Makapuku Forum

Makapuku Forum

.
JUST IN: Baada ya Kariakoo Derby, mechi ya Namungo dhidi ya Simba na Singida Big Stars dhidi ya Yanga kwenye NBC Premier League ambapo zilitarajiwa kupigwa wiki hii zimeahirishwa ili kuwapa muda wa kujiandaa Simba na Yanga kwenye mechi za robo fainali kimataifa.
Screenshot_20230418_071125.jpg
 
NANI ATAVUNJA REKODI YA KIBADENI
.
Simba imemaliza ubishi kwa kushinda pambano la 110 la Ligi Kuu tangu kuasisiwa kwa ligi hiyo mwaka 1965, lakini bado rekodi ya Hat trick ya Abdallah Kibadeni 'King' ikishindwa kuvunjwa kwenye mechi za watani wa jadi.
.
Kibadeni alifunga hat trick kwenye pambano lililopigwa Julai 19, 1977 wakati Simba ikiifumua Yanga kwa mabao 6-0 (Sita yai ) na imeshindwa kuvunjwa wala kufikiwa kwa muda unaokaribia miaka 46 licha ya Simba na Yanga kuwa na mastraika walioweka heshima kubwa kwa kutupia mipira kambani.
.
Katika mechi hiyo iliyokuwa ya 11 iliyopigwa Jumanne, Kibadeni alifunga mabao yake dakika za 10, 42 na 89, huku Jumanne Hassan 'Masimenti' akifunga mengine mawili katika dakika za 60 na 73, huku beki wa Yanga, Selemani Sanga akijifunga dakika ya 20.
Screenshot_20230418_070709.jpg
 
“Baleke licha ya kutokufunga kwenye derby lakini aliifanya mechi iwe ngumu kwa Yanga. Aliwanyima uhuru wachezaji wa Yanga wa eneo la ulinzi kwa sababu Yanga huanzia mashambulizi kutoka kwa Diarra ambaye anapiga pasi kwa mabeki wake lakini jana Jean Baleke alikuwa busy kwenye eneo hilo na hakuruhusu Yanga wacheze.”

“Jana kama mara mbili Yanga walipoteza mipira wakati wanaanza kutokea golini kwao na mara zote ilisababishwa na pressing za Baleke. Kwa hiyo Yanga hawakuwa huru tena kuanzisha mashambulizi yao kutokea golini.”

“Goli la pili la Simba lilitokana na Simba kukabia juu, wakanyang’anya mpira, Kibu akawa na nafasi ndefu ya kutembea na mpira na uhuru wa kufanya maamuzi.”

- Master Tindwa
Screenshot_20230418_071403.jpg
 
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Hamad Hassan Chande amemuagiza Kamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuhakikisha Wajasiriamali wapya hawatozwi kodi kabla ya kuanza kufanya biashara.

Chande ametoa agizo hilo Bungeni Jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Ng'wasi Damas Kamani, alipotaka kujua ni lini Serikali itaona haja ya kuondoa malipo ya kodi kwa Wajasiriamali kabla ya kuanza rasmi kufanya biashara.

Chande amesema kuwa Serikali kupitia Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2019, Kifungu cha 43 imetoa unafuu wa kutolipa kodi kwa kipindi cha miezi sita kwa biashara mpya tangu muhusika anapopewa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi, lengo likiwa kumpa Mjasiriamali nafasi ya kustawi kibiashara.
Screenshot_20230418_163336.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametengua uteuzi wa Sekiete Yahaya Selemani, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuanzia April 16,2023.
Screenshot_20230418_163506.jpg
 
Nchi za Ufaransa, Italia na Marekani zimekuwa vinara wa kuleta wageni wengi wa kimataifa nchini katika kipindi cha Januari hadi Februari 2022 kutoka nje ya Afrika.

Huku kwa nchi za ndani ya Afrika, Kenya na Burundi zikiongoza. Hata hivyo katika kipindi hicho watalii wa kimataifa wameongezeka kwa asilimia 49 mwaka huu ikilinganishwa na mwaka 2022.

“Wageni wa kimataifa wamefika 290,896 mwaka huu katika kipindi cha Januari na Februari kutoka wageni 195,483 mwaka 2022 katika kipindi kama hicho.” Imesema ripoti ya NBS.

Katika ripoti iliyotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inaonyesha kwa nchi Ufaransa iliongoza kuleta watalii 25,837 ikifuatiwa na Italia iliyoleta watalii 18,556 na Marekani walikuwa 16,567.

Nchi nyingine ni Ujerumani (15,705), Poland (12,369) na Uingereza (10,657). Kwa upande wa nchi za Afrika, Kenya inaongoza kwa kuleta watalii 29,615 ikifuatiwa na Burundi (16,832), Rwanda (7,627) na Malawi (6,563).

Nchi nyingine ni Uganda (6,511) na Afrika Kusini ilileta watalii 5,196.

Screenshot_20230418_163648.jpg
 
Kesi ya waliokuwa wanachama wa Chadema iliyofunguliwa na Halima Mdee na wenzake 18 wanaopinga kuvuliwa uanachama wa chama hicho, imeshindwa kuendelea leo katika Mahakama Kuu, Masjala Kuu ya Dar es Salaam.

Sababu ya kuahirishwa kwa kesi hiyo ni Jaji anayesikiliza shauri hilo, Cyprian Mkeha kuwa na majukumu mengine nje ya ofisi.

Mdee ambaye aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) na wenzake walifungua shauri hilo Mahakama Kuu Masjala Kuu ya Dar es Salaam, wakipinga kufukuzwa uanachama kwa utaratibu wa Mapitio ya Mahakama (Judicial Review).

Screenshot_20230418_163752.jpg
 
Kijana mmoja nchini Marekani, Ralph Yarl (16) amepigwa risasi mbili na raia mmoja baada ya kugonga kengele ya mlangoni kwake kimakosa hali iliyozua taharuki na kusababisha maandamano katika Jiji la Kansas, Missouri nchini humo.

Kwa mujibu wa baba wa kijana huyo, Paul Yarl amesema kuwa mwanawe alitumwa na wazazi wake kwenda kuwachukua ndugu zake kutoka katika nyumba ya rafiki yao lakini akakosea na kwenda kubisha hodi kwenye nyumba ambayo sio sahihi na ndipo alipopigwa risasi na mwenye nyumba.

Amesema mwanawe ameruhusiwa kutoka hospitalini na anaendelea kupata matibabu akiwa nyumbani.

Polisi imemwachia huru mtu aliyefyatua risasi huku mawakili wa haki za kiraia, Ben Crump na Lee Merritt wanaowakilisha familia ya Yarl katika kesi hiyo wakikosoa maamuzi hayo.
Screenshot_20230418_163850.jpg
 
Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Sudan, Aidan O'Hara, ameshambuliwa nyumbani kwake mjini Khartoum nchini Sudan ambako kumekuwa na mapigano makali kati ya vikosi vya kijeshi na waasi.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ireland, Micheal Martin amethibitisha Mwanadiplomasia huyo kutoka Ireland hakujeruhiwa sana.

Martin alielezea shambulio hilo kama "ukiukaji mkubwa wa majukumu ya kuwalinda wanadiplomasia".

Takriban watu 185 wameuawa na zaidi ya 1,800 wamejeruhiwa katika siku tatu za mapigano, kwa mujibu wa UN.

Screenshot_20230418_163945.jpg
 
Takriban watu 200 wameuawa na zaidi ya 1,800 wamejeruhiwa katika siku tatu za mapigano kati ya vikosi vya kijeshi na vikosi binafsi nchini Sudan.

Mapigano hayo yalizuka Jumamosi kati ya vikosi vya majenerali wawili walionyakua mamlaka katika mapinduzi ya 2021: Mkuu wa jeshi la Sudan Abdel Fattah al-Burhan na naibu wake, Mohamed Hamdan Daglo, ambaye anaongoza Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF).

Wachambuzi wanasema mapigano katika mji mkuu wa nchi hiyo ambayo ina machafuko kwa muda mrefu hayajawahi kushuhudiwa na yanaweza kurefushwa, licha ya wito wa kimataifa wa kusitisha mapigano huku wanadiplomasia wakihamasishana.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken alisema alikuwa amezungumza na majenerali hao wawili na "kusisitiza haja ya dharura ya kusitishwa kwa mapigano".
Screenshot_20230418_164050.jpg
 
SIMBA, WYDAD KUPIGWA SAA 10
.
Uongozi wa klabu ya Simba, umethibitisha kuwa mchezo wao wa hatua Ya Robo Fainali dhidi ya Wydad Casablanca utapigwa Jumamosi saa 10:00 jioni na hali ya hewa itakuwa rafiki kwa vijana wao kupambana kupata matokeo.
.
Simba inakuwa nyumbani katika mchezo huo wa Klabu Bingwa unaotarajiwa kupigwa Jumamosi kuanzia saa 1o jioni kwa saa badala ya ya ratiba ya awali iliyokuwa saa 1 usiku.
.
Simba inashuka dimbani kuwakabili miamba hao, ikiwa na morali ya kutoka kumkanda mtani wake, Yanga SC.
Screenshot_20230418_164335.jpg
 
.
“Kwa Aziz KI kutokuanza yalikuwa masuala ya kiufundi tu, huyu ni mchezaji mzuri lakini niliona kuwa haikuwa mechi muhimu sana kuanza, huko mbele bado tuna michezo mingine mingi,”

- Kocha Nasreddine Nabi.
Screenshot_20230418_164447.jpg
 
VAR KUTUMIKA JUMAMOSI KWA MKAPA
.
Kesho Alhamisi wataalamu wa teknolojia ya Video Assistants Referee (VAR) kutoka Misri wanatinga nchini tayari kwa kufunga mitambo yao na kuijaribu kwa ajili ya mechi ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayozikutanisha Simba na Wydad Casablanca ya Morocco, Jumamosi hii.
.
Hii itakuwa ni kwa mara ya pili katika Historia kwa VAR kutumika Tanzania katika Uwanja wa Benjamin Mkapa na mara zote ni Simba SC pekee wametumia VAR.
Screenshot_20230418_164558.jpg
 
CAF YAIGOMEA RIVERS UNITED
.
Mpango wa Rivers United ya Nigeria kutaka kuwapeleka mabingwa wa Tanzania, Yanga kwenye Uwanja wa Adokiye Amiesimaka, Port Harcourt umegonga mwamba na badala yake mchezo huo wa mkondo wa kwanza wa robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika utapigwa Godswill Akpabio, Uyo.
.
Rivers walikuwa wakitarajia kupata kibali kutoka CAF, kurejea katika uwanja wao wa nyumbani, wa Adokiye Amiesimaka, Port Harcourt baada ya ukarabati mkubwa kukamilika. Lakini maombi hayo yametupiliwa mbali na Caf na badala yake wataendelea kucheza michezo yao ya nyumbani kwenye Uwanja wa Godswill Akpabio.
.
Baada ya ukaguzi wa awali uliofanyika kwenye Uwanja wa Adokiye Amiesimaka, inatarajiwa kuwa CAF itatuma kikosi kingine ili kuthibitisha matokeo hayo lakini inaonekana hakutakuwa na muda wa kutosha kufanya hivyo kabla ya mchezo wa robo fainali dhidi ya Yanga.
Screenshot_20230418_164808.jpg
 
MATAJI MATATU
.
Nyota wa Manchester City, Rodri, ameionya timu yake kwamba wana uwezo wa kubeba makombe matatu msimu huu lakini wanatakiwa kuwa makini dhidi ya wapinzani wao.
.
Kocha wa timu hiyo Pep Guardiola naye anaamini Man City itabeba makombe makubwa matatu msimu huu nayo ni Ligi Kuu, Ligi Mabingwa Ulaya, na FA. Katika mechi za hivi karibuni Man City imekuwa moto wa kuotea mbali huku Arsenal ikianza kukata pumzi.

Screenshot_20230418_165018.jpg
 
ANTONY KAMA ROBBEN TU
.
Kocha Erik ten Hag amemfananisha Antony na nyota wa zamani wa Chelsea na Bayern Munich, Arjen Robben baada ya kufuta ukame mabao kwenye mechi 15 alizocheza.
.
Winga huyo huyo aliyesajiliwa kwa ada ya Pauni 85.5 milioni anajulikana kwa aina ya uchezaji wake kutokea pembeni na amekuwa mgumu kutabirika kila mara anapotumia mguu wake wa kushoto.
.
Kocha huyo Mholanzi akasema: “Mwanzo tulijua ana uwezo wa kutumia mguu wake wa kulia lakini anatakiwa kuongeza ujuzi zaidi, kitu kingine ni mzuri zaidi anapocheza kwa kuingia ndani zaidi kwenye eneo la hatari, nimemfuatilia sana na uchezaji wake unafanana na Ajern Robben, walikuwa wanasemaga ni mjanja sana, alichofanya Antony kwenye mechi ni hatari sana na hakuna wa kumzuia, bila shaka kama ukicheza kwa kutumia miguu yote hakika hakuna atakayekuzuia, alisema Ten Hag.
Screenshot_20230418_165153.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom