Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kumekuchaaa tuamke na magazeti ya leo Jumanne April 18, 2023
Screenshot_20230418_065117_Opera%20Mini.jpg
 
Farhan Jr

ALLY SALIM JUMA, THE PRIDE OF TANGA muiteni nae ataitika na mtumeni naye atawatumikia! Haikuwa tu suala la mpira wa miguu lakini suala la kuiweka mitaa yake kwenye ramani, Mkubwa Roma yupo Marekani, Odo Ummy yupo Bungeni na Salim yupo uwanjani.

Well the Admn alijua tangu Jumatatu kuwa Ally Salim ataanza langoni, alipoitwa langoni kwa derby akaitika na signature perfomance! Kipa wa Mali karuhusu mali mara mbili, mbele ya Mtanzania kutoka Tanga na cleansheet.

Wahadhiri walisema Football is the game of passing the torch, ila Ally ameweka mkono kwenye tochi! Ameomba ubao na kuandika No Aishi, No Beno trust me there is no problem! Hakuna Matata amini hivyo.

Wakati @baraka_mpenja wa Umalila anasema Get ready to rumble kama Michael Buffer, wakati Bookmakers wanaamini kuna GG, basi mikono miwili ya Bwamdogo inasema your story is not my story, namaliza hii tukutane kwa Carry Mastory.

Usitumie picha hizi hovyo bila idhini ya TCRA maana ni hatari kupaa hivyo kwa watoto chini ya miaka 18, up to the stars bila kutumia darubini pale Serengeti, juu zaidi kuliko mitambo ya Mamlaka ya hali ya hewa, Ally is officially a certified Goalie.

Dont try this at home, hairuhisiwi kwa wenye umri chini ya miaka 18
Screenshot_20230418_070358.jpg
 
Farhan Jr

MOHAMED HUSSEIN, tatizo kubwa amezaliwa Tanzania kisha ana ndui bega la kulia! Amecheza sana Magomeni na amefundishwa na Herry Mzozo.

Tatizo lingine ana passport ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, halafu hana jina la Kizungu flani au Ufaransa ndanimo bali ZIMBWE la Kibantu, kisha kazima sana kabumbu humu mtaani kwahiyo tunaleta kumjua sana.

Likizo zake sio lazima afike Terminal 3 pale kwa Babu yetu Julius wa Kambarage ama Mzanaki wa Butiama ili acheck in abusu anga, bali kilometa chache tu kutoka kambi ya Simba huko Mbweni mpaka nyumbani kwake, hilo ni tatizo.

Mbaya zaidi hata jina lake MOHAMED ndio hao wakina MUDI ana MDI, wakienda mbali sana utasikia MO! Wapo MO Tajiri, wapo MUDI Mkandaji, MUDI Mapikipiki na wengine kisha kuna yeye MO wa mpira, watu wanaona poa tu.

Ila huyu angetokea nje ya Tanzania, halafu jina kidogo la lugha za kimataifa basi stori ingekuwa tofauti sana! CAPTAIN wa mpira anaishi nao sana tu, ndui begani, passport ya Jamhuri ya Muungano, roho ya Simba na damu inachemka mitaa ya Magomeni na Mburahati alipoanza kabumbu.

CAPTAIN TSHABA dropped a street will never forget perfomance! Certified Premier League Hall of Fame nominee @official_mohamedhussein15 @carlos_mastermind

Screenshot_20230418_070515.jpg
 
Farhan Jr

KIBU DENIS ACHAFUA HALI YA HEWA, habari nzima kwenye App! Weka bando lolote na ambaye hana mpatie hotspot! Ni stori ya Mkimbizi iliyobadilika kuwa simulizi kama Shabaan Robert.

Your pain, yet more my pain! Kutoka kambi ya Wakimbizi mpaka kambi ya Simba Sports, wape hii headline Wahariri kuhusu KDP, kidole mdomoni kwa ajili ya Haters wote, Kibu this Kibu that!

Aliitwa Djigui Diarra Mdaka Mishale, akaitwa Kibu mtoa roho! Aliitwa Diarra Screen protector! Akaitwa Kibu the Projector, Cleansheet? No he was the Beast.

The Kibu tumepigwa phrases! Ila Rastaman alimwachia Jah, nobody can stop Kibu! Kwenye derby ngumu mbele ya ukuta mgumu, eneo gumu na maamuzi magumu ndio namna Mchezaji mkubwa anakuamulia mechi kubwa.

Kipigo cha kwanza baada ya Massih kufufuka, zawadi ya kwanza ya maana baada ya Massih kufufuka na Eid ya mpira kabla ya Eid ya mfungo! Utulivu na amani, raha mustarehe kama Fanani na Hadhira, this is football hakuna hasira.

Ziache shangwe zao ziwe zaidi ya kelele zao juu ya KDP, kama Kigoma na Saratoga, kama Mbeya na Sauli, kama Tanzania na Kilimanjaro, kama Mnyama na mechi kubwa

Screenshot_20230418_070709.jpg
 
BUKAYO SAKA AOMBA RADHI
.
Nyota wa Arsenal, Bukayo Saka amewaomba radhi mashabiki baada kukosa penalti muhimu katika sare ya mabao 2-2, dhidi ya West Ham.
.
Baada ya mchezo kumalizika Saka akawaomba radhi mashabiki wa Arsenal kupitia akaunti yake ya Twitter kutokana na makosa yake.
.
“Kutokana na kilichotokea, siku zote nabeba majukumu, haijalishi nini kitatokea, nawaomba radhi mashabiki wa Arsenal, nitafanya juu chini kuweka mambo sawa,” aliandika Saka.
.
Huo ulikuwa mchezo wa pili mfululizo ambao washika bunduki wanadondosha pointi na kupunguza pengo la pointi kufikia nne dhidi ya vijana hao wa Pep Guardiola wakiwa na mchezo mkononi.

…………………
Screenshot_20230418_070838.jpg
 
Ni mzuri, mchezaji mwenye uzoefu. Watu wanasema tuna kikosi kikubwa sana, lakini hatuna wachezaji wengi wa kuziba nafasi na kikosi cha Ligi ya Mabingwa Ulaya ni tofauti na Ligi Kuu England. Ni pigo kubwa kwake na kwetu, lakini ni nafasi ya kupambana na kusonga mbele bila ya huduma yake, tunaamini atarejea haraka.” Kocha wa Chelsea, Frank Lampard akimzungumzia beki wake, Kalidou Koulibaly ambaye atakosekana kwenye mchezo wa marudiano wa Uefa dhidi ya Real Madrid.
Screenshot_20230418_071008.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom