Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,870
Mwanaume Wilaya ya Kayunga nchini Uganda (jina linahifadhiwa), ametozwa faini ya Sh400,000 (sawa na Sh600, 000 za Uganda) kwa madai ya kufanya mapenzi na mpenzi wake kwenye mimbari ya kanisa.
Wakazi wa mji huo wameuambia mtandao wa Monitor kuwa wiki iliyopita, waliwapata wawili hao wakifanya kitendo hicho ndani ya jengo jipya la kanisa la Bugonya katika Kaunti Ndogo ya Kayonza nchini humo.
Tukio hilo lilitengeneza vichwa vya habari kwa ‘utatu’ wake usio wa kawaida kwani mwanamume Mkatoliki alikutwa akifanya mapenzi na mwanamke Mwislamu kwenye madhabahu ya Kanisa la Anglikana.
Wawili hao walipelekwa hadi kwa Afisa namba moja moja wa eneo hilo (LC1), ambapo waliachiliwa wakisubiri kusikilizwa kwa kesi yao, hata hivyo, mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 23 ametoweka.
Inasemekana mwanaume huyo anajificha kwa rafiki yake katika kijiji hicho, huku mwanamke ambaye ni ametalakiwa, akiwa amechukuliwa na mama yake.
Wakazi wa mji huo wameuambia mtandao wa Monitor kuwa wiki iliyopita, waliwapata wawili hao wakifanya kitendo hicho ndani ya jengo jipya la kanisa la Bugonya katika Kaunti Ndogo ya Kayonza nchini humo.
Tukio hilo lilitengeneza vichwa vya habari kwa ‘utatu’ wake usio wa kawaida kwani mwanamume Mkatoliki alikutwa akifanya mapenzi na mwanamke Mwislamu kwenye madhabahu ya Kanisa la Anglikana.
Wawili hao walipelekwa hadi kwa Afisa namba moja moja wa eneo hilo (LC1), ambapo waliachiliwa wakisubiri kusikilizwa kwa kesi yao, hata hivyo, mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 23 ametoweka.
Inasemekana mwanaume huyo anajificha kwa rafiki yake katika kijiji hicho, huku mwanamke ambaye ni ametalakiwa, akiwa amechukuliwa na mama yake.