Farhan Jr
Nakumbuka mengi kuhusu mpira, nakumbuka the rainy nights in Stoke wakati Stoke City wakiwa uwanjani ile Jumatatu ya mvua na baridi kali, leo hawapo tena na mitaa inasema “Bring back our rainy nights in Stoke” yes! Ryan Shwacross atapiga munda kama hajui kitu na Howard Webb atapeta kama hakijatokea kitu.
The Good old days! Usiku wa kelele nyingi kwenye jiji la mitindo Milano! At the heart of fashion there is football! Wanaliita tempo la mpira ndio San Siro! Pale Ricardo Kaka na Seedord juu yupo Philpo Pippo Inzaghi, touchline ni Don Carlo na ufundi wake.
Ziko wapi nyakati? Wakati Manchester United wanavaa AIG, Arsenal wana O2! Liverpool wana Carlsberg na Chelsea wana Samsung Mobile, kabla ya Nandy kuwa mainstream, Zuchu ni bikra huko Paje! Lulu Diva hajui wanaume na Gigy Money yupo Mbeya anashindia parachichi.
Gone are the days! Wakati Fergie anatafuna big G ya mamillion, Wenger na makoti ya bei mbaya! Fabregas mtoto hapo analelewa kwa Mama wa Kiingereza, Man City wana Mido Upara Stephen Ireland kabla ya Kipara Guardiola, utaniambia nini?
The days! Jay Jay Okocha anapiga goli anaenda kukatika kuliko Angel Nyigu! Kipindi hicho EPL ni TVT na Star TV, kabla ya Instagram na Matonya anaitwa Seif Shabaan, enzi hizo sisi ni Chawa halisi wa game kabla ya Mwijaku na GSM, kipindi hicho Mond anamtazama Baba Levo kama role model.
Zipo wapi nyakati? Bambo na Senga, Steven Gerrard na Alonso Xabi! Ray na Kanumba, Patrick Viera na Roy Keane! Zipo wapi nyakati? Au lipigwe goli nislide kama Didier Drogba kwenye DM ya Hamisa? Hapana Kaka Ali atanipiga
Zipo wapi nyakati?