Makapuku Forum

Kuelekea 01/6/2016.
"SIMU FEKI KUZIMWA"
SHAIRI LA KUWAAGA BAADHI YA WADAU WA FORUM HII

Twahuzunika kwakweli,
Makamanda wa ukweli,
Kwa kuwaaga kwaheli,
Nunua nyingine rudi.

Hiyo ni kama ajali,
Simu yako si halali,
Kuwa nayo si kibali,
Nunua nyingine rudi.

Inaumiza ni kweli, gharama kuikabili,
Simu yako kubadili,
Nunua nyingine rudi.

Hii ndyo serikali,
Meamua kukatili,
Simu ziso na kibali,
Nunua nyingine rudi.

Twakuhitaji kwakweli,
Kwenye kundi letu hili,
Twaliona pengo hili,
Nunua nyingine rudi.

Ndg wala usijali,
Simu yako kubadili,
Mana si la kujadili,
Nunua nyingine rudi.

Huwezi kupinga hili,
Ni lazima ukubali,
Mana meshika makali,
Nunua nyingine rudi.

Mpendwa kila lakheri,
Kwa ya dukani safari,
Simu feki ni hatari,
UNAWEZA KUZIMIA...
 
Daaah!!!

Ndo tuna malizia malzia sasa
 
Daaah.....
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…