Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230307_064611_OGInsta%2B.jpg
 
Shaffih Dauda

Kijana anapaswa kurejea uwanjani kucheza mpira, Washauri na Wasimamizi wake mpira ni kazi yake kijana na anapaswa kucheza, sitaki kuamini kama protocol hazifahamiki kama nilivyozungumza redioni ila mfumo wa mpira una sauti mbili moja sahihi na moja ya uongo iliyokaa kimaslahi binafsi.

Exceptional talent indeed ila anastahili watu sahihi tu, anachotaka ni kitu kidogo sana na njia yake ni rahisi sana.
Screenshot_20230307_064845_OGInsta%2B.jpg
 
Shaffih Dauda

Kama ambavyo huwa nasema siku zote Kibu Denis akiwa fit hapaswi kukaa bench pale Simba, ni aina ya wachezaji ambao wanahitajika sana kwenye soka la kisasa anakupa 100% ya kile ambacho Mwalimu anakihitaji kutoka kwake.

Simba will miss Kibu wakati huu yupo kwenye majeraha.
Screenshot_20230307_064948_OGInsta%2B.jpg
 
MAJANGA! BISHOO NJE HADI MSIMU UJAO
.
PSG imethibitisha kuwa supastaa wake, Neymar Jr atazikosa mechi zilizosalia za kufungia msimu kwa timu hiyo, kwani anatarajiwa kuonekana tena uwanjani August ikiwa ni msimu ujao.

Screenshot_20230307_065053_OGInsta%2B.jpg
 
Kocha mpya wa Taifa Stars, Adel Amrouche ni muumini wa soka la pasi nyingi maarufu kama soka la kitabuni linalotandaza mpira chini zaidi kuliko kutubua hovyo, mfumo ambao kwa mashabiki wa soka wa Tanzania wanapenda kuita soka biriani.
.
Anatumia zaidi mfumo wa 4-2-3-1 ambao unaifanya timu inapopoteza mpira kuwa na wachezaji sita wanaokaba na inaposhambulia inakuwa na wachezaji sita pia. Anapenda zaidi kumtumia straika mmoja huku akiwa na mawinga wenye kasi.
.
Mfumo uliyowasumbua Wanaigeria walipocheza na Harambee Stars katika fainali ya Chalenji 2013 iliyowapa Wakenya ubingwa waliousotea kwa miaka karibu 11.
Screenshot_20230307_065154_OGInsta%2B.jpg
 
PEP Guardiola anaamini Vincent Kompany atakwenda kuwa kocha atakayechukua mikoba yake huko Manchester City.
.
Beki huyo nahodha wa zamani wa Man City, Kompany atarudi uwanjani hapo kukabiliana na timu hiyo yake ya zamani, wakati atakapoingoza Burnley kwenye mchezo wa robo fainali ya Kombe la FA baadaye mwezi huu.
.
Na kutokana na kazi nzuri anayofanya huko Turf Moor hiyo ina maana anapita kwenye hatua nzuri za kuelekea kuwa kocha wa Man City kwa mujibu wa kocha wa sasa wa miamba hiyo ya Etihad.
Screenshot_20230307_065239_OGInsta%2B.jpg
 
Taarifa zinaeleza klabu ya TP Mazembe imeweka nguvu kutaka kumpata kocha mkuu wa Yanga, Mtunisia Nasreddine Nabi.
.
Tajiri Moise Katumbi wa TP Mazembe anadaiwa kumtaka kocha huyo baada ya kufanya usajili mkubwa ambao anaona bado haujazaa matunda kimataifa.

Screenshot_20230307_065413_OGInsta%2B.jpg
 
Baada ya dili lake la kujiunga na Arsenal kufeli katika dirisha lililopita, kiungo wa Brighton Moises Caicedo ameripotiwa kuafiki mkataba mpya wa kuendelea kubaki Brighton ambao utamfanya alipwe mara 10 ya mshahara wake wa sasa wa Pauni 5,000 na hivyo atavuta Pauni 50,000 (Sh 140.7 milioni) kwa wiki.
.
Staa huyo wa kimataifa wa Ecuador alitaka kuondoka ili kupata maslahi bora zaidi kama ilivyo kwa Zanzibar finest anayepambania kuachana na mlo wa Ugari na sukari.
Screenshot_20230307_065516_OGInsta%2B.jpg
 
KOCHA VIPERS: TUTATUMIA MBINU ZA RAJA
.
VIPERS muda wowote asubuhi hii watatua Dar, Na sasa kocha wao amefichua baada ya kuisoma Simba mbele ya Waarabu ameamua kubadili mfumo kwa timu hiyo kisha kuwalisha nyota wake mbinu za kuimaliza Simba kesho Kwa Mkapa kama ilivyonyooshwa na Raja.
.
“Kesho tutakuwa na mifumo mingi na italenga maeneo yote kuanzia safu ya ulinzi hadi ushambuliaji, sihitaji kuona Vipers inakuwa timu ya mwisho tutafanya kama Raja Casablanca kushinda ugenini.” Kocha wa Vipers, Beto Bianchi.

Screenshot_20230307_065616_OGInsta%2B.jpg
 
MBAPPE WA MALI KUTUA YANGA
.
Taarifa zinaeleza dakika 52 alizocheza winga wa Bamako Cheickna Diakite ‘Mbappe’ mwenye umri wa miaka 18 dhidi ya Yanga zimemfanya wakati wowote anaweza kuwa staa mpya wa Jangwani kwani kwa sasa amebakiza hatua moja tu za mechi ya marudiano Jumatano uwanja wa Mkapa.
.
Yanga ikiwa ugenini dhidi ya Bamako mabosi wake walivutiwa na kazi ya Diakite aliyewasumbua mabeki wa Yanga katika mchezo huo ulioisha kwa sare. Baada ya mchezo huo bosi huyo wa Yanga aliteta na staa huyo kisha kuchukua taarifa zake juu ya mkataba wake na Bamako kabla ya kufanya uamuzi.
Screenshot_20230307_065707_OGInsta%2B.jpg
 
Taarifa zinaeleza klabu ya TP Mazembe imeweka nguvu kutaka kumpata kocha mkuu wa Yanga, Mtunisia Nasreddine Nabi.
.
Tajiri Moise Katumbi wa TP Mazembe anadaiwa kumtaka kocha huyo baada ya kufanya usajili mkubwa ambao anaona bado haujazaa matunda kimataifa.

View attachment 2540002
Huyo Katumbi atulie. Au akamchukue Mgunda 😅😅😅
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom