Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi Rajab Omar Luhwavi kuwa Mshauri wa Rais kwenye Siasa na Uhusiano wa Jamii ambapo Balozi huyu alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji.

Vilevile Rais amemteua Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na Waziri Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Haji Omar Kheir kuwa Mshauri wa Rais upande wa Siasa na Uhusiano wa Jamii.
Screenshot_20230614_053553_Instagram.jpg
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua Mbunge wa Isimani Iringa William Vangimembe Lukuvi kuwa Mshauri wa Rais (Siasa na Uhusiano wa Jamii), Lukuvi ni Mbunge wa Jimbo la Isimani, Iringa.

Rais Samia pia amemteua Mbunge Mstaafu Abdallah Bulembo kuwa Mshauri wa Rais (Siasa na Uhusiano wa Jami).
Screenshot_20230614_053703_Instagram.jpg
 
Waandaaji wa Tuzo kubwa na maarufu za Grammy za Nchini Marekani wameongeza Vipengele vitatu vipya kwenye Tuzo hizo kuanzia mwaka 2024 ambapo moja ya vipengele hivyo ni BEST AFRICAN MUSIC PERFOMANCE ambacho ndani yake kina miziki mbalimbali ya Afrika ikiwemo Bongofleva.

Taarifa rasmi ya Grammy imeeleza yafuatayo ——— > “Lengo letu ni kutambua na kuheshimu nyimbo bora zaidi kutoka kote ulimwenguni, kila mwaka tunajitahidi kuwakilisha na kusherehekea kwa usahihi tamaduni, mvuto wa aina mbalimbali unaoutengeneza ulimwengu wetu"

"Leo tunajivunia kutangaza kitengo kipya cha Tuzo za 66 za Grammy, Best African Music Perfomance, kitengo hiki cha wimbo na single hutambua rekodi zinazotumia misemo ya kipekee ya nadani kutoka katika Bara zima la Afrika, kitengo hiki kinajumuisha Afrobeat, Afro-fusion, Afro pop, Afrobeats, Alte, Amapiano, Bongo flava, Genge, Kizomba, Chimurenga, High Life, Fuji, Kwassa, Ndombolo, Mapouka, Ghanaian Drill, Afro-house, Muziki wa Hiphop wa Afrika Kusini, Ethio Jazz n.k" ——— imeeleza taarifa ya Grammy leo.

Tuzo za Grammy zilianza kutolewa Nchini Marekani miaka 64 iliyopita (May 4 1959) na zinatajwa kuwemo kwenye orodha ya Tuzo nne kubwa za burudani Nchini Marekani.
Screenshot_20230614_054128_Instagram.jpg
 
Mahakama ya Wilaya ya Babati Mkoa wa Manyara imemuhukumu Gurtu Sirro (33) Mkazi wa Sarame Magugu kifungo cha miaka 20 kwenda jela baada ya kukutwa na meno matatu ya Tembo ambayo thamani yake ni zaidi ya shilingi Milioni 45.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu wa Mahakama hiyo Victor Kimario ambapo amesema Sirro alikamatwa January 17,2023 katika Kijiji cha Mafuta akiwa na meno matatu ya Tembo ambayo ni nyara za Serikali.

Waendesha mashtaka wa Serikali katika kesi hiyo Rusticus Mahundi na Abood Komanya wamesema Mshtakiwa hana rekodi zozote za matukio kama hayo hivyo wameiomba Mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa Watu wengine wenye tabia kama hizo huku Mshtakiwa (Gurtu Sirro) akiiomba Mahakama imuondolee adhabu hiyo kwa kuwa anategemewa na Watoto wanne ambao Mama yao hawezi kufanya kazi hivyo wanamtegemea yeye pekee.

Hakimu Kimario amesema Mshtakiwa anayo haki ya kukata rufaa ndani ya siku 30 kuanzia leo huku akiagiza meno hayo ya Tembo ambayo yalitumika kama kielelezo namba moja kukabidhiwa kwa Afisa Wanyamapori wa Wilaya ili kuyapeleka sehemu husika kwa mujibu wa sheria.
Screenshot_20230614_054257_Instagram.jpg
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki Tamasha la Utamaduni la Bulabo Mkoani Mwanza leo June 13,2023 ambapo moja ya mambo aliyoyasema kwenye hotuba yake ni kuwaomba Wakulima kuhifadhi chakula na kutouza nje.

“Ndani ya Taifa letu sasa akiba ya chakula ipo kama Tani laki 2 hadi laki 2 na Elfu 50 kwa kuanzia mwaka huu mavuno yaliyoanza tunakwenda kumwaga fedha kununua chakula, tunataka kuwa na hifadhi ya chakula Tani laki 5 kwa mwaka huu tunaoanzia, Nchi yetu iwe na Tani laki 5 tutakazohifadhi kwenye maghala yetu, nimeshampa kibali Waziri wa Kilimo na Waziri wa Fedha atoe fedha tuanze kununua mazao sasa”

“Niwaombe sana Wakulima mazao tusivushe kwenda nje tusubiri Wizara inakuja kununua mazao ili tuweke kwenye hifadhi, naziomba Familia zote za Wakulima waweke chakula cha kutosha kwa ajili yao, nitoe wito kwa Wakulima kutunza chakula cha kutosha, kuweka akiba ya chakula kwa matumizi ya Familia na tusiuze chakula nje kibakie ndani kwa matumizi yetu, litakapokuja suala la uhaba wa chakula Tanzania tuwe tumejiweka vizuri hatuna shida ya chakula”

“Narudia tena tukumbuke kuweka akiba ya chakula, najua Ndugu zangu wa kisukuma mavuno haya tukishauza na bei zipo nzuri sasa wakina Baba tutakimbilia kuongeza nyumba za pili, mwenye mbili anakwenda ya tatu, si vibaya hatuna wivu hatukatai lakini mnapokumbuka kuongeza nyumba mkumbuke kuongeza na mashamba ili tuvune zaidi tuongeze chakula zaidi”
Screenshot_20230614_054434_Instagram.jpg
 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Dkt. Eliezer Feleshi amewasilisha muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali wa mwaka 2023 Bungeni Jijini Dodoma ikiwemo Sheria ya Mazishi ya Viongozi wa Kitaifa, Sura ya 419 ambapo pamoja na mambo mengine marekebisho haya yanakusudia kutoa mamlaka kwa Rais kutangaza tarehe ya maziko ya Rais aliyefariki akiwa madarakani kuwa ni siku ya mapumziko.

“Sehemu ya Tano ya Muswada inapendekeza marekebisho kwenye Sheria ya Mazishi ya Viongozi wa Kitaifa, Sura ya 419 ambapo kifungu cha 6 kinapendekezwa kufutwa na kuandikwa upya kwa lengo la kuboresha masharti kuhusu mamlaka ya Rais kutoa tangazo la kifo cha Kiongozi wa Kitaifa au Kiongozi mahsusi aliye madarakani”

“Marekebisho hayo pia yanampa mamlaka Kiongozi mahsusi aliye madarakani kutoa tangazo la kifo cha Kiongozi mahsusi mstaafu, vilevile marekebisho haya yanakusudia kutoa mamlaka kwa Rais kutangaza tarehe ya maziko ya Rais aliyefariki akiwa madarakani kuwa ni siku ya mapumziko”

“Lengo la mapendekezo haya ni kuweka bayana na kutofautisha mamlaka zinazopaswa kutoa matangazo ya vifo vya Viongozi wa kitaifa na Viongozi mahsusi, vifungu vya 9 na 10 vinapendekezwa kurekebishwa ili kutoa Mamlaka kwa Kiongozi mahsusi aliye madarakani kutoa tangazo la kifo cha Kiongozi mahsusi mstaafu, lengo ni kutambua utaratibu unaotumika sasa ambapo pamoja na kwamba Sheria imemtaja Rais kama mamlaka ya kutoa tangazo la kifo cha Kiongozi mahsusi mstaafu, matangazo ya aina hiyo kwa kawaida yamekuwa yakitolewa na Viongozi mahsusi walio madarakani”
Screenshot_20230614_054744_Instagram.jpg
 
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imezindua rasmi Ubalozi na Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa jijini Vienna nchini Austria.

Akizungumza katika uzinduzi huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dr. Stergomena Tax amesema kufunguliwa kwa Ubalozi huo ni mafanikio yanayoimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Austria na Taasisi za Umoja wa Mataifa zilizopo jijini Vienna na kinaonesha jinsi Tanzania inavyoipa kipaumbele Austria.

“Kufunguliwa kwa Ubalozi huu ni mafanikio makubwa ambayo yanaimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Austria na Taasisi za Umoja wa Mataifa zilizopo hapa jijini Vienna na kinaonesha kwa vitendo kuwa Tanzania inaipa kipaumbele Uhusiano wake na Austria” ——— alisema Dkt. Tax.

Ameishukuru Serikali ya Austria na Wizara inayoshughulikia masuala ya Ulaya na uhusiano wa Kimataifa kwa ushirikiano mkubwa ambao imekua ikiupatia Ubalozi wa Tanzania Vienna tangu ulipoanzishwa hadi kufikia siku ya uzinduzi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Ubalozi huo jijini Vienna Naibu Waziri anayeshughulikia Masuala ya Ulaya na Uhusiano wa Kimataifa Mhe. Peter Launsky-Tieffenthal amesema Austria inapongeza uamuzi wa Serikali ya Tanzania wa kufungua Ubalozi wake Austria na kuungana na nchi nyingine 16 za Afrika zenye Ubalozi nchini humo na kuahidi kuusaidia Ubalozi huo kwa kila hali ili kufikia malengo ya kuanzishwa kwake.
Screenshot_20230614_054913_Instagram.jpg
 
Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Haji Omar Kheir ambaye ni Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na Waziri mstaafu Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kuwa Mshauri wa Rais - Siasa na Uhusiano wa Jamii.

Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu mesema uteuzi huo umeanza leo Juni13, 2023.

Screenshot_20230614_055045_Instagram.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi Rajab Omar Luhwavi ambaye aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, kuwa Mshauri wa Rais - Sera na Uhusiano wa Jamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, uteuzi huo umeanza leo Juni 13, 2023

Screenshot_20230614_055151_Instagram.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan amemteua William Lukuvi, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Ismani mkoani Iringa, kuwa Mshauri wa Rais - Siasa na Uhusiano wa Jamii.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu iliyotumwa kwa vyombo vya habari, imesema uteuzi huo umeanza leo Juni 13, 2023
Screenshot_20230614_055244_Instagram.jpg
 
Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amemteua mwanasiasa Abdallah Bulembo ambaye ni Mbunge mstaafu, kuwa Mshauri wa Rais - Siasa na Uhusiano wa Jamii. Uteuzi huu umeanza leo Juni 13, 2023.

Screenshot_20230614_055336_Instagram.jpg
 
Dar es Salaam. Sakata la mkataba wa ushirikiano wa kiuchumi na kijamii wa uendelezaji wa bandari kati ya Tanzania na Dubai, lawaibua Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (Lhrc), ambao wataka Serikali kurejea upya vipengere vyenye changamoto kisheria.

Akizungumza leo Juni 13, 2023 Mkurugenzi Mtendaji Lhrc Anna Henga amesema Serikali inatakiwa kurejea upya vipengele vya mkataba vyenye changamoto ya kisheria, hususani vile vilivyoibua mijadala mikubwa kwa wananchi.

Ameitaka Serikali kuchukua hatua ya kufanya marekebisho mapema ili kuweka wazi, mazingira imara ya mkataba, ikiwemo mazingira ya kikodi yaainishwe bayana ili kuepuka kutumia mwanya huo kwa maslahi binafsi na kuumiza maslahi ya umma.

Hata hivyo Henga ameitaka Serikali kuweka wazi kiwango cha umiliki wa sehemu ya uwekezaji huo ili wananchi kufahamu faida itakayopatikana katika uwekezaji hususani katika mikataba ya utekelezaji wa mradi.

"Ni vema kuendelea kwa ari ya uwazi wa mikataba ya kiuwekezaji inayohusu maslahi mapana kwa Taifa kama ilivyojitokeza katika mkataba huu kati ya Serikali na Dp World,"amesema Henga.

Pia ameitaka serikali kuwepo na ushirikishwaji mpana wa wananchi kwani mkataba huu uliopitishwa na Bunge Juni 10, 2023 haukuwa na ushirikishwaji wa kutosha.

Kutokana na hayo wamependekeza mikataba iainishe ukomo wa juu na chini wa motisha ya kikodi zitakazotolewa katika mikataba mingine ya utekelezaji ili kuepuka kutumika vibaya kwa kipengele hicho kwa baadhi ya watendaji wa serikali wasio waaminifu.
Screenshot_20230614_055426_Instagram.jpg
 
Dar es Salaam. Mtu mmoja (23) amepoteza maisha na wengine nane kujeruhiwa, baada kuangukiwa na kontena lililokuwa limebebwa na gari aina ya Scania namba 171CAG, maeneo ya Yombo mwisho wa Lami (maarufu kwa jini), wilayani Temeke.

Taarifa za tukio hilo lilotokea leo juni 13,2023, zimethibitishwa na Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamanda wa Mkoa wa Temeke, Maria Luoga huku akibanisha tukio hilo lilitokea majira ya saa 2:24 mchana.

“Gari haikudondoka isipokuwa kontena ilidondokea nyumba ya kuishi lakini ndani yake kuna ofisi ya mchezo wa kubahatisha (betting), kifo killichotokea ni kimoja ambaye ni binti anayekadiriwa kuwa na miaka 23,” amesema na kuongeza;

“Majeruhi nane, na kati yao wawili kwa hali siyo nzuri na wamepelekwa kwa matibabu zaidi katika Hospitali ya Wilaya Temeke, majeruhi sita walitibiwa palepale kuna Dispensari inaitwa Malawi,” amesema.

Kamanda huyo amesema madhara kwa upande wa mali ni uharibifu wa nyumba moja lakini tathimini bado haijafanyika kujua thamani halisi ya uharibifu huo huku akieleza wanasubiri mkuu wa wilaya hiyo atume watathimini.

Amesema kuhusu chanzo cha ajali hiyo haijafahamika kwa sababu dereva wa gari hiyo amekimbia baada ya kutokea kwa tukio hilo.” Kesho nitakuwa na taarifa zaidi kwakuwa nitaamkia Hospitali ya Temeke,” amesema.
 
Dar es Salaam. Mtu mmoja (23) amepoteza maisha na wengine nane kujeruhiwa, baada kuangukiwa na kontena lililokuwa limebebwa na gari aina ya Scania namba 171CAG, maeneo ya Yombo mwisho wa Lami (maarufu kwa jini), wilayani Temeke.

Taarifa za tukio hilo lilotokea leo juni 13,2023, zimethibitishwa na Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Kamanda wa Mkoa wa Temeke, Maria Luoga huku akibanisha tukio hilo lilitokea majira ya saa 2:24 mchana.

“Gari haikudondoka isipokuwa kontena ilidondokea nyumba ya kuishi lakini ndani yake kuna ofisi ya mchezo wa kubahatisha (betting), kifo killichotokea ni kimoja ambaye ni binti anayekadiriwa kuwa na miaka 23,” amesema na kuongeza;

“Majeruhi nane, na kati yao wawili kwa hali siyo nzuri na wamepelekwa kwa matibabu zaidi katika Hospitali ya Wilaya Temeke, majeruhi sita walitibiwa palepale kuna Dispensari inaitwa Malawi,” amesema.

Kamanda huyo amesema madhara kwa upande wa mali ni uharibifu wa nyumba moja lakini tathimini bado haijafanyika kujua thamani halisi ya uharibifu huo huku akieleza wanasubiri mkuu wa wilaya hiyo atume watathimini.

Amesema kuhusu chanzo cha ajali hiyo haijafahamika kwa sababu dereva wa gari hiyo amekimbia baada ya kutokea kwa tukio hilo.” Kesho nitakuwa na taarifa zaidi kwakuwa nitaamkia Hospitali ya Temeke,” amesema.
Screenshot_20230614_061353_Instagram.jpg
 
Mwanamke wa makamo kutoka Ecuador aliyezinduka baada ya madaktari kutangaza kuwa amefariki, anapatiwa matibabu katika hospitali ya serikali ambayo ilitangaza kuwa amekufa siku mbili zilizopita, mtoto wake alisema Jumapili.

Video iliyotumwa kwenye Twitter inamuonyesha Bella Montoya, 76, kwenye jeneza likiwa wazi akipumua kwa nguvu huku wanaume wawili wakimsaidia.

Mtoto wake, Gilbert Balberán, alisema "alikuwa akipiga sanduku" kwa mkono wake wa kushoto baada ya kuamka kwa saa tano.

Balberán alilazimika kuomba mchango wa jeneza kwa familia maskini baada ya hospitali hiyo, kutangaza kuwa Montoya amekufa siku ya Ijumaa.

"Hata walitupa cheti cha kifo," alisema kwenye video iliyotangazwa na vyombo vya habari vya ndani.

Vyombo vya habari vya Ecuador viliripoti tukio hilo lisilo la kawaida, na vichwa vya habari vikisheheni ‘kufufuka’ kwa mwanamke huyo.

"Mama yangu amepata oksijeni. Moyo wake uko shwari. Daktari alimfinya mkono wake na akaitikia," Balberán alisema katika ripoti ya gazeti la El Universo.

"Wananiambia kuwa hii ni nzuri, kwa sababu ina maana kwamba anarejesha afya yake taratibu."

Montoya alilazwa hospitalini akiwa na kiharusi "na alikuwa hapumui kutokana na mapigo ya moyo kusimama, kwa hivyo daktari wa zamu alithibitisha kifo chake," Wizara ya Afya ya Ecuador ilisema katika taarifa yake Jumapili.

Wizara ilisema kuwa imeunda kamati ya kuchunguza tukio hilo na kwamba itasimamia uangalizi wa Montoya.

Balberán alisema alikuwa amemtembelea mama yake katika chumba cha wagonjwa mahututi siku ya Jumapili.

"Kidogo kidogo naelewa kilichotokea. Sasa namuombea tu afya ya mama yangu iwe bora. Namtaka awe hai na awe upande wangu," alisema
Screenshot_20230614_061833_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom