Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230507_065520_Opera%20Mini.jpg
 
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuagiza Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi, kuitisha kikao maalum cha Baraza la Vyama vya Siasa lengo likiwa ni kuwashirikisha Wadau katika kutathmini utekelezaji wa mapendekezo ya Kikosi Kazi kilichokuwa kikiratibu maoni ya watu kuhusu demokrasia ya Vyama vingi vya siasa nchini.

Rais Samia ametoa maelekezo hayo wakati wa kikao kilichofanyika Ikulu ya Chamwino, kilichohudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali kuhusu kuanza kwa mchakato wa Katiba mpya.

Kikao hicho kimejadili namna ya kushirikisha Wadau mbalimbali na hasa ushirikishwaji wa Wananchi katika mchakato huo kutoka pande zote mbili Tanzania Bara na Zanzibar.

Mbali na mchakato huo wa Katiba mpya, masuala mengine yanayotarajiwa kushughulikiwa ni marekebisho ya sheria mbalimbali zinazohusiana na uchaguzi, zikiwemo Sheria ya Tume ya Uchaguzi, Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Msajili wa Vyama vya Siasa.

Miongoni mwa Viongozi waliohudhuria kikao hicho ni pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Jenista Mhagama, Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro na Watendaji wa Taasisi mbalimbali.
Screenshot_20230507_071111.jpg
 
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu @ummymwalimu amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Dkt. Isack Sima aliyekuwa Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Nyangoto, kilichopo Wilaya ya Tarime Vijijini, Mkoa wa Mara ambaye inadaiwa ameuawa tarehe 03 May, 2023 kwa kukatwakatwa na mapanga na Watu wasiojulikana wakati akirejea nyumbani kwake akitokea kazini.

Waziri Ummy amelaani vikali kitendo hicho cha mauaji ya Mwanataaluma ya Udaktari ambacho hakikubaliki katika Jamii ambapo ametoa pole nyingi kwa Ndugu, Jamaa, Marafiki, Watumishi wote wa Sekta ya Afya Tarime, na Wanataaluma Nchini kwa ujumla na Watu wote walioguswa kutokana na mauaji haya.

Ummy amenukuliwa akisema “Tunaamini Vyombo vya Dola vitafanikisha kupatikana kwa Wahusika waliofanya kitendo hiki”
Screenshot_20230507_071339.jpg
 
Wakati ripoti ya matokeo ya sensa ya Tanzania yaliyotangazwa mwaka 2022 yakionesha kuwa Tanzania ina Watu milioni 61 na laki saba, Ripoti mpya iliyotolewa na TCRA imeonesha kuwa hadi March 2023 idadi ya laini za simu zilizoko kwenye matumizi Nchini ni milioni 58.1

Kwenye idadi hiyo Dar es salaam imeongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya laini za simu zinazotumika ‘active simcards) kuliko Mkoa mwingine wowote.

1. DSM - 10,936,342
2. Mwanza 3,958,286
3. Arusha 3,713,004
4. Mbeya 3,591,274
5. Dodoma 3,216,101
Screenshot_20230507_071501.jpg
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo May 06, 2023 akiwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, amepokea taarifa ya Kamati aliyoiunda kuchunguza tukio la kukatika umeme katika uwanja huo wakati wa mechi ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika kati Timu ya Yanga na Rivers United ya Nigeria.

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Waziri Dkt. Chana amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Said Yakubu kufanyia kazi taarifa hiyo ikiwemo kuchukua hatua zinazostahili kulingana na taarifa hiyo.

Tukio hilo la kupokea taarifa limehudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu, Nicholaus Mkapa.

Kamati hiyo imeongozwa na Mwenyekiti Mhandisi Keneth Boymanda kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), ikiwa na Wajumbe kutoka Wakala wa
Majengo (TBA) na baadhi ya Watumishi wa Wizara.
Screenshot_20230507_072242.jpg
 
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezifungia bar za wazi za Rainbow na Chako ni Chako Pub za Jijini Dodoma baada kukuta kelele zilizo kinyume cha sheria ya usimamizi wa mazingira namba 20 ya mwaka 2004 na kanuni ya viwango vya udhibiti wa kelele na mtetemo ya mwaka 2015.

Akiongea leo Dodoma katika oparesheni hiyo Saida Madusi Afisa Mkaguzi wa Mazingira wa NEMC Kanda ya Kati, amesema walifanya ukaguzi huo majira ya saa tisa usiku na kukuta ukiukwaji wa sheria hiyo “Sheria hiyo inasema maeneo ambayo yanazunguka maeneo ya Watu na kuna biashara kelele zinatakiwa kuwa 60 DBA wakati wa mchana na 40 usiku, tumefanya ukaguzi katika maeneo mbalimbali ya biashara yaliyo jirani na makazi ya Watu”

“Tumefika hapa tumekuta kelele zimefika mpaka 68 DBA na zilikuwa zinasikika hadi nje na tumetembela Majirani walikuwa wanalalamika hizo kelele, sasa tumewaagiza Jumatatu wafike Ofisi za NEMC Kanda ya Kati”
Screenshot_20230507_072534.jpg
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo May 06, 2023 akiwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, amepokea taarifa ya Kamati aliyoiunda kuchunguza tukio la kukatika umeme katika uwanja huo wakati wa mechi ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika kati Timu ya Yanga na Rivers United ya Nigeria.

Baada ya kupokea taarifa hiyo, Waziri Dkt. Chana amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Said Yakubu kufanyia kazi taarifa hiyo ikiwemo kuchukua hatua zinazostahili kulingana na taarifa hiyo.

Tukio hilo la kupokea taarifa limehudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu, Nicholaus Mkapa.

Kamati hiyo imeongozwa na Mwenyekiti Mhandisi Keneth Boymanda kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), ikiwa na Wajumbe kutoka Wakala wa
Majengo (TBA) na baadhi ya Watumishi wa Wizara.
View attachment 2612802
Hawa watu wa hovyoo kabisa, wamezoea matume tu kwa ajiri ya upigaji.. mataa yale ya kizamani huitaji hata kuwa elimu kubwa kuona wanakiwa badirisha mifumoo s
 
Halmashauri ya Jiji la Arusha kupitia kwa Kaimu Mkurugenzi wa Jiji hilo Hargney Chikuturo imetoa ufafanuzi baada ya kusambaa kwa picha na video mtandaoni na kusema mgahawa uliovunjwa katika barabara ya Sokoni one ni kutokana na Mfanyabiashara huyo hakuwa na kibali cha ujenzi wa eneo hilo pamoja na eneo hilo kuwa karibu na Benki huku ujenzi wa kituo cha mafuta ukiendelea.

Kaimu Mkurugenzi huyo amesema hawakumuonea bali walivunja kupisha miundombinu ya maji iliyojengwa katika eneo hilo na kusaidia barabara hiyo kupitika pale inapotokea majanga mbalimbali

George Peter ambaye ni Mmiliki wa mgahawa huo amesema amefanya biashara kwa zaidi ya miaka 11 katika eneo hilo na hajawahi kupewa notisi yoyote ya kuhama na kwamba kitendo kilichofanyika ni uonevu ambapo kimemsababishia hasara kubwa.
Screenshot_20230507_072717.jpg
 
Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limezifungia bar za wazi za Rainbow na Chako ni Chako Pub za Jijini Dodoma baada kukuta kelele zilizo kinyume cha sheria ya usimamizi wa mazingira namba 20 ya mwaka 2004 na kanuni ya viwango vya udhibiti wa kelele na mtetemo ya mwaka 2015.

Akiongea leo Dodoma katika oparesheni hiyo Saida Madusi Afisa Mkaguzi wa Mazingira wa NEMC Kanda ya Kati, amesema walifanya ukaguzi huo majira ya saa tisa usiku na kukuta ukiukwaji wa sheria hiyo “Sheria hiyo inasema maeneo ambayo yanazunguka maeneo ya Watu na kuna biashara kelele zinatakiwa kuwa 60 DBA wakati wa mchana na 40 usiku, tumefanya ukaguzi katika maeneo mbalimbali ya biashara yaliyo jirani na makazi ya Watu”

“Tumefika hapa tumekuta kelele zimefika mpaka 68 DBA na zilikuwa zinasikika hadi nje na tumetembela Majirani walikuwa wanalalamika hizo kelele, sasa tumewaagiza Jumatatu wafike Ofisi za NEMC Kanda ya Kati”
View attachment 2612803
Dah! Chako ni chako kuna makuku matamu
 
Siku chache baada ya Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro kutangaza kuanza mchakato wa Katiba Mpya uliokwama, Rais Samia Suluhu Hassan amemuagiza Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kuitisha kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa.

Lengo la kuitishwa kwa Baraza hilo linaloshirikisha vyama vyote vya siasa vyenye usajili wa kudumu kutathimini utekelezaji wa mapendekezo ya kikosi kazi kilichokuwa kikiratibu maoni ya watu mbalimbali kuhusu demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Kikosi kazi hicho kilichokuwa kikiongozwa na Mwenyekiti, Profesa Rwekaza Mukandala pamoja na mambo mengine, kilipendekeza mchakato wa Katiba uliokwama mwaka 2014 kwa hatua ya Katiba Pendekezwa kufufuliwa.

Rais Samia ametoa maagizo hayo leo Jumamosi Machi 6, 2023, Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma alipofanya kikao na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Jaji Mutungi na Waziri Ndumbaro.
Screenshot_20230507_073233.jpg
 
Mkazi wa kijiji cha Kibitilwa kata ya Ilula wilayani Kwimba mkoani Mwanza, Marko Samwel (32) amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando baada ya kujikata na kuziondoa sehemu zake za siri kwa kutumia kisu.

Samwel anadaiwa kujifanyia kitendo hicho cha kikatili Mei 3 mwaka huu Saa 7 usiku baada ya kwa madai kuwa amechoka kuuguza maradhi yanayomsumbua (yamehifadhiwa) kwa zaidi ya miaka mitano.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza amesema hayo leo Mei 6, 2023 alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza.

Screenshot_20230507_073345.jpg
 
Wakati ripoti ya matokeo ya sensa ya Tanzania yaliyotangazwa mwaka 2022 yakionesha kuwa Tanzania ina Watu milioni 61 na laki saba, Ripoti mpya iliyotolewa na TCRA imeonesha kuwa hadi March 2023 idadi ya laini za simu zilizoko kwenye matumizi Nchini ni milioni 58.1

Kwenye idadi hiyo Dar es salaam imeongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya laini za simu zinazotumika ‘active simcards) kuliko Mkoa mwingine wowote.

1. DSM - 10,936,342
2. Mwanza 3,958,286
3. Arusha 3,713,004
4. Mbeya 3,591,274
5. Dodoma 3,216,101
View attachment 2612790
Hapo kuna watu Wana line Hadi kumii.. duh!

Najipa hongera kwa kuwa na line moja toka nimeumbwa duniani
 
Siku chache baada ya Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Damas Ndumbaro kutangaza kuanza mchakato wa Katiba Mpya uliokwama, Rais Samia Suluhu Hassan amemuagiza Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi kuitisha kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa.

Lengo la kuitishwa kwa Baraza hilo linaloshirikisha vyama vyote vya siasa vyenye usajili wa kudumu kutathimini utekelezaji wa mapendekezo ya kikosi kazi kilichokuwa kikiratibu maoni ya watu mbalimbali kuhusu demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Kikosi kazi hicho kilichokuwa kikiongozwa na Mwenyekiti, Profesa Rwekaza Mukandala pamoja na mambo mengine, kilipendekeza mchakato wa Katiba uliokwama mwaka 2014 kwa hatua ya Katiba Pendekezwa kufufuliwa.

Rais Samia ametoa maagizo hayo leo Jumamosi Machi 6, 2023, Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma alipofanya kikao na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Jaji Mutungi na Waziri Ndumbaro.

Screenshot_20230507_073751.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom