Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230304_073812_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20230304_073829_Opera%20Mini.jpg
 
@AhmedAlly_ alianza kufanya hamasa kuita mashabiki uwanjani kwa kuzunguka mitaa tofauti ya Dar kwa kutumia ‘kispika’ akafanikiwa.

Baadae tukaona @AliKamwe na maandamano kule Mabagala na baadae jogging na yeye pia akafanikiwa kwa upande wake.

Jana Ally kamwe aliendelea na hamasa kuelekea mchezo wao dhidi ya Real Bamako, tumeona watu wanakula ugali kwa sukari pale maeneo ya Buguruni.

Leo Ahmed Ally amekuja tena na kitu kipya, safari hii amesema hatazunguka na kispika chake kakini amewaita mashabiki wa Simba wakutane Coco Beach ‘Wenye nchi Beach Party’.

Ahmed anasema mashabiki wanakutana, wanakula upepo, wanafahamiana, wanafurahi na kukubaliana namna bora ya kushangilia siku ya mechi lakini vilevile kutakuwa na wauzaji wa tickets za mechi yao dhidi ya Vipers.

Alichofikiria Ahmed naona ni kitu kizuri na vitu vipya vinaingia kwenye mpira wetu! Pata picha siku hiyo kunakuwa na sound nzuri pale Coco Beach halafu kunakuwa na wasanii kadhaa kwa ajili ya kutengeneza vibe kwa mashabiki.View attachment 2536490
Waige na hii

Sent from my vivo 1906 using JamiiForums mobile app
 
Watu watatu wamepoteza maisha na wengine wanne kujeruhiwa baada ya mapema leo Lori kufeli breki wakati likiteremka Mlima na kugonga Bajaji mbili ambazo zilikuwa mbele yake katika eneo la Mlima Ipogolo Iringa Mjini.

Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Ipogolo, Mathias Maheri amethibisha kuwapokea Watu watatu wakiwa tayari wamepoteza maisha pamoja majeruhi wanne (Wanaume wawili, Mwanamke mmoja na Mtoto mmoja) ambao wote baada ya kupatiwa matibabu wameruhusiwa kutoka kituoni hapo.

Mashuhuda wamesema baada ya Dereva kugonga Bajaji hizo alikimbia lakini Polisi kwa kushirikiana na Wananchi walimkamata na kwasasa yupo Kituo cha Polisi, jitihada za kumpata RPC Iringa kwa taarifa zaidi zinaendelea.
Screenshot_20230305_043917_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan leo amefunga Mkutano wa Faragha wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu Jijini Arusha ambapo amewataka Viongozi wasahau yaliyopita na wagange yajayo na amewataka pia wajitahidi kupandisha walio chini yao ili na wao wapate fursa ya kupanda madaraja zaidi.

“Yaliyopita sindwele tukagange yajayo, Wazungu wanasema sio kila dhoruba inakuja kuharibu maisha yako, dhoruba nyingne zinakuja kutengeneza njia kwa ajili ya maisha yako, kwahiyo madhoruba mengine tuliyowapa huko nyuma yamekuja kusafisha njia ya kwenda huko, sasa Mjengaji njia na atakayepanda juu ni wewe mwenyewe”

“Wanasema ukitaka kupanda daraja pandisha Mtu ili nawe upande daraja, usipopandisha Mtu utasimama palepale lakini ukipandisha Mtu atakuwa chini yako wewe upo juu, kwahiyo ukitaka kupanda daraja pandisha Mtu kwaza halafu panda wewe”
Screenshot_20230305_044057_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan leo amefunga Mkutano wa Faragha wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu Jijini Arusha ambapo amewataka Viongozi kujiamini wakati wa kutekeleza majukumu yao na wanapofanya maamuzi.

“Tutekeleze majukumu lakini tutoe taarifa za utekelezaji na pia tuweke mbele maslahi ya Taifa kabla ya maslahi binafsi, mlioko hapa mmeaminiwa hatuna budi kujiamini, kuamini uwezo wetu tulionao, ukijiamini utafanikiwa, usipojiamini unajiwekewea vikwazo”

“Unapofanya maamuzi sema haya ni maamuzi yangu na nimeamua haya kutokana na hili na hili na uwe tayari kusimama kutetea maamuzi yako”
Screenshot_20230305_044619_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan leo amefunga Mkutano wa Faragha wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu Jijini Arusha ambapo amewataka Viongozi baada ya mkutano huo wakaache migongano, kusengenyana, kuhujumiana, uvivu na uzembe ili wakaaminiane na kushirikiana kufanya kazi za Watu “Tukaache pia dharau tusiwadharau Wananchi wala tusidharauliane wenyewe kwa wenyewe”

“Kosa kubwa tunalolifanya Serikalini ni kudhani mawasiliano yamefanyika hatuhakikishi, kuna tofauti kati ya taarifa na mawasiliano, tukafanye mawasiliano tusitoe taarifa, usidhani jambo lako limefika hakikisha”
Screenshot_20230305_044719_OGInsta%2B.jpg
 
Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limemtangaza Adel Amrouche Raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria kuwa Kocha Mpya wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars.

Adel ambaye atakuwa akilipwa mshahara na Serikali wakati wote wa mkataba wake amewahi kuwa Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Kenya Harambee Stars na kuiongoza kucheza michezo 20 mfululizo bila kupoteza.

Pia Adel amewahi kuwa Kocha wa Burundi, Botswana, Equatorial Guinea, Libya na Yemen huku akiwa kuwa Mkurugenzi wa micheza wa FC Brussels ya Ubelgiji.
Screenshot_20230305_044825_OGInsta%2B.jpg
 
Mstahiki Meya wa Kinondoni, Songoro Mnyonge amesema kampeni ya kutokomeza Madanguro (Nyumba ambazo Madada poa wanazitumia kuuza miili yao) aliyoianza ataendelea nayo huku akiwataka Wamiliki wa nyumba hizo wajisalimishe ambapo kwa Mwananyamala, Msasani na Uwanja wa Fisi pekee kuna Madanguro 324.

Amesema Madada Poa hao wanajiuza hadi kwa Tsh Elfu 2 tena hadharani wakati wa mchana kitendo ambacho kinachangia ongezeko la UKIMWI na mmomonyoko wa maadili hadi kwa Watoto kwakuwa Madanguro hayo yapo maeneo ya makazi ya Watu “Nimebaini Madada Poa huchangisha fedha na kuwahonga baadhi ya Viongozi ili wasiwazuie kufanya kazi, Viongozi hao wakibainika watachukuliwa hatua kali”

Songoro amemuomba Waziri Dorothy Gwajima kulitazama jambo hilo kwa jicho la huruma na kuweka nguvu katika kukomesha Madanguro “Nilishtukiza Mwanyamala kuna Madanguro 150 yapo Watu wamegeuza nyumba zao kuwa za biashara za Wadada kuuza miili yao, Uwanja wa Fisi (Tandale) yapo 139, Msasani yapo 35 kwahiyo Madanguro jumla 324 kwa maeneo hayo pekee”

“Kuna Taasisi ikaona pana janga ikaweka mashine ya condom ili Mtu awe anabonyeza anachukua na zinaisha shughuli inafanyika kweli, tumewataka wenye nyumba wajisalimishe, hivi Dada ambaye anakaa asubuhi nusu uchi nje Kijana wangu anatoka Shule kama wanachukua hadi Elfu 2 na kuna Mzazi anampa Mwane Elfu 3, anashindwa kumrubuni Mwanangu aingie kule akamfundishe vitu ambavyo sio?”
Screenshot_20230305_045018_OGInsta%2B.jpg
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya, kimemuonya aliyekuwa mbunge Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) kuacha kutoa maneno ya kejeli dhidi ya Spika wa Bunge, Dk Tulia Ackson na kwamba kama chama wanamsubiri Oktoba 2025.

Katibu Mwenezi CCM Mkoa, Bashiru Madodi ametoa kauli hiyo leo Jumamosi, Machi 4,2023 katika Viwanja vya Ruanda nzovwe wakati Spika wa Bunge na Mbunge wa Mbeya Mjini akiwezesha kiuchumi wanawake 1,000 kupitia taasisi yake ya Tulia Trust.

“Februari, 25 mwaka huu kwenye mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hili alisimama na kutoa maneno ya kejeli ikiwepo utiaji saini miradi ya barabara njia nne na maji kutoka mto Kiwira kuwa ilianza mchakato wakati yeye akiwa na ridhaa ya kuwatumikia wanambeya ,” amesema.
Screenshot_20230305_045148_OGInsta%2B.jpg
 
Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) kimesema licha ya wanachama wengi kujitokeza kuchukua fomu kuwania nafasi ya mwenyekiti wa chama hicho, uongozi wa chama hicho umesema kinachochelewesha kumpata mtu wa kuziba nafasi hiyo, ni ukata wa kifedha.

Uchaguzi wa kwanza ulipangwa kufanyika Februari 28, lakini uliahirishwa na sasa unatarajiwa kufanyika Machi 06 mwaka huu ili kuziba nafasi iliyoachwa na Augustino Lyatonga Mrema, aliyefariki dunia Agost 21 mwaka jana akiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.

Akizungumza na Mwananchi, Katibu Mkuu wa chama hicho, Richard Lyimo alisema ratiba ya uchaguzi huo imepelekwa mbele kutokana na changamoto za kibajeti.

Screenshot_20230305_045301_OGInsta%2B.jpg
 
Mwanamke mmoja Ubelgiji aliyetambulika kwa jina Genevieve Lhermitte ambaye aliwaua watoto wake watano ameuwawa kwa ombi lake mwenyewe baada ya miaka 16 toka kufanya tukio hilo.

Lhermitte alimuua mwanawe wa kiume na mabinti wanne, wenye umri wa miaka mitatu hadi 14, katika mji wa Nivelles, Ubelgiji Februari 28, 2007, wakati baba yao hayupo.

Mwanamke huyo alijaribu kujitoa uhai lakini akashindwa, na kuishia kupiga simu za dharura kwa usaidizi wa polisi.

Mama huyo mwenye umri wa miaka 56 alihukumiwa kifungo cha maisha jela mwaka wa 2008, kisha kuhamishiwa hospitali ya magonjwa ya akili mwaka wa 2019.

Nchini Ubelgiji sheria inaruhusu watu kuchagua kuuawa ikiwa watachukuliwa kuwa na matatizo ya kisaikolojia "yasiyovumilika", na si tu mateso ya kimwili, ambayo hayawezi kuponywa.
Screenshot_20230305_045409_OGInsta%2B.jpg
 
BAADA ya kukaa kimya muda mrefu bondia Hassan Mwakinyo sasa atapanda ulingoni Aprili 22 kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma kupigana na bondia kutoka Afrika Kusini.

Pambano hilo limeandaliwa na promota maarufu wa kike nchini, Sophia Mwakagenda wa kampuni ya Lady in Red Promotion.

Mwakagenda alisema wanatarajia kuwa na pambano la kusisimua siku hiyo kwani wanatarajia kushirikisha mabondia nyota wa kiume na wa kike.

Kwa upande wake, Mwakinyo alisema kuwa anatarajia kurejea kwa nguvu zote pamoja na kutoingia ulingoni kwa miezi zaidi ya mitano. Alisema kuwa amejiandaa vilivyo katika pambano hilo na ataonyesha uwezo wake.

Screenshot_20230305_045540_OGInsta%2B.jpg
 
.
—KOCHA wa AS Roma, Jose Mourinho ana kadi nyekundu (2) nyingi zaidi ya mchezaji yeyote wa Serie A msimu huu
Screenshot_20230305_045655_OGInsta%2B.jpg
 
CAF CHAMPIONS LEAGUE
.
FT: AL AHLY 3-0 COTTON SPORTS
02’—️ Sherif
40’—️ Kondouci
90’—️ Khalil
.
Msimamo Kundi B
1. Mamelodi —(3)— 7pts
2. Al Hilal —(3)— 6pts
3. Al Ahly —(3)— 4pts
4. Cotton —(3)— 0pts
Screenshot_20230305_045800_OGInsta%2B.jpg
 
THE GUNNERS. HAWASHIKIKI
.
FT: ARSENAL 3-2 BOURNEMOUTH
01’—️ Billing
57’—️ Senesi
62’—️ Partey
70’—️ Ben White
90+7’—️ Nelson
.
Mbio za Ubingwa
1. Arsenal (26) — 63pts
2. Man City (26) — 58pts
3. Man United (24) — 49pts
Screenshot_20230305_045906_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom