Princess Diana akiwa na baba mkwe wake, Mohamed Al Fayed. Huyu ndiye baba yake Dodi Fayed aliyekuwa mchumba wa Princess Diana.
Mwaka 1997 Diana na Dodi walifariki kwenye ajali ya gari huko Paris, Ufaransa wakati dereva wao alipokuwa akiwakimbia waandishi wa habari.
Mzee huyu anasema Diana na mwanaye walikuwa wamepanga kuoana na siku moja kabla ya kifo chao walikuwa wamepanga kuvishana pete za uchumba.
Baada ya kifo cha Diana, Mzee huyu alifungua kesi mahakamani akidai kwamba wapenzi hao waliuwawa, hata hivyo mahakama iliamua kwamba kifo cha Diana na Dodi kilisababishwa na uzembe wa Dereva.
Hata hivyo bado Mzee huyu anaamini kwamba mtoto wake aliuwawa na vyombo vya ulinzi vya Uingereza na anasema anaamini ipo siku mambo yatakuwa hadharani.
Mzee Mohamed ni mzaliwa wa Misri. Kwa sasa Mzee Mohamed ana umri wa miaka 94 anaishi Uingereza na muda mwingi amekuwa akiutumia kukaa pembeni ya kaburi la mwanae...!
View attachment 2689753