Makapuku Forum

Makapuku Forum

OFFICIAL & CONFIRMED:
.
Klabu ya Yanga imethibitisha kukamilisha usajili wa beki wa kulia Kouassi Attohoula Yao kutoka Asec kwa Mkataba wa mwaka mmoja.
.
Yao (26) anahesabika kuwa beki bora wa kulia pia na ubora wa kucheza kama winga mshambuliaji na kupiga krosi za mabao.
Screenshot_20230715_052323_Instagram.jpg
 
NAHODHA wa timu ya taifa, Taifa Stars na mshambuliaji wa Fenerbahce, Mbwana Samatta yupo mbioni kujiunga na PAOK inayoshiriki Ligi Kuu nchini Ugiriki.
.
Samatta ambaye msimu uliopita alikuwa anacheza kwa mkopo Genk, aliifungia timu hiyo mabao sita katika Ligi Kuu na kuifanya PAOK kuitaka saini yake.

Taarifa za Uturuki zinaeleza tayari Samatta ameshafanya makubaliano na PAOK kwa ajili ya kuitumikia msimu ujao. Samatta anatarajiwa muda wowote kwenda Ugiriki kufanya vipimo vya afya na kusaini.
Screenshot_20230715_052605_Instagram.jpg
 
Fulham inataka kuwasilisha ofa nyingine kwa mshambuliaji wao Willian, 34, ili kumshawishi asaini mkataba mpya wa kuendelea kusalia kwenye viunga vyao baada ya mkataba wake wa sasa kumalizika.

Staa huyo wa kimataifa wa Brazil pia anahusishwa na Nottingham Forest na baadhi ya timu kutoka Saudi Arabia, msimu uliopita alifunga mabao matano kwenye mechi 30 za michuano yote alizocheza
Screenshot_20230715_052702_Instagram.jpg
 
Ofa ya Inter Milan kwa Chelsea ni €35m na nyongeza ya €5m kumsajili Lukaku.

Inter bado hawajatoa jibu kuhusu kukamilisha usajili huo, hii ni baada ya kuonekana Lukaku akifanya mazungumzo na Juventus ambao walituma ofa kwenda Chelsea ya €37.5m na nyongeza ya €2.5m Ili kumsajili Lukaku kitendo ambacho Inter hakijawapendeza .

Inter or Juventus ? Chochote kinawezekana
Screenshot_20230715_052803_Instagram.jpg
 
Naibu Mkuu Kadhi wa Zanzibar Sheikh Othman amemshukuru Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Ali Mwinyi kwa kuridhia ombi la siku ya mwaka mpya wa Kislam Hijjria iwe siku maalum kitaifa na iwe na mapumziko kiserikali kama zinavyoadhimishwa siku nyingine.

Hii ni baada ya Waumini wa Dini ya Kiislam Zanzibar kumuomba Rais Mwinyi ambapo aliomba kupewa muda kulifikiria hilo lakini sasa ameridhia hivyo July 19 Mwaka mpya huo utasherekewa kitaifa na kua siku ya mapumziko Zanzibar.

"Nipongeze juhudi na jitihada kubwa zilizochukuliwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar na Wasaidizi wake katika kuhamasisha na kuitaka siku hii iwe rasmi na itambulike kitaifa ,nimpongeze Rais Mwinyi kwa kuweza kutukubalia, Zanzibar katika Bara la Afrika ni Nchi ya kwanza kwenye hili" ——— Sheikh Othman.
Screenshot_20230715_053217_Instagram.jpg
 
Beki wa zamani wa Man City na Timu ya Taifa ya Ufaransa Benjamin Mendy (28) amekutwa hana hatia katika kesi ya ubakaji iliyokuwa inamkabili na kumfanya asimame kucheza soka.

Mendy aliyekuwa anatuhumiwa kubaka Wanawake kwa vipindi viwili tofauti, alituhumiwa kumbaka Mwanamke mwenye umri wa miaka 24, October, 2020 chumbani kwake Cheshire Jijini Manchester, miaka miwili nyuma pia alituhumiwa kufanya jaribio la kutaka kumbaka Mwanamme wa miaka 29 nyumbani kwake Cheshire.

Mendy baada ya kukutwa hana atia alivyotoka nje ya Mahakama Waandishi walimuuliza ana nini cha kuzungumza kwa Mashabiki wa Soka Duniani kote ambapo amejibu kwa neno moja tu la kiarabu “Alhamdulillah”.
Screenshot_20230715_053313_Instagram.jpg
 
Rais wa Kenya, William Ruto amemtuhumu mtangulizi wake, Uhuru Kenyatta kuwa anafadhili maandamano ya upinzani nchini humo.

Akizungumza huko Kaunti ya Nakuru leo Julai 14, 2023, Ruto amedai kuwa Kenyatta alikuwa akiwafadhili vijana wa Mungiki kufanya fujo wakati wa maandamano ya Azimio la Umoja nchini humo.

Rais Ruto ameonya kuwa ikiwa Rais huyo wa zamani ataendelea kufadhili shughuli za Azimio, atalazimika kumchukulia hatua.

Amemtaka Kenyatta kuwa muungwana, akisema kuwa yeye alimuunga mkono katika kipindi akiongoza nchi hiyo, huku akimtaka Kenyatta kuacha kujihusisha na kiongozi wa ODM, Raila Odinga.

“Nikuombe rafiki yangu Uhuru, achana na huyo mzee (Raila), acha kutoa pesa za kuajiri mungiki kuiharibu Nairobi, wewe ulikuwa Rais tukakuunga mkono, tafadhali kuwa muungwana,” amesema Rais Ruto. (Victor Tullo, Mwananchi)

Screenshot_20230715_053428_Instagram.jpg
 
Mchezaji wa zamani wa Manchester City, Benjamin Mendy amefutiwa mashtaka yake mawili ya kudaiwa kubaka na kujaribu kubaka wanawake wawili tofauti.

Mendy (28) alishtakiwa kwa shtaka la kwanza la kumbaka mwanamke mwenye umri wa miaka 24 katika kijiji cha Mottram St Andrew, Uingereza mnamo Oktoba 2020 na jingine pia la kujaribu kubaka mwanamke mwenye umri wa miaka 29.

Beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa, ambaye alikuwa amekanusha mashtaka yote mawili, alikutwa hana hatia na Mahakama ya Chester Crown.

Mchezaji huyo aliangua kilio baada ya kusomewa kuwa hana hatia na msimamizi wa mahakama kufuatia kesi iliyodumu kwa wiki tatu katika Mahakama ya Chester Crown huku Jaji Steven Everett akisema; "Mendy anaweza kuachiliwa kutoka kizimbani."
Screenshot_20230715_053603_Instagram.jpg
 
Bunge la Ukraine limepiga kura kupitisha sheria inayoridhia matumizi ya bangi kwa maveterani wa vita kama mbinu ya kuwasaidia kupambana na kiwewe kinachotokana na vita inayoendelea kati ya nchi hiyo na Russia.

Mtandao wa The Telegraph umeripoti jana Julai 13, 2023 kuwa mswada huo unaoridhia matumizi ya bangi kama tiba uliwasilishwa bungeni kwa mara ya kwanza Alhamisi ya Julai 13, mwaka huu huku, watunga sheria 268 kati 344 wakiupigia 'kura ya ndiyo.'

Muswada huo unasubiria kusomwa na kupitishwa kwa mara ya pili bungeni kabla ya kuwasilishwa mbele ya Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky kwa ajili ya kutiwa saini kuwa sheria.

Matumizi ya bangi kama tiba yamekuwa yakipigiwa chapuo nchini Ukraine huku msukumo zaidi wa kupitisha sheria inayoruhusu, ukiongezeka tangu kuanza kwa kinachoitwa uvamizi wa Russia nchini humo. (Mgongo Kaitira, Mwananchi)

Screenshot_20230715_053722_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom