Farhan Jr
Leo naomba niongee na CEO wangu Kajula kuhusu Simba Sports kidogo!
Kaka mkubwa Iman Kajula, tuna mambo kadhaa kwanza tuhakikishe utamaduni wa kuwa na Kocha Mzawa kwenye set up yetu, Kocha anayejua soka la Tanzania pamoja na utamaduni wake! Tunaweza kuwa na Robertinho pamoja na Msaidizi wake (Kwa mujibu wa mapendekezo yake) ila tuwe na Msaidizi wa pili ambaye ni Mtanzania hii ina maana kubwa sana.
Point yangu ni nini? Point ni kuwa Robertinho anaweza kuhitaji Msaidizi wake ila Baba Mkwe Mgunda akasalia kama Msaidizi wa pili ikimpendeza ama yoyote kwa ajili ya kuchota vitu zaidi ikitokea wameondoka, timu haiyumbi sana kimfumo, anakuwa caretaker mzuri kabla ya mipango ya klabu kuleta Kocha mpya.
Lakini faida yake nyingine inafahamika kupata mawazo tofauti tofauti! Mfano Mamelodi wana Makocha watatu wa viwango, nadhani hii ni nzuri sana! Msaidizi wa Robertinho anaweza kuja na bado Mgunda akasalia klabuni.
Kaka CEO suala lingine ni hili la Mkurugenzi wa Ufundi na Mkurugenzi wa mpira! Huyu aje kuitazama timu, atuundie falsafa yetu ili mpira wa kufanana uanze timu ya vijana mpaka senior team!
Boss MO alisema ana ndoto ya timu za Vijana bora lakini itafanikiwa kwa falsafa za kufanana, leo hii Mamelodi tunaona wanavyofaidika na watoto kutoka timu B! Leo hii tunaona Generation Foot inavyoifaidisha Senegal! Tukiwa na falsafa tutajua tunataka wachezaji gani wa kuendana nasi.
CEO la mwisho ni hili la Legends wetu wa Simba! Tuwe na utamaduni wa kuwapeleka shule wachezaji wetu wa zamani, baadhi wakasomee Ukocha waanze na timu zetu za Vijana seriously na wapelekwe course mpaka nje ya nchi wapate exposure zaidi na zaidi.
CEO hata Watendaji wa klabu tunaweza kuwapata kutoka kwa Legends wetu, uwepo mpango maalum wakale kitabu ili wakija kuwa Maafisa wa klabu watashauri kwa ufasaha.
Wasalaam!