Makapuku Forum

Makapuku Forum

Aliyewahi kuwa Sheikh mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania Sheikh Alhad Mussa Salum amekemea na kulaani mapenzi na ndoa za jinsia moja.

Sheikh Mussa amekemea hilo Dodoma kwenye siku ya maridhiano kitaifa leo March 03,2023 ambapo amesema "Shetani mwenyewe hafanyi hayo tena wanaita ndoa za jinsia moja hapana, huo ni uchafuzi wa jinsia moja tusiruhusu na sisi Viongozi wa Dini tutaendelea kulaani maana hata Rais wetu haruhusu vitendo hivi"
Screenshot_20230304_045530_OGInsta%2B.jpg
 
Ndoa ya Mwanasiasa, David Kafulila na Jesca Kishoa imevunjwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke kupitia Kituo Jumuishi cha Huduma za Kimahakama, Mirathi na Ndoa.

Katika shauri hilo namba 217 la mwaka 2022 mpeleka maombi ambaye ni Kishoa kupitia Wakili wake Eden Kilatu ameiomba Mahakama ione ndoa yake na David Kafulila imevunjika kiasi cha kutorekebisha, hivyo ivunjwe kwani walitengana tangu mwaka 2019.

Katika hukumu hiyo ambayo imetolewa na Hakimu Mwandamizi Swai S.O ameeleza kuwa hana mashaka kuwa ndoa hiyo imevunjika kiasi cha kutorekebishika chini ya kifungu 107 (2) (f) cha sheria ya ndoa.

“Kwa msingi huo amri ya kuivunja ndoa na talaka inatolewa.
Sambamba na hilo, Watoto wataishi chini ya uangalizi wa Mama yao, Kafulila atakuwa na haki ya kuwaona na kuwa na Watoto wake mwishoni mwa juma na vipindi vya likizo za masomo”

Pia kupitia nakala ya hukumu hiyo imeeleza kuwa chini ya kifungu 129 cha Sheria ya Ndoa, mjibu maombi anawajibika kutoa matunzo ya Watoto kikamilifu ikiwe ada za Shule ambazo zilipwe kwa uwiano linganifu (asilimia 50) kwa kila Mzazi katika Shule watakazokubaliana pamoja.

Ndoa hiyo iliyofungwa Aprili 22, 2014 ilivunjwa rasmi Februari 20, 2023 baada ya Wanandoa hao kutengana tangu mwaka 2019.
Screenshot_20230304_050111_OGInsta%2B.jpg
 
Meneja wa Kiwanja cha Ndege cha Arusha, Eng. Elipid Tesha, amesema kukamilika kwa ujenzi wa jengo la abiria katika kiwanja hicho kutaongeza mapato ya kiwanja kutoka Tsh. Bilioni 2.8 hadi kufikia Tsh. Bilioni 6 kwa mwaka.

Akiongea mbele ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa ambaye alifika kukagua maendeleo ya ujenzi huo, Tesha amesema kukamilika kwa jengo hilo kutaruhusu kuhudumia abiria laki tano hadi sita kwa mwaka ambapo kwa sasa jengo lililopo linahudumia abiria laki mbili tu kwa mwaka.

Eng.Tesha amemuhakikishia Waziri Prof Mbarawa kuwa TAA itakamilisha jengo hilo kwa kuzingatia thamani ya fedha na ubora.

Jengo la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Arusha linagharimu kiasi cha Tsh. Bilioni 2.8 na limeshafikia asilimia 75 na linatarajiwa kukamilika mwezi Aprili mwaka huu.
Screenshot_20230304_050200_OGInsta%2B.jpg
 
Staa wa Soka kutokea nchini Argentina Lionel Messi (35) ametumiwa barua ya vitisho baada ya Watu wenye silaha kushambulia duka kubwa linalomilikiwa na Familia ya Mke wake Antonela Roccuzzo (35) jijini Rosario, nchini Argentina, AFP wanaripoti.

Kwa mujibu wa maelezo ya Mashuhuda wa tukio hilo lililotokea mapema jana saa tisa alfajiri, Watu wawili waliokuwa kwenye pikipiki walifyatua takriban risasi kumi na nne kwenye madirisha ya duka la Unico liliko jijini Rosario.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi hakuna aliyejeruhiwa katika eneo la tukio ingawa kulikuwa na uharibifu uliofanyika kwenye duka hilo huku barua ya vitisho iliachwa na ikiwa imeandikwa "Messi, tunakusubiri! Javkin ni muuza madawa ya kulevya, hatokusaidia.", Javkin ndiye Meya wa jiji la Rosario, nchini Argentina.

Meya wa Rosario Pablo Javkin ameripotiwa kufadhaika na tukio hilo huku akisema jambo hilo limeleta ongezeko la ghasia na wasiwasi jijini humo, mpaka sasa, Messi pamoja na mke wake Antonela Roccuzzo hawajazungumzia tukio hilo.
Screenshot_20230304_050259_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama nchini Belarus imemhukumu mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel, Ales Bialiatski kifungo cha miaka 10 jela.

Bialiatski amepatikana na hatia ya kusafirisha na kufadhili vitendo vinavyokiuka utaratibu wa umma, Shirika la Haki za Binadamu la Viasna limesema.

Wafuasi wa Bialiatski wanasema utawala wa kimabavu wa kiongozi wa Belarus Alexander Lukashenko unajaribu kumnyamazisha.

Bialiatski alikuwa mmoja wa washindi watatu wa Tuzo ya Amani ya Nobel ya mwaka 2022.
Screenshot_20230304_050424_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Dk Peter Mathuki aliyeambatana na ujumbe wake Ikulu ndogo ya Arusha.

Rais Samia amekutana na Dk Mathuki leo Ijumaa, Machi 03, 2023 jijini Arusha.

Screenshot_20230304_050519_OGInsta%2B.jpg
 
Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo ameiagiza Wizara ya Kilimo kuongeza vituo vya kuuzia mbolea kuanzia mwaka ujao ili wananchi wasitembee umbali mrefu kufuata huduma hiyo.

Chongolo amebainisha hayo leo akiwa katika Kijiji cha Mtinko kilichopo Wilaya ya Singida Vijijini wakati akitembelea shina namba 2 na kusikiliza kero za wananchi wa kijiji hicho.

Mkazi wa kijiji hicho, Amon Lunde ameeleza kwamba wanatembea umbali mrefu kufuata mbolea ya ruzuku na wakati mwingine wanalazimika kununua mbolea kwa bei ya juu ya hadi Sh100,000 tofauti na bei elekezi ya Sh70,000.

Screenshot_20230304_050652_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Uchukuzi na Ujenzi, Profesa Makame Mbarawa amesema kuwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mkoa wa Arusha wamejipanga kuhakikisha wanatumia mfumo maalumu wa kitasa janja (Smart Lock) kwenye nyumba zao ili kudhibiti uwepo kwa wadaiwa sugu ambao wamekuwa wakisumbua kulipa kodi ya nyumba.

Profesa Mbarawa ameyasema hayo leo Ijumaa, Machi 3,2023 alipotembelea mradi wa jengo la nyumba za TBA uliopo jijini Arusha.

Amesema kuwa, kumekuwepo na changamoto kubwa ya wadaiwa sugu katika nyumba hizo hali inayopelekea kufikishana hadi mahakamani kwa ajili ya kudai pango la nyumba ila kwa kutumia mfumo huo itakuwa ndio mwarobaini pekee wa suala hilo.
Screenshot_20230304_051034_OGInsta%2B.jpg
 
SIMBA na Yanga zimepumzika kwa muda kwenye pilikapilika za mechi za kimataifa, kwani kuanzia jana na leo zipo kwenye majukumu ya ASFC, lakini rekodi zinaonyesha nyota watano tu wazawa, akiwemo beki Dickson Job na kipa Aishi Manula wakikabana koo anga za CAF.

Job anayekipiga Yanga ndiye mchezaji pekee wa timu kuongoza kucheza kwa dakika nyingi katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, wakati Manula ni kati ya wachezaji wanne wa Simba waliokinukisha kwa muda mrefu kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

Wazawa hao ndio pekee waliotumika kwa muda mrefui wa vikosi vya timu hizo kila mmoja akiwa ametumika kwa jumla ya dakika 270 kutokana na kucheza kwa dakika 90 za mechi hizo zilizoiweka Simba katika nafasi ya tatu kwenye kundi walilopo na Yanga kushika nafasi ya pili Kundi D
Screenshot_20230304_051328_OGInsta%2B.jpg
 
Msemaji wa Simba, Ahmed Ally amesema wapinzani wao Vipers ya Uganda watawasili Dar Jumatatu Machi 6 kwa ajili ya mechi ya 4 hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika huku wakienda na kauli mbiu ya Nguvu moja kwa Mkapa hatoki mtu.
Mechi ya kwanza Simba ilishinda ugenini bao 1-0 na kusogea nafasi ya tatu sasa itasaka alama 3 nyingine ili iweze kusogea nafasi nzuri katika kundi C Ligi ya Mabingwa Afrika.
Screenshot_20230304_051834_OGInsta%2B.jpg
 
Msimu wa mwisho Yanga kucheza makundi ya Shirikisho ndio uliokuwa mbaya zaidi kwani timu hiyo haikufunga bao lolote ugenini, achilia mbali kupata japo pointi moja, tofauti na 1998 ilipofunga bao moja katika kipigo cha 2-1 kutoka na Asec Mimosas na 2016 ilijitutumua na kufunga mara mbili katika mechi ilizopoteza 3-1 kwa Medeama ya Ghana na TP Mazembe ya DR Congo.

Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi alikaririwa kabla ya kwenda Mali akisema "Rekodi zipo ili zivunjwe, lakini tunachopambana ni kuona timu inafika mbali zaidi katika michuano hii ya Afrika, bado tuna kazi kubwa".

Kama Yanga itafanya kweli mechi ya marudiano dhidi ya Bamako Jumatano ijayo itakuwa ni rekodi mpya kwa timu hiyo kukusanya pointi nyingi zaidi kwenye hatua hiyo, kwani itavuka zile nne ambazo ilizokuwa ikigota kwa misimu mitatu ya kucheza makundi michuano ya CAF.

Screenshot_20230304_052036_OGInsta%2B.jpg
 
Msimu wa mwisho Yanga kucheza makundi ya Shirikisho ndio uliokuwa mbaya zaidi kwani timu hiyo haikufunga bao lolote ugenini, achilia mbali kupata japo pointi moja, tofauti na 1998 ilipofunga bao moja katika kipigo cha 2-1 kutoka na Asec Mimosas na 2016 ilijitutumua na kufunga mara mbili katika mechi ilizopoteza 3-1 kwa Medeama ya Ghana na TP Mazembe ya DR Congo.

Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi alikaririwa kabla ya kwenda Mali akisema "Rekodi zipo ili zivunjwe, lakini tunachopambana ni kuona timu inafika mbali zaidi katika michuano hii ya Afrika, bado tuna kazi kubwa".

Kama Yanga itafanya kweli mechi ya marudiano dhidi ya Bamako Jumatano ijayo itakuwa ni rekodi mpya kwa timu hiyo kukusanya pointi nyingi zaidi kwenye hatua hiyo, kwani itavuka zile nne ambazo ilizokuwa ikigota kwa misimu mitatu ya kucheza makundi michuano ya CAF.

View attachment 2536485
 
KUNDI A BADO GUMU !!
.
FT: WYDAD 1-0 AS VITA
55’—️ Magema (Og)
.
Msimamo Kundi A
1. Wydad — 6pts
2. Petro Atletico — 4pts
3. JS Kabylie — 4pts
4. AS Vita — 3pts

Screenshot_20230304_052540_OGInsta%2B.jpg
 
.
"Sisi ndio waanzilishi wa kila kitu, safari hii 'Kispika' kitakuwa Coco Beach. Jumapili itakuwa Wenye Nchi Beach Party, tunakula bata tunafurahi, tunanunua tiketi na jezi kwa ajili ya Vipers Jumanne.” - Ahmed Ally.
Screenshot_20230304_052924_OGInsta%2B.jpg
 
@AhmedAlly_ alianza kufanya hamasa kuita mashabiki uwanjani kwa kuzunguka mitaa tofauti ya Dar kwa kutumia ‘kispika’ akafanikiwa.

Baadae tukaona @AliKamwe na maandamano kule Mabagala na baadae jogging na yeye pia akafanikiwa kwa upande wake.

Jana Ally kamwe aliendelea na hamasa kuelekea mchezo wao dhidi ya Real Bamako, tumeona watu wanakula ugali kwa sukari pale maeneo ya Buguruni.

Leo Ahmed Ally amekuja tena na kitu kipya, safari hii amesema hatazunguka na kispika chake kakini amewaita mashabiki wa Simba wakutane Coco Beach ‘Wenye nchi Beach Party’.

Ahmed anasema mashabiki wanakutana, wanakula upepo, wanafahamiana, wanafurahi na kukubaliana namna bora ya kushangilia siku ya mechi lakini vilevile kutakuwa na wauzaji wa tickets za mechi yao dhidi ya Vipers.

Alichofikiria Ahmed naona ni kitu kizuri na vitu vipya vinaingia kwenye mpira wetu! Pata picha siku hiyo kunakuwa na sound nzuri pale Coco Beach halafu kunakuwa na wasanii kadhaa kwa ajili ya kutengeneza vibe kwa mashabiki.
Screenshot_20230304_053038_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Shida ilianza pale watu muda wote waliamini YANGA wana shida kwenye suala la sheria, shida ni kwamba wengi waliishi kimazoea kuwa ikija suala la sheria basi Yanga watapoteza tu.

Bahati mbaya sana Yanga wanaweza kutaka kwenda beyond mfano huko huko CAS ama TFF wakaripoti kuwa kuna msukumo kutoka nje (Influence of third party) kwenye uamuzi wa Mchezaji wao, unafikiri itakuwaje?

Simple logic ni kuwa Our Brother Feisal kama inavyosemekana anakula ugali na sukari, Our Brother Feisal anaenda mazoezini na bodaboda lakini Our Brother Feisal ndie aliedepost MILLION 100 kwenye account ya Yanga.

Kwahiyo kwa simple logic hiyo hiyo Our Brother Feisal ana uwezo wa kulipa MILLION 100 lakini bado akala ugali na sukari? Katika kitu ambacho FIFA wanapiga vita ni THIRD PARTY ni sumu mbaya kwenye biashara ya mpira haswa uhamisho wa wachezaji.

Tuwe smart! Kama Mchezaji anahitajika popote pale basi fikeni kwa Yanga watawapa valuation yake kama ambavyo kifungu cha 16(2) kinavyosema kuhusu release clause yake, ni kitu simple sana.

You need Our Brother Feisal? Wafuate Yanga mnamalizana hata sasa hivi naamini wapo tayari kumwachia, we love our Brother you know! We wish whats best for him.
Screenshot_20230304_053248_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom