Makapuku Forum

Makapuku Forum

Miss you zaidi Auntie wangu...
Nimerudi sasa...

Naona Notifications kwa App hakuna tena..
Mh mbona me napata pata auntie bora umerudi tena leo nilitaka nije WhatsApp tar 30 jiandae tukae hata nusu saa nina ratiba ya kulala mjini

Saa kumi nina kikao mikocheni nikitoka uko ndio nataka tuonane kama una mda lakini halafu nitaelekea magomeni kwenye birthday party ya dada yangu mmoja
 
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango akiwa ziarani Mwanza amesema hataki kusikia tena Barabara zikifungwa kwa masaa mengi ili apite, huku akiseka dakika 10 zinatosha ili Wananchi waendelee na shughuli zao.

Dr. Mpango amewaomba pia Wananchi kwa usumbufu walioupata baada ya jana Barabara kufungwa kwa saa nne ili yeye apite “Nilishamwambia IGP na nirudie kuwaambia Makamanda wa Polisi wa Mikoa, mambo ya kufunga Barabara kwa masaa mengi kisa tu Mtoto wa masikini Philip Mpango anapita hapana”

“Jana naambiwa mmefunga Barabara mpaka masaa manne haiwezekani, kwanini?, sitaki kusikia tena hili linajirudia, muambizane na wanaopokea msafara huko tutakakopita”

“Acheni Wananchi wapite kwani dakika 10 hazitoshi), masaa manne kweli!?, nawaomba radhi ya dhati kabisa Wananchi”
Screenshot_20230413_185020.jpg
 
Polisi mkoani Njombe wamemkamata Mfanyabiashara (jina linahifadhiwa) akituhumiwa kuhusika kuchoma moto maduka likiwemo duka lake akiwa na lengo la kutaka kujipatia faida kupitia bima ya biashara yake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Hamis Issah amesema Mfanyabiashara huyo anatuhumiwa kutekeleza tukio hilo April 1 mwaka huu kwenye milango inayomilikiwa na Jumuiya ya Wanawake wa CCM UWT Wilaya ya Njombe baada ya kuhamisha bidhaa zake lengo likiwa ni kutaka kunufaika na bima aliyokuwa analipia.

"Kwenye hili tukio kwenye vibanda takribani 7 mali zake ziliteketea na aliyefanya hivi tumemkamata na atafikishwa Mahakamani na alifanya hivyo kwa tamaa zake binafsi akijua hawezi kugundulika na alikuwa na lengo ajipatie faida lakini sasa hivi faida imekuwa hasara" ——— Kamanda Issah.
Screenshot_20230413_185238.jpg
 
Shirika la Ndege la Air Tanzania limesema linapitia changamoto za mabadiliko ya ratiba za ndege kutokana na uchache wa ndege zilizobaki uliosababishwa na kuchelewa kwa upatikanaji wa injini mbadala za ndege mbili za Airbus A220-300 kutokana na injini zake kuwa na matatizo.

“Injini mbadala, zinazotakiwa kutolewa na Mtengenezaji Pratt & Whitney (P&W), zilitarajiwa kuwasili mwanzoni mwa mwezi Aprili 2023 kutokana na changamoto hizi, tunalazimika kutoa huduma kwa ratiba inayobanana sana ili kukidhi mahitaji makubwa ya wateja wetu”

“Wakati tunashughulikia changamoto hizi kwa haraka, tunaomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza, Kampuni ya Ndege itaendelea kuhakikisha inatoa huduma bora ili kufikia matarajio ya Wateja wetu” ——— imeeleza taarifa ya Air Tanzania.
Screenshot_20230413_185439.jpg
Screenshot_20230413_185501.jpg
 
Shirika la Umeme TANESCO limesema kuwa mvua zinazoendelea kunyesha katika Mikoa ya Mogororo, Tanga na Dodoma zimesaidia ongezeko la maji katika Bwawa la Kidatu, New Pangani, Mtera na Hale.

Akiongea na Waandishi wa Habari Kidatu Mkoani Morogoro, Meneja Mawasiliano na Uhusiano kwa Wadau wa TANESCO Elihuruma Ngowi, amesema kwa mwezi mmoja sasa Nchi nzima kumekuwa hakuna upungufu wa umeme (mgao) ambapo hali hiyo imechangiwa na mvua zinazoendelea kunyesha.

"Kama Nchi hatuna upungufu wa umeme kwa takribani zaidi ya mwezi mmoja sasa, mahali ambapo kuna upungufu au kukosekana kwa umeme hiyo inachangiwa na matengenezo kinga ambayo yanafanyika au matengenezo makubwa ya mitambo yetu yanayofanyika lakini siyo kwasababu ya upungufu wa umeme" ——— Ngowi.
Screenshot_20230413_185636.jpg
 
Mh mbona me napata pata auntie bora umerudi tena leo nilitaka nije WhatsApp tar 30 jiandae tukae hata nusu saa nina ratiba ya kulala mjini

Saa kumi nina kikao mikocheni nikitoka uko ndio nataka tuonane kama una mda lakini halafu nitaelekea magomeni kwenye birthday party ya dada yangu mmoja
Mimi sipati Auntie...

Hata picha hazifunguki...Shidah!!!

Kuna Uzi nimeona huko na Mello akawa anatoa Ufafanuzi....nimefanya kama alivyoeleza ila sioni mabadiliko...
 
Mh mbona me napata pata auntie bora umerudi tena leo nilitaka nije WhatsApp tar 30 jiandae tukae hata nusu saa nina ratiba ya kulala mjini

Saa kumi nina kikao mikocheni nikitoka uko ndio nataka tuonane kama una mda lakini halafu nitaelekea magomeni kwenye birthday party ya dada yangu mmoja
Naaaam....Naaam...Auntie..

Mambo napendaga mimi hayoo....
Hiyo siku nadhani hiyo nusu saa haitatutosha....Unajua

Maelekezo yafuate Watsap basi Auntie...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom