Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230319_063813_Opera%20Mini.jpg
 
Farhan Jr

Mwisho wa filamu nzuri ya INTO THE BADLANDS, Lamata Leah wa soka ameicheza pale kwa Anko Benny wa Mkapa, walisema flash ina virus ikaletwa disc, wakasema umeme changamoto ikawashwa jenereta tukisubiri Stigglers Gorge.

CLATOUS CHOTA CHAMA, picha ya sanaa inayotembea ni kama maisha yake yote ameyachora Masoud Kipanya The Artist, ipe wewe tafsiri lakini kwake ni rahisi tu ni Champions League ila uwezo ni ule ule kama FA ama Simba Day, another day simply another magic.

From Magic Fingers to you! Alisema Peter Drury! Yes its vintage beyond forgery! Kwenye ukanda wa dunia ya tatu ulizaliwa kugawa burudani! Mungu hakutaka kutupa mzigo tusioweza kuubeba! Nje na kudaiwa kodi na VICOBA na Bodaboda basi tuna Clatous Chama.

Clatous Chama kwenye darasa la Fizikia niliwasikia wakisema ni Step Up and Step Down transformer yeye ndie anaamua Simba ichezaje! CCC kwenye Theolojia wanasema Mtoto usimnyime mapigo, that one for Wachambuzi, lingine la Horoya na moja la Simba

SIMBA Mfalme wa mwituni, Simba maarufu kutoka mbuga ya Serengeti alitaka kuikumbusha Africa kuhusu maajabu ya dunia, hivi ndivyo ambavyo Mfalme wa mwituni anaurejesha Ufalme! Naweza kuhesabu namba mpaka saba, check that!

SADIO KANOUTE PUTIN, umeongoza mashambulizi ya kuidai Jamhuri leo hii! Si ni wewe unatakiwa ICC? Yes kesi acha iendelee lakini uwanjani lazima kazi iendelee, chuma mbili kambani! You beamed as one for the fans and one for the haters.

PROFESA JANABI hapo Muhimbili ikikupendeza hii clip ya mechi ya leo inaweza kutumika kama ganzi inapobidi, hakuna starehe kama ya Lunyasi! Kaka Nsekela hapo CRDB tuje nayo kuombea mkopo na hata wakubwa hapo TIGO hata ofa ya bando bure kwa siku saba

A trademark night! Proper Football show! THE LION OF SERENGETI IS TALKING TO AFRICA SIMBARCELONA.

The City is RED and WHITE! Literally the ADMN is crying of joy

Screenshot_20230319_163106_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

CLATOUS CHOTA CHAMA, leo ni Jumapili Machi 19, Dominika ya 4 ya Kwaresma na leo Mama Kanisa anatukumbusha kuhusu Kuponywa kwa Upofu (Healed of Blindness)!

Nimshukuru sana Mama Kanisa kwa somo hili la leo! Ngoja niwape kidogo kuhusu somo hili, nasi tunataka kuwaponya watu upofu leo hii! Kuhusu Mchezaji bora wa muda wote kuwahi kutokea nchini.

Somo linaanza na kuwa kuna Kijiji alizaliwa kipofu, yeye kila ifikapo jioni huchukua taa yake kukatisha kwenye msitu mmoja mkubwa sana, siku moja kuna Mtu akamuuliza!

“Wewe ni kipofu kwanini unabeba taa?” Nae akamjibu kuwa anabeba taa ili wao wanaoona wasigongane na yeye kwakuwa haoni, tazama ukuu wa heshima na busara hii.

Ni kama sisi tunaposema CLATOUS CHAMA ndie MCHEZAJI BORA KUWAHI KUTOKEA, kwakuwa tunafahamu macho yenye afya hayawezi kuona yote, trust me! Nasi tunataka mbebe taa ili tusigongane, hizo taa ziwe takwimu kama hazipo basi msitembee wakati wa jioni.

Kuna upofu mwingine pia ambao umejikita katika mizani ya ulimwengu,: pesa, mafanikio, kazi, mapenzi, afya na ugonjwa, ujana na uzee! Nasi kwa kufahamu hayo tunaendelea kuwakumbusha bila kuchoka kuhusu CHAMA.

Mchezaji wa kwanza kufunga mabao matatu kwenye hatua ya makundi kutoka timu za Tanzania, Mchezaji wa kwanza eneo la Kiungo kufikisha mabao 14 kwenye Champions League, Mchezaji wa kwanza kutoka Zambia kufanya hivyo Champions League na anaongoza mabao manne na assist moja mbele ya wote Afrika.

Upofu ni nini? Upofu” ni kushindwa kuona mkono wa Mungu ukifanya kazi kati yetu. Tunakazana kutafuta miujiza ya Neema za Mungu zinazo onekana kwetu na kwa wengine.

Hili ni somo la kwanza Jumapili ya leo! Makala bado zipo, Asante!

Niwatakie Dominika Njema Watu wa Mungu
Screenshot_20230319_163509_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

THE BRAIN CCC, 17 ways to success as opposed to 48 Laws of Power! Remember never to outshine this Football Master as so to the Football Commanding Law states:

Rule number one “Chama is never wrong”

Rule Number two “If Chama is wrong, refer to number one”

Born and raised in a Copper Belt Province a city called Ndola in the present day Zambia formerly known as Northern Rhodesia in Colonial era, his dream was to play football, copper in his head, football in blood.

Gamers use CCC17 as a cheat code! The Fantasy Boys tripled him as Captain and the CAF ADMN is technically making a bold statement, this Lad means business! Ice on his veins.

This CAF Champions League is proudly brought to you by TOTAL ENERGIES, but this Football show and brainy touches are proudly brought to you by MWAMBA WA LUSAKA, free of charge!

Its March before April Fools, its March after arsh Wednesday! Its Clatous Chama cooking it in Quaresma! We aint joking around we are just destined to the top, make that one a trademark statement.

The same night of Miss Tanzania Higher Learning Finals, the same night actually three hours before it CCC gave us a festival of football, Football Fiesta to call it, just a joy to watch.


THE GREATEST IS, THE GREATEST WAS, THE GREATEST WILL EVER BE @realclatouschama

Ya pili hii kwa ENGLISH VERSION

Screenshot_20230319_163645_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Urusi Vladimir Putin jana amefanya ziara ya kushtukiza katika rasi ya Crimea katika kuadhimisha miaka tisa tangu alipoinyakua kutoka Ukraine, Putin ameutembelea pia Mji wa Ukraine wa Mariupol unaokaliwa kimabavu.

Ziara ya Putin inajiri siku chache baada ya Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu ICC kutoa waranti wa kukamatwa kwake kwa uhalifu wa kivita, ikimtuhumu kwa uwajibikaji katika utekaji nyara wa watoto nchini Ukraine.

Ukraine inasema tangu kuanza kwa uvamizi huo Februari 2022, zaidi ya Watot 16,000 wa Ukraine walihamishwa kinyume cha sheria kuelekea Urusi.

Urusi imetupilia mbali uamuzi wa Mahakama hiyo na bado mapigano makali yanaendelea huko Donetsk hasa katika mji wa Bakhmut.
Screenshot_20230319_164603_OGInsta%2B.jpg
 
Polisi Mkoani Njombe imetoa tahadhari kwa Wafanyabiashara na Wakulima wanaobeba hela nyingi mikononi wakati wa kuzipeleka Bank au kukabidhiana baada ya kuuza mazao kutoa taarifa kwa Vyombo vya Usalama ili vitoe huduma ya Polisi ya kusindikiza kwa ajili ya usalama (Escort).

RPC wa Njombe Hamis Issah ameeleza hayo wakati akizungumza na kutoa elimu kwa Madereva wa malori pamoja na Madalali katika kituo cha magari ya mizigo kilichopo Edina Halmashauri ya Mji wa Njombe.

"Msikubali kubeba hela kwenye mifuko na siku ukiwa umebeba hela njoo tuambie kuwa nimebeba hela Mimi nitakupa Askari hiyo ruhusa ipo kuna sheria unachukua Askari akusindikize, nyie njooni na hata wakati mnawapa Wakulima hela Askari atakuwepo"
Screenshot_20230319_164802_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali ya Korea Kaskazini imedai kuwa takribani Raia 800,000 wamejitolea kujiunga au kujiandikisha katika Jeshi la Taifa hilo kwa dhamira ya kupambana na Jeshi la Marekani kwa kile wanachodai kuchoshwa na uchokozi wa Marekani usioisha.

Takriban Wanafunzi na Wafanyakazi 800,000 kwa siku ya Ijumaa pekee walifunguka na kusema walitaka kujiandikisha na kulitumikia Jeshi la Taifa ili kukabiliana na Marekani, Gazeti la Serikali la Korea Kaskazini Rodong Sinmun limeripoti Wikiendi hii.

Madai hayo yamekuja baada ya Korea Kaskazini kurusha kombora la Hwasong-17 (ICBM) kujibu mazoezi ya kijeshi ya Marekani na Korea Kusini yanayoendelea, Makombora ya aina ya ICBM ya Korea Kaskazini yamepigwa marufuku chini ya maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na zoezi hilo lililaaniwa na Serikali za Korea Kusini, Marekani na Japan.

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un anaishutumu Marekani na Korea Kusini kwa kuongeza mvutano baina yao kwa kitendo cha wao kufanya mazoezi ya kijeshi pamoja.
Screenshot_20230319_164048_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo akiwa Dar es salaam katika Sherehe za maadhimisho ya miaka miwili ya Serikali ya awamu ya sita iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), amesema bado zile milioni tanotano za kununua magoli ya Simba na Yanga kwenye mechi za kimataifa zipo.

“Niwapongeze Wanangu wa Yanga na Simba kwa kuitumia vizuri fursa niliyowapa ya goli moja milioni 5 wameitumia vizuri sana, kwa hesabu nilizonazo nadhani Yanga wameshalamba milioni 30 na Simba jana milioni 35 na nyuma nadhani walikula 5 kwahiyo niwapongeze kwa kuitumia vema fursa hii, niwapongeze na ni imani yangu kwamba ile kasi iliyopo miguuni ya milionk 5 kwa goli itaendelea kuwepo huko mbele milioni 5 zitakapoondoka”

“Kwa sasa hivi niwahakikishie wale waliokuwa wakitania jana, niliona utani nampigia Msigwa namwambia ‘ebu maliza mpira haraka mimi pesa zimeisha’, nataka niwahakikishie kwamba Mama bado anazo wekeni mipira kwenye wavu jengeni jina la Nchi yetu, bado zipo” ———Rais Samia.
Screenshot_20230319_164802_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom