Makapuku Forum

Makapuku Forum

duh, kumbe ndiyo iko hivi. Inaweza kuwa imetafsiriwa kutoka anga za Kanada na Marikani wanakowaita 'aliens'.
Kwa hiyo Lee ni ajinabi hapa Bongo.



Makiwendo you are missed big time. Bado naendelea kuuliza kama TCRA wanawea kunipatia namba yako ya simu
Shunie mara zaote asante kwa magazeti na Je wajua
mkwepu jr popote ulipo kula chuma hicho, kivumbi leo , like-d the like
makaveli10 mdau veterani huna baya na mtu nakusalimia mwanaSimba

Makapuku, sehemu nzuri kabisa kuwepo sababu wewe upo
Asante binamu yangu kwa kushukuru mkwepu jr apewe maua yake tu
 
Moja ya tukio lililojitokeza Bungeni Jijini Dodoma leo May 9, 2023 ni pamoja na Mbunge wa Tarime Vijijini, Mwita Waitara kutoka nje ya ukumbi wa Bunge huku akivua koti na tai baada ya kuonesha kutoridhidhishwa na majibu ya Serikali wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

Mbunge Waitara baada ya kutoka nje ya ukumbi wa Bunge, ameongea na @ayotv_ ambapo pamoja na mambo mengine amemuomba Rais wa Tanzania Dkt. Samia kuingilia kati suala fidia katika baadhi ya maeneo ya mgodi wa Barrick North Mara.

“Mimi nimetembea usikuusiku na Watu wanajua leo kuna majibu ya Serikali sasa kwa majibu haya unaenda kuwaambia kitu gani?, imagine Mtu ameondolewa eneo miaka 11, Waziri wa Madini aliahidi haitofika mwezi wa sita “

“Juzi RC alikuwa anatukana mbele ya Mabula, kuhusu kama nitarudi Bungeni au laah vikao vinaendelea ngoja nipumzike nitajua cha kufanya, Watu wamekaa kwenye Hifadhi zile kabla ya Uhuru leo unawaambia waondoke waende wapi”

“Rais aingilie kati hapa kuna shida, na kama kuna Mtu hamtaki Waitara Tarime aseme Mimi nipo tayari kuachia ngazi ili wamuweke wanayemtaka pale lakini hakuna Mbunge atakuwa Mjinga anaona Watu wake wanaumia”
Screenshot_20230510_051703.jpg
 
Jeshi la Polisi Tanzania limesema linatarajia kumuaga rasmi aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Mstaafu Balozi Simon Nyakoro Sirro, tarehe 10 Mei 2023 baada ya kustaafu Utumishi ndani ya Jeshi la Polisi kwa mujibu wa sheria mwezi Machi 2023.

Sherehe za kumuaga IGP Mstaafu Balozi Simon Nyakoro Sirro zitafanyika katika Chuo cha
Taaluma ya Polisi Dares Salaam (DPA) kilichopo Kurasini Jijini Dar es salaam kuanzia saa moja asubuhi kwa gwaride maalum la kumuaga ikiwa ni utaratibu wa Jeshi la Polisi kuwaaga kwa gwaride maalum Viongozi wa Polisi waliofikia cheo cha Kamishna wa Polisi na Inspekta Jenerali wa Polisi.

Polisi imesema IGP Mstaafu Balozi Simon Nyakoro Sirro amelitumika Jeshi la Polisi kwa miaka 30 tangu tarehe 19 Februari 1993 alipojiunga rasmi hadi kustaafu mwezi Machi, 2023 na ni Mkuu wa Jeshi la Polisi wa 10 kuliongoza Jeshi la Polisi tangu uhuru na ameliongoza kuanzia tarehe 28 Mei 2017 hadi tarehe 20 Julai 2022 na kupata mafanikio makubwa kwenye mapambano dhidi ya uhalifu na Wahalifu ikiwemo kukomesha vitendo vya mauaji yaliyokuwa yakitokea Wilayani Kibiti na maeneo mengine pamoja na kupunguza uhalifu nchini.

Wakuu wa Jeshi la Polisi waliomtangulia ni IGP Mstaafu Elangwa Shaidi ambaye ni IGP wa kwanza tangu uhuru aliyeliongoza Jeshi La Polisi Tanzania kuanzia mwaka 1964 hadi mwaka 1970, IGP mstaafu Hamza Azizi (1970 - 1973), IGP mstaafu Samweli Pundugu (1973 - 1975), IGP Mstaafu Philemon Maya (1975 - 1980), IGP Mstaafu Solomon Liani (1980 - 1984), IGP Mstaafu Harun Mahundi (1984 - 1996) IGP Mstaafu Omari Mahita (1996 - 2006), IGP Mstaafu Saidi Mwema (2006 - 2013) na IGP Mstaafu Ernest Mangu (2013 - 2017).
Screenshot_20230510_051852.jpg
 
Wizara ya Afya imesikitishwa na taarifa iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na mkazi mmoja wa Arusha aliyefahamika kwa jina la Esther Mkombozi aliyeeleza kuwa alichomwa sindano katika duka la dawa na kumsababishia madhara katika mkono wake.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo Jumanne Mei 9, 2023 na wizara hiyo, imekemea kitendo hicho ikisema ni kosa kisheria kwa duka lolote la dawa nchini kutoa huduma za kitabibu ikiwa ni pamoja na kuchoma sindano, kufanya tohara au vipimo vya maabara.

Kutokana na hilo, Wizara imeelekeza Baraza la Famasi (PC) na Bodi ya Hospitali Binafsi (PHAB) kufuatilia suala hilo mara moja na hatua stahiki ziweze kuchukuliwa kwa wote watakaobainika kukiuka sheria, kanuni, miongozo na Taratibu za Usimamizi na Udhibiti wa utoaji wa huduma za Afya nchini.

“Tunampa pole Esther kutokana na madhara aliyopata. Tuwaomba wananchi kuendelea kuwa watulivu ambapo suala hill linafanyiwa kazi.” ilinukuliwa sehemu ya taarifa hiyo.

Screenshot_20230510_052130.jpg
 
Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson amesema kitendo cha Mbunge wa Tarime Vijijini (CCM), Mwita Waitara kuvua koti na tai akiwa ndani ya Bunge,”Hairuhusiwi kufanya hivyo ndani ya Bunge na huo ni utovu wa nidhamu. Kanuni zetu zinaelekeza jinsi ya kuvaa humu bungeni.”

“Huko nyuma imewahi kujitokeza mtu anapiga magoti, anapiga sarakasi sasa hii ya kutoa nguo, hapa hairuhusiwi na isijirudie tena, kama una hasira kazitolee nje.”

Dk Tulia ametoa kauli hiyo usiku wa leo Jumanne, Mei 9, 2023 wakati akihitimisha kikao cha Bunge jijini Dodoma. Alikuwa akizungumzia tukio lililojitokeza asubuhi la Mbunge Waitara kukiuka kanuni za Bunge baada ya kudai swali lake halijajibiwa ipasavyo na kuamua kutoka ukumbini akiwa amekwisha kuvua koti na tai.
Screenshot_20230510_052234.jpg
 
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya maxungumzo na Watanzania wanaoishi nchini Namibia (Diaspora) katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Jijini Windhoek.

Rais Samia alikuwa Namibia kuhudhuria katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Organ Troika, SADC Troika na Nchi zinazochangia Vikosi vya Jeshi katika Force Intervention Brigade (FIB). Mkutano huo utajadili hali ya Usalama Mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Screenshot_20230510_052407.jpg
 
Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara), Tundu Lissu amelishukuru Jeshi la Polisi kwa kulilinda gari lake baada ya shambulio la risasi kutoka kwa watu wasiojulikana.

Lissu (55) alishambuliwa mchana wa Septemba 7, 2017 akiwa ndani ya gari hilo akijiandaa kushuka nyumbani kwake, Area D jijini Dodoma akitoka kuhudhuria vikao vya Bunge.

Akizungumza Dodoma leo Jumanne Mei 9, 2023 baada ya kuliona gari hilo kwa mara ya kwanza amesema alifanya mawasiliano na uongozi wa Polisi mkoa huo pamoja na maafisa wake ndipo walipomruhusu kuliona.

“Hii gari imekuwa chini ya Polisi kwa muda wote huu na mimi binafsi nilikuwa sijawahi kuliona kabisa, nilikuwa nasikia tu kwamba nilipigwa risasi nyingi, leo wameniwezesha nimeona ina matundu 30 ya risasi na imenipa shida sana nashukuru kwa kulilinda gari hii,” amesema.

Hata hivyo, Lissu amelitaka Jeshi la Polisi kuwatafuta waliofanya tukio hilo washughulikiwe kwa mujibu wa sheria.

“Mimi ningependa huyo aliyepiga hizo risasi zote hizo atafutwe na ashughulikiwe kwa mujibu wa sheria,” amesema.

Screenshot_20230510_052500.jpg
 
BAADHI ya wachezaji wa Wigan wenye hasira wamepanga kufanya maandamano na waligoma kucheza mechi yao mwisho ya Ligi daraja la Kwanza dhidi ya Rotherham.

Wachezaji wa kikosi hicho cha Wigan waligoma kufanya mazoezi wikiendi iliyopita ikidaiwa kwamba mmiliki wao ameshindwa kuwapa mishahara yao yote.
Imeelezwa kuna Wachezaji ambao wamechelewa kulipwa mishahara yao, lakini wale ambao mkataba wao inamalizika mwisho wa msimu hawajalipwa mishahara yao.

Ingawa mishahara hiyo imechelewa kuingia kabla ya mechi yao dhidi ya Millers, wachezaji wa Wigan wangegoma kucheza mechi ya mwisho ya msimu huku Ligi daraja la Kwanza.

Mwenyekiti wa Wigan, Talal Al Hammad aliweka wazi mishahara haitawekwa hadi mechi itakapochezwa jambo ambalo limepingwa vikali na wachezaji wao.
Screenshot_20230510_052627.jpg
 
Mo janja janja sana
BAADHI ya wachezaji wa Wigan wenye hasira wamepanga kufanya maandamano na waligoma kucheza mechi yao mwisho ya Ligi daraja la Kwanza dhidi ya Rotherham.

Wachezaji wa kikosi hicho cha Wigan waligoma kufanya mazoezi wikiendi iliyopita ikidaiwa kwamba mmiliki wao ameshindwa kuwapa mishahara yao yote.
Imeelezwa kuna Wachezaji ambao wamechelewa kulipwa mishahara yao, lakini wale ambao mkataba wao inamalizika mwisho wa msimu hawajalipwa mishahara yao.

Ingawa mishahara hiyo imechelewa kuingia kabla ya mechi yao dhidi ya Millers, wachezaji wa Wigan wangegoma kucheza mechi ya mwisho ya msimu huku Ligi daraja la Kwanza.

Mwenyekiti wa Wigan, Talal Al Hammad aliweka wazi mishahara haitawekwa hadi mechi itakapochezwa jambo ambalo limepingwa vikali na wachezaji wao.
View attachment 2616232
 
Mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) kati ya Baobab Queens dhidi ya Simba Queens umemalizika katika uwanja wa Jamhuri jioni ya leo Mei 9, kwa wenyeji kupokea kichapo cha mabao 2-0.

Licha ya Simba Queens kuibuka na ushindi huo inasikilizia michezo ya JKT Queens na Fountain Gate Princess kuweza kujua hatma ya ubingwa.

Baada ya ushindi huo, Simba Queens inaongoza ikiwa na pointi 42 ikifuatiwa na JKT Queens yenye alama 40 na Fountain inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 38.

Simba Queens imecheza michezo 17 huku JKT Queens na Fountain zikiwa zimecheza michezo 16.

Mchezo unaosubiriwa kwa hamu ni kati ya Fountain Gate Princess dhidi ya JKT Queens unaotarajiwa kupigwa keshokutwa (Alhamisi Mei 11) katika uwanja wa Jamhuri.

Screenshot_20230510_052743.jpg
 
Nimependa hapo .... Queens ... Kileleni...
Mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) kati ya Baobab Queens dhidi ya Simba Queens umemalizika katika uwanja wa Jamhuri jioni ya leo Mei 9, kwa wenyeji kupokea kichapo cha mabao 2-0.

Licha ya Simba Queens kuibuka na ushindi huo inasikilizia michezo ya JKT Queens na Fountain Gate Princess kuweza kujua hatma ya ubingwa.

Baada ya ushindi huo, Simba Queens inaongoza ikiwa na pointi 42 ikifuatiwa na JKT Queens yenye alama 40 na Fountain inashika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 38.

Simba Queens imecheza michezo 17 huku JKT Queens na Fountain zikiwa zimecheza michezo 16.

Mchezo unaosubiriwa kwa hamu ni kati ya Fountain Gate Princess dhidi ya JKT Queens unaotarajiwa kupigwa keshokutwa (Alhamisi Mei 11) katika uwanja wa Jamhuri.

View attachment 2616233
 
Kinda wa Real Madrid, Rodrydo amezungumzia kuhusu mechi ya nusu fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City huku akimhofia mshambuliaji wa timu hiyo Erling Haaland.

"Hakuna anayejua jinsi ya kumzuia Haaland, ila nina imani hatofunga dhidi yetu,"
Screenshot_20230510_052855.jpg
 
Kocha mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi amewaita mashabiki kwenye mechi ya kesho nusu fainali Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Marumo Gallants saa 10:00 jioni Uwanja wa Mkapa.

"Niwashukuru sana mashabiki wa Yanga kwa sapoti mliyotupa kutoka mwanzo mpaka leo, nawaomba kesho tuongeze kitu kimoja. Kesho tushangilie kwa dakika zote 90, hata katika nyakati timu haina mpira tusiwe kimya, tupambane kushangilia ili kuwapa nguvu wachezaji wetu. Hii mechi sio nyepesi kama wengi wanavyodhani" amesema Nabi na kuongeza;

"Marumo ni timu nzuri, na sisi tunajiandaa kucheza na timu iliyofika hatua ya nusu fainali"
Screenshot_20230510_053005.jpg
 
Siku kadhaa tangu mashabiki wa PSG kuandamana nyumbani kwa nyota wa soka wa PSG, Neymar Jr, klabu hiyo imesema ipo tayari kumuachia staa huyo wa Brazil endapo watapata ofa nzuri.

Mkataba wa Neymar Jr umebakia miaka minne katika klabu hiyo ila uongozi umesema upo tayari mchezaji huyo aondoke.
Screenshot_20230510_053248.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom