Mfanyabiashara kutoka Sekta ya Viwanda nchini Nigeria Aliko Dangote, ambaye utajiri wake umeshuka kwa kiasi cha dola milioni 400 kufikia dola bilioni 13.5, bado ameendelea kuwa Mtu Tajiri zaidi kwa mwaka wa 12 mfululizo akifuatiwa na tajiri kutokea Afrika Kusini Johann Rupert ambaye anashikilia nafasi ya pili kwa mwaka wa pili mfululizo, licha ya kushuka kwa Dola Milioni 300 hadi kufikia Bilioni 10.7.
Kwa mujibu wa ripoti ya jarida la Forbes, Watu matajiri zaidi Afrika wamepoteza USD Bilioni 3.1 wote kwa pamoja katika muda wa miezi 12, Mabilionea 19 wa kutokea Africa wana thamani ya wastani ya USD Bilioni 81.5 ikionesha kupungua kutoka USD Bilioni 84.9 mwaka mmoja uliopita.
Jarida la Forbes limemuorodhesha Mfanyabiashara kutokea nchini Tanzania Mohammed Dewji, akishikilia nafasi ya 13 kwenye list hiyo ya Watu Matajiri zaidi Afrika huku pia akionekana akishikilia nafasi ya 1,913 duniani akiwa na utajiri wa Dola Biliono 1.5, mwaka jana, Mo alishika nafasi ya 15.
Orodha ya Watu 15 Matajiri zaidi Africa ni 1.Aliko Dangote (Nigeria) - $13.5bn, 2.Johann Rupert (Africa Kusini) - $10.7bn, 3. Nicky Oppenheimer (Africa Kusini) - $8.4bn, 4. Abdulsalmad Rabiu (Nigeria) - $7.6bn , 5. Nasser Sawiris (Misri) - $7.3bn, 6. Mike Adenuga (Nigeria) - $6.3bn, 7. Issad Rebrab (Algeria) - $4.6bn, 8. Naguib Sawiris (Misri) - $3.3bn, 9. Patrice Motsepe (Africa Kusini) - $3.2bn, 10.Mohamed Mansour (Misri) - $2.9bn, 11. Koos Becker (Africa Kusini)- $2.6bn, 12.Strive Masiyiwa (Africa Kusini)- $1.9bn, 13.Aziz Akhannouch and family (Morocco) $1.5bn, 13. Mohammed Dewji (Tanzania) $1.5bn na 13.Youssef Mansour (Misri) $1.5bn.