Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mkazi wa Dar es salaam, Gaston Massawe amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa shitaka la kusambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa Tiktok zilizosema “ukiagiza gari nje ya nchi, watumishi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) wanang’oa vifaa.”

Mshitakiwa amekiri kufanya kitendo hicho akidai video ilikuwa ya bandari nyingine na kwamba alifanya hivyo ili kuwapa taarifa polisi juu ya mambo hayo yanayofanyika.
Screenshot_20230503_140909.jpg
 
Serikali ya Urusi imeishutumu Ukraine kwa kujaribu kufanya mashambulizi kwa kutumia ndege zisizo na rubani (drones) kwenye Ikulu ya Kremlin Nchini Urusi kwa lengo la kumuua Rais Vladimir Putin, hizi zikiwa ni shutuma kubwa zaidi ambazo Urusi imetoa dhidi ya Ukraine tangu vita dhidi yake ianze.

Ikulu ya Urusi ijulikanayo kama Kremlin imesema inachukulia shambulio hilo kama hatua ya kigaidi iliyopangwa na italipiza kisasi wakati wowote na popote inapoona inafaa, Sky News na Aljazeera wameripoti.

Urusi inadai kuwa Ukraine ilirusha ndege mbili zisizo na rubani kuelekea Ikulu ya Urusi jana usiku katika kile inachodai kuwa ni jaribio la kumuua Rais Vladimir Putin, Rais wa Urusi hakuwepo katika jengo hilo wakati huo, Msemaji wa Serikali ya Urusi Dmitry Peskov amesema.

Afisa Mkuu wa Rais wa Ukraine Mykhailo Podolyak amesema Ukraine haina uhusiano wowote na tukio hilo linalodaiwa kutokea.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy kwa sasa yuko Nchini Finland na anapanga kusafiri hadi Ujerumani kwa dhumuni la kuomba msaada zaidi wa kijeshi kutoka kwa Washirika wa Magharibi.
Screenshot_20230504_050848.jpg
 
Serikali kupitia kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imepanga kutoa jumla ya mitungi 100,000 bure ifikapo July,2023 katika maeneo ya Vijijini Nchi nzima ikiwa ni hatua ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi.

Mpango huo umekuja mara baada ya Serikali kutenga Tsh. Bilioni 3.2 kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwaajili ya usambazaji wa gesi safi ya kupikia.

Akiongea Dar es salaam Mkurugenzi wa Uenezaji Masoko na Teknolojia Kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage alipokutana na Wadau wa gesi nchini, amesema wameshaanza kuweka fomu ya maoni tangu Aprili 19 na kukamilishwa May 10,2023 ili kupata Watu watakaonufaika na gesi hizo.

Amesema nishati safi ni ile ambayo haichafui mazingira, inalinda afya ya Mwananchi lakini pia inatoa fursa kuwa kazi ya kupika ni starehe na isiwe shida hadi kufikia Mtu anapika huku anatoa machozi.

Mwaijage amesema Serikali ina mipango mingi kuhakikisha Wananchi wote wanafikiwa na nishati hiyo na licha ya kufikiwa wakiihitaji wapate kwa wakati.
Screenshot_20230504_051140.jpg
 
"Kuna mifumo ya kiutendaji Serikalini ambayo inawakandamiza wafanyakazi mfano ni kutokuangalia tija ya mfanyakazi husika na mchango wake kwenye jamii ikilinganishwa na mishahara wanayopewa. Hapa kuna walimu, madaktari, manesi, maofisa ugani wanafanya kazi kubwa lakini malipo yao ni duni ikilinganishwa na wanaofanya kazi kwenye mashirika.

Changamoto nyingine ni makato makubwa ya kodi, inawezekana kabisa mshahara ukaongezwa lakini makato yakamuacha mfanyakazi akiwa katika hali ile ile." Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Faraja Kristomus wakati akichangia katika mjadala wa Mwananchi Twitter Space.
Screenshot_20230504_051257.jpg
 
"Tutaendele kutoa ushirikiano kwa Serikali na wadau wake katika kutekeleza mipango kazi yenye staha na kuimarisha haki za msingi.

Tuko tayari kuendelea kutoa elimu kwa Serikali na wanachama mbalimbali tuna milango yetu iko wazi karibuni tuone ni kwa namna gani tuendelee kufanya kazi pamoja.

" Mwakilishi wa ILO, Nasikiwa Berwa wakati akichangia mjadala wa Twitter Space ulioandaliwa na Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd.

Screenshot_20230504_051414.jpg
 
"Si kwamba tumeiacha sekta binafsi, tunaomba iundwe bodi ya kima cha chini cha mishahara ili ifanye tafiti na kujiridhisha kiwango kitakachopangwa kitaendana na uhalisia wa maisha."

Katibu Mkuu Tucta Henry Mkunda wakati akizungumza wakati wa mjadala wa Twitter Space kuhusu maoni ya hotuba ya Rais na maslahi ya wafanyakazi nchini.

Screenshot_20230504_051528.jpg
 
“Nyongeza ya mshahara kila mwaka hili lipo kisheria lakini Rais aliyepita akaamua kuondoa, sasa tumepewa ahadi kuwa itarudi, hatuelewi nyongeza hiyo itahusisha na ile miaka iliyopita maana athari yake inaonekana pia kwenye pensheni.

Suala la posho ya kufundishia ni jambo la msingi, wote tunajua walimu ndio chanzo cha kila kitu na maendeleo ya taifa lolote lile. Itawapa morali walimu wafanye kazi yao vizuri.

Suala la nyongeza ya mshahara ni muhimu liendane na hali ya maisha,” amesema Spika wa Bunge la Wananchi Chadema, Susan Lyimo wakati akichangia mjadala ulioandaliwa na Mwananchi Communications Limited kuhusu hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu maslahi ya wafanyakazi nchini.

Screenshot_20230504_051658.jpg
 
“Walimu wa Tanzania tumeguswa kwa kiasi kikubwa na hotuba ya Rais hasa alipogusia maslahi ya walimu.
Suala la posho ya kufundishia, tumelipigia kelele kwa muda mrefu na Rais ameliona hili ameahidi anakwenda kulifanyia kazi hii itatufanya tuwe na ari kubwa ya kufundisha.

Kuna mengi yamefanyika katika sekta ya elimu ikiwemo kuboresha miundombinu, kwa sasa tunashuhudia mazingira mazuri ya shule. Tumepewa vishkwambi ambavyo vinatusaidia katika utendaji kazi wetu wa kila siku, ahadi yetu ni kufanya kazi kwa bidii.” Rais wa Chama cha Walimu Tanzania(CWT), Leah Ulaya.
Screenshot_20230504_051805.jpg
 
"Panapokuwa na maboresho ya maslahi hata ari ya kufanya kazi inaongezeka, bahati mbaya suala la nyongeza ya mshahara linaonekana kugusa zaidi sekta ya umma ingawa kwa uhalisia ilipaswa kugusa hata sekta binafsi kwa kuwa gharama za maisha ni zile zile.

Suala la kuboresha maslahi kwa wafanyakazi ni jambo ambalo halitakiwi kusubiri utashi wa kiongozi bali kuangalia uhalisia wa hali ya maisha." Kaimu Mhariri wa Jarida la Uchumi Gazeti la Mwananchi Ephrahim Bahemu

Screenshot_20230504_052036.jpg
 
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza aliyekuwa akishikiliwa katika kituo cha polisi cha Khwisero kilichopo Kaunti ya Kakamega nchini Kenya anadaiwa kubakwa na mmoja wa ofisa wa polisi wa kituo hicho.

Kwa mujibu wa tovuti ya Tuko ya nchini humo imesema mwanafunzi huyo alikamatwa Aprili 28, mwaka huu akiwa na rafiki yake kwa kosa la kwenda kwa mtu anayesemekana ni mpenzi wake, hivyo wazazi wao wakawaomba polisi kuwakamata na kuwasweka mahabusu kama adhabu.

Wakiwa kituoni hapo askari alikwenda na kumtaka mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16, kumfuata kwenye chumba kingine ambapo alimuamuru avue nguo.

Mkurugenzi wa Huduma za Kijamii, Huduma za Watoto, Utamaduni na Jinsia wa kaunti hiyo, Vivian Ayuma amesema kuwa mtuhumiwa alimnajisi mtoto huyo kwa kutumia kinga (kondomu) ingawa bado hajakamatwa.

Screenshot_20230504_052212.jpg
 
Polisi mkoani Songwe limemkamata, Aloyce Nyabwanzo (53), Mkazi wa Kitongoji cha Kikamba, Kijiji cha Kapalala wilayani, Songwe kwa tuhuma za kuwaua wajukuu zake wawili kwa kuwapasua mafuvu ya kichwa na mchi wa kutwangia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Theopista Mallya amesema tukio hilo lilitokea Aprili 30, 2023 majira ya saa 5:00 alfajiri na kwamba jeshi hilo linaendelea na uchunguzi ili kujua sababu za mtuhumiwa huyo kutenda tukio hilo.

Amesema mtuhumiwa aliwashambulia wajukuu zake wakati wanatoka chumbani wakimfuata bibi yao sebleni aliyekuwa anajaribu kuzuia vurugu hizo zilizoanzishwa na babu nyakati hizo za usiku.

Marehemu wamefanyiwa uchunguzi na daktari na kubaini kuwa vifo vyao vimesababishwa na kupasuka kwa mafuvu ya vichwa baada ya kupigwa na kitu kizito hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi na ubongo kutoka nje,” amesema Kamanda Mallya.

Amewataja marehemu hao kuwa ni Jackson Chacha (2) na George Chacha (5) wote wakazi wa kitongoji cha Iwindu- Kikamba katika Kijiji cha Kapalala na walikuwa wakilelewa na mtuhumiwa.

Hata hivyo, Kamanda Mallya amesema wakati uchunguzi wa kujua sababu zilizosababisha mtuhumiwa kutenda tukio hilo, watapelekwa hospitali ili kupimwa afya ya akili.
Screenshot_20230504_052442.jpg
 
CITY KAREJEA KILELENI
.
50’—️ Ake
70’—️ Haaland
85’—️ Foden
.
FT: MAN CITY 3-0 WEST HAM
.
Mbio za Ubingwa EPL
1. Man City — (33)— 79pts
2. Arsenal — (34) — 78pt
Screenshot_20230504_052829.jpg
 
POCHETTINO KUMVUTA MANE CHELSEA
.
Kocha mtarajiwa huko Chelsea, Mauricio Pochettino ameripotiwa kupitisha mpango wa usajili wa mshambuliaji wa Bayern Munich, Sadio Mane ili atue kukipiga Stamford Bridge katika dirisha lijalo la usajili.
.
Mane, 31, amekuwa akikabiliwa na wakati mgumu huko Bayern. Hivi karibuni aliripotiwa kumpiga ngumi Leroy Sane, Jambo hilo linadaiwa kumtibulia sifa yake Mane miongoni mwa mabosi wa Bayern pamoja na mashabiki wa timu hiyo na hilo linaelezwa linaweza kumsukumia Msenegali huyo kwenye mlango wa kutokea.
.
Kwa mujibu wa Sky sports, Mauricio Pochettino amewapa ruhusu waajiri wake wapya watarajiwa, Chelsea kwenda kukamilisha usajili wa Mane, huku kocha huyo wa zamani wa Tottenham akidai anamkubali sana mchezaji huyo.
Screenshot_20230504_053001.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom