa
Hili lisiwe tatizo sisi tuendelee tukiwa wamoja na kuleta ubunifu ili kuleta mvuto zaidi. Na ndg zetu wakirudi pia itakuwa jambo la kheri kwetu na wasiporudi isiwe tabu pia.
Ni maombi yangu kama family tutambue tuna wajibu wa kuchukuliana, kupendana na kuvumiliana.
Mwisho ni maombi yangu kf idumu zaidi.
Nawaomba mniruhusu wanaume wenzangu ni mpongeze huyu kiumbe jimena a.k.a jike shupavu, mwanamke wa shoka, kwa kusimama kidete peke yake bila kukata tamaaa, najua dada zake ipo siku watarudi.
Nawapenda wote mliopo
Pia nawamiss waliotingwa na walio tuacha, nawakaribisha tena na tena tulisongeshe
Nakuona th name japo unaadimika kaka, briz pia nakuona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom